: kwa kutumia mifano jarabati eleza kwa utondoti tofauti iliyopo baina ya isimu elekezi na isimu elezi


.
           Isimu ni ‘taaluma yauchunguzi wa lugha kisayansi’. Ipo taaluma kama vile ya Falsafa ambayo nayo inaweza kujishughulisha na uchambuzi wa masuala ya lugha lakini si kwa kutumia vigezo vya kisayansi. Wanaisimu huhakikisha kuwa wakati wa kutafiti na hatimae kuwasilisha matokeo ya utafiti wao wanatumia vigezo vya kisayansi hatua kwa hatua. Kwanza huchunguza na kukusanya data, Halafu, wanafanya malinganisho kabla ya kuunda nadharia na kuzipima nadharia na kuonyesha matokeo yake.Baadaye hujiundia nadharia na kutoa kanuni ambazo zinapimika.
Isimu imegawanyika katika matawi mbalimbali, miongoni mwa matawi hayo ni pamoja na  matawi mawili ambayo ni isimu elekezi na isimu elezi kama yafuatavyo.

Uelekezi (isimu elekezi).
        Huu ni mtazamo unaojaribu kuweka kanuni za usahihi wa namna watu wanavyotakiwa kutumia lugha. Isimu hii ilianzishwa katika kipindi cha mapokeo ambapo wanaisimu waliwekeza kwenye sheria na kanuni za kuzingatia watumiaji wa lugha wanavyotakiwa kutumialugha hiyo wakati wa kuandika na kuzungumza. Sheria na kanuni hizo ni pamoja na muktadha, mada, wahusika, jinsia, na umri.

Isimu elezi.
       Uelezi au ukipenda (isimu elezi) ni mtazamo ambao huelezea ukweli wa lugha jinsi ilivyo na inavyotumika na jamii lugha husika na wala sio namna inavyotakiwa kutumika. Isimu elezi haiweki kanuni ngumu au sheria ngumu zozote zinazotokana na mawazo ya mtu juu ya lugha fulani bali huelezea lugha kwa kuangalia namna lugha hiyo inavyojidhihirisha yenyewe. Huelezea sheria na kanuni ambazo mwanajmaii wa lugha ameziweka kichwani na zinazoakisi uwezo wake wa lugha. Kwa kifupi, haielezi wala kuagiza namna mtu anavyotakiwa kutumia lugha bali namna lugha ilivyo na inavyotumika na wamilisi wa lugha hiyo.
          Pamoja na yote kuwa ni matawi ya isimu lakini matawi haya yametofautiana kwa namna moja ama nyingine. Tofauti iliyopo baina ya isimu elekezi na isimu elezi.

         Isimu elekezi hii hujaribu kuweka sheria na kanuni za matumizi sahihi ya lugha ili watumiaji wa lugha walazimike kuzitumia sheria hizo, wakati wa sarufi mapokeo wagreek  na wanawima wengine walielezea safuri ya lugha kwa kuegemea matumizi sahihi jinsi ya kuizungumza na kuiandika, wanaoshikilia mtazamo wa wanaotumia kigezo cha maana katika kutathimini usahihi wa kusema. Kwa mujibu wa wanasarufi elekezi neno huelezea kwa kuzingatia kigezo chenye maana, hivi kwamba ni kipashio chenye maana moja. Wanazingatia neno na maana yake bila kuhusisha muktadha aidha hawakutoa maelezoya kutosha kuhusu uchanganuzi wao wa lugha walizingatia andishi na hivyo maelezo yao yaliegemea katika sarufi maandishi.  Lakini mkabala huu wa isimu una udhaifu wake kama ifuaatavyo.
- waliegemea katika lugha ya maandishi na kusahau lugha ya mazungumzo,
-hawashughulikii miundo mbalimbali ya sentensi,
-wanasisitiza maneno bila kujali amilifu gani katika sentensi,
-huzingatia maana bila muktadha siyo sahihi mfano mbuzi.
          Lakini, Isimu elezi ni mtazamo wa isimu unaozingatia umuhimu wa kuchambua vipemgele vya lugha kama vilivyo, hii hujikita katika kutoa maelezo ya muundo wa lugha na kila lugha ina miundo yake inayojitokeza kupitia ruwaza zinazo bainika bayana. Lengo la wanaisimu elezi ni kuchunguza uhusiano wa vipashio katika sentensi na kutumia mwelekeo wa uchunguzi wao kuigawa sentensi katika makundi mbalimbali lama kirai nomino na kirai kitenzI (KN+ KT). Wanaisimu elezi walitumia vigezo vifuatavyo katika kubainisha vipashio katika sentensi,
(a)    Kutambulisha uhusiano sambamba, ni kubainisha uhusiano wa maneno katika uhusiano sambamba (ulalo) mfano. Mtoto huyu amechapwa (sentensi hii ipo sahihi imeanza na
                                            kikundi nomino)
                                           Kimevunjika kiti hiki (sentensi hii haipo sahihi kwasababu
                                            haijaaza na kikundi nomino)       
(b)   Kutambulisha uhusiano wima, kutambulisha uhusiano wa maneno na kuweka mazingira sawa ya kiwima. Mfano.  Mtoto huyu amelala
                                          Kiti hiki kimevunjika
Isimu elezi ni msingi mwafaka katika uchanganuzi wa lugha kubainisha viamba jengo katika sentensi. Mkabala huu unabainisha viamba jengo kwa kuzingatia maumbo ya maneno na jinsi ya navyo husiana ndani ya sentensi, sentensi kwa kawaida huundwa na mfatano viamba jengo au makundi ya maneno makundi hayo ndo huitwa viamba jengo. Lakini pia mkabala huu wa isimu una udhaifu wake kama ifuatavyo,
Udhaifu wa  isimu elezi ni kwamba ni vigumu kutumia mkabala huu kuchambua sentensi yenye utata kwasababu yenyewe imejikita katika kuangalia muundo wa sentensi na sio maana ya sentensi, kwa  mfano sentensi, ulifikaje hapa?
Kwa kuhitimisha, tofauti kuu iliyopo baina ya isimu elekezi na isimu elezi ni kwamba isimu elekezi imejikita katika sheria na kanuni za lugha lakini isimu elezi yenyewe imejikita katika kutazama muundo wa sentensi, pamoja na hayo lakini yote ni matawi ya isimu yanayoshughulika na sayansi ya uchunguzi wa lugha kama tulivyoelzwa na wataalamu mbalimbali walivyoelezea maana ya isimu.





 MAREJELEO
AAA TUKI (1990)Kamusi sanifu ya isimu na lugha. Dar es salaam:
Mgullu,R.S (1999).Mtaala wa isimu, fonetiki, fonolojia na mofolojia ya kiswahili, Nairobi Kenya, longhorn publishers.
King’ei, K. (2010).Misingi ya Isimu Jamii. Taasisi ya Taaluma za Kiswahili: Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.

Comments

Popular posts from this blog

International Law

KATIBA YA KIKUNDI