Fasihi Simulizi


Fasihi Simulizi ,ni fasihi inayotungwa au kubuniwa kichwani na kuwasilishwa kwahadhira kwa njia ya mdomo na vitendo bila kutumia maandishi mulokozi( 1996).
Hivyo fasihi simulizii na fungamana namuktadha au mazingira Fulani ya kijamii na kutawaliwa na mwingiliano wa mambo kama vile fanani, hadhira, fani, tukio, mahali  pamoja na wakati wa utendaji.
Ni aina ya fasihi  ambayo hutumia mdomo katika kuumbwa, kuwasilishwa na kusambazwa kwa wasikilizaji na watumiaji wake (Balisidya, 1983).
Fasilihi hii zinasisitiza kwamba fasihi simulizi inategemea uwepo wafanani, hadhira, jukwaa na mada. Hivyo kwa ujumla, tunaweza tunaweza kusema kuwa fasihi simulizi ni sanaa inayotumia lugha kisanaa ili kufikisha ujumbe kwa hadhira iliyokusudiwa kwa njia yam domo.
Msanii katika fasih isimulizi ni mtu anayesimulia hadithi, methali, vitendawili au kucheza ngoma mbele za hadhira .
Msanii ,mahiri, ni fundi stadi mwenye akili timamu ,mwenye uwezo wa kueleza na kupanga fikra katika njia ya hisia au zana. Anao uwezo wa kubuni sanaa za mitindo ya aina mbalimbali kama vile kuchora, kuchonga kufinyanga kusuka na kufuma. Baraza la sanaa la taifa( 1982).
Hadhira ni wapokeaji ,watazamaji,au wasikilizaji wakazi yafasihi . Katika fasihi simulizi hadhira wanahusiana kwa karibu sana na msanii wakazi ya fasihi ssskiutendaji. Kwani utendaji wa fasihi simulizi hukutanisha pamoja hadhira na fanani pamoja na kufanikisha kazi hiyo.
Kuna uhusiano wakaribu sana baina  ya fanani na hadhira katika fasihi simulizi kama sifuatavyo:
Ushiriki
Hadhira anahusiana na fanani kama ushiriki wa kazi yake kwani fanani anamtegemea hadhira katika utendaji wakazi yake . fanani ili kufikisha ujumbe aliokusudia katika jamii lengwa anamtegemea uhusika wahadhira katika vipengele mbalimbali mfano  , kupiga makofi, fanani anaetamba hadithi anaanza kwakushikisha hadhira yake mfano:
Fanani :hadithi hadithi
Hadhira :hadithi njoo utamkolea.
Fanani: hapo zamani za kale………………
Hadhira: mmhhh
Kutokana na uhusiano huo huipa fasihi simulizi sifa ya uhai kwani fanani na hadhira wanakuwa pamoja kiutendaji tofauti na fasihi andishi ambapo hadhira yake haiusiki kabisa katika kazi husika. Lakini katika tanzu mbalimbali ya fasihi simulizi hadhira wanahusika katika ushiriki wao mfano katika kupiga    makofi kusikitika kucheka kuimba nyimbo au  kujibu maswali hadhira ikikoseka na fanani ni ngumu kufanya kazi yake hivyoo ni kweli kuwa kuna uhusiano kati ya hadhira na fanani.
Utazamaji
Katika kufanikisha kwa kazi ya fasihi simulizi kiutambaji jukwaani inatagemea pia kuwepo kwa hadhira ambao ndio watazamaji wa kazi hio hadhira ikikosekana ni vigumu kufanikisha kwa kazi hio mfano sanaa  za maonyesho, ngoma,  maigizo, utani, hutegamea kuwepo kwa watazamaji wa matukio hayo kukosekana kwa watazamaji huondoa sifa ya fasihi simulizi hali hii ndio hupelekea kukutanisha ana kwa ana baina ya fanan na hadhira hivyo msanii ana uhusiano mkubwa na hadhira yake Kwani hutegemea hadhira kutazama kile kinafanyika  jukwaani tofauti na  fasihi andish itanzu kama riwaya ushairi hautegeme I uwepo wa hadhira  ana  kwa ana kutazama kazi hio.
Suala la fanani kuitambua hadhira yake.
Msanii wa fasihi simulizi ni zao la jamii husika hivyo ana uhusiano na hadhira kwa kuwa yeye ni zao la jamii hio hivyoo ingekuwa ngumu msanii kutamba hadithi ambae ninje ya jamii yake na kutoa mifano kulinga na na mandhari hayo  kulingana na tajiriba ya jamii husika hivyo kutokana na msanii ni mjuzi wa tamaduni husika ndio humwezesha msanii  kuitawala hadhira yake vizuri suala hili hudokeza uhusiano kati ya msani inahadhira katika fasihisi mulizi tofautina fasihi andishi msani in ivigumu kuelewa tamaduni nahadhira kwa sababu hadhira yake ni pana zaidi.
matumiziyaishara
Nalo linathibitisha uhusiano uliopo baina ya msanii na hadhira kiutendaji kwani kutokana na kuwa na uhusiano wa karibu humsaidia msani ipiakutumia lugha ya ishara mfano kutikisa kichwa, kukonye za macho na kutikisa mabega ambaye humsaidia katika uwailishaji wake kwa hadhira hali hii ni kwa sababu ya uhusiano baina ya msanii na hadhira kiutendaji katika fasihi andishi kutokana na kukoseka na uhusiano huo msani ihawezi kutumia ishara kumsaidia katika hadhira yake.
Uteuzi wa matumizi ya lugha
Uhusiano wa msanii na hadhira  ndio utakae muongoza katika uteuzi wa lugha  ili kuitawala jamii  yake kulingana na hadhi ya watu aliokuwa nao mfano wazee atatumia lugha ya hekima na busara pia kwa vijana atatumia lugha ya kihuni  kulingana nao ili asiweze kuwa kwaza na kuwaondolea hadhira hio umakini wakumfuatiliua kwani atakuwa anawakera hivyoo kutokana na kuwepo kwa uhusiano huoina msaidia fanani kufanya kazi itakaopendwa na kila mtukuto kanana uhusino huo.
Suala la toni
Toni ni hali ambaea na  kuwa  nae msani ipindianawa silishakazi yake mfano huzuni furaha hasira hali hio inakuwa na uhusiano wa moja kwa moja mfano msani ianaposimulia hadithi za kuhuzunishawa kati huo hadhira itawapelekea kuhuzuni kapia hata kutokwana machozi lakini msanii atakapotamba kazi za kufurahisha mfano hadithi za abunuasi,atasababisha hadhira yake kufurahi sana na kucheka hivyo toni ya msanii ndio inahusianawa moja kwa moja na toni ya hadhira sa yake hivyo basi msani inahadhira wana uhusiano katika kazi ya fasihi.

Uwezo wa msani ikuitawala hadhira yake.
Msanii anaweza kuwa ni chanzo cha kufanya hadhira yake kuwa makini kufuatilia kazi yake kama atakuwa na uwezo mkubwa wakuitawala mfano msanii anapoonyesha umahiri wake, kujiamini ,kutumia lugha ya ucheshi kiutendaji ataweza kuifanya hadhira yake kufurai na kuwa makini wakati wote na    kuwa na hamu  ya kuendelea kumfuatilia msanii lakini kama msanii atashindwa kuitawala hadhira yake atasabaisha hadhira kuchoka  kwa haraka kisha kupoteza umakini wao wa kufuatilia  tukio linalotendeka jukwani hivyo .msanii anapoona hadhira yake inaanza  kuchoka kufuatilia kazi anakuwa huru kutumia mbinu mbalimbali ya kurudisha hadhira yake katika hali ya mwanzo swala ambalo ningumu kufanyika katika fasihi andishi.
HITIMISHO
Hivyo katika utendaji wa fasihi simulizi inahusisha kuwepo kwa fanani, hadhira ,tukio lenyewe na muktadha wakufanyika tukio hilo . Kutokana na kukutana ana kwa ana kati  ya  msanii na hadhira unajenga uhusiano mkubwa kati ya hadhira na msanii na ndio huipa fasihi simulizi sifa ya uhai kwani fanani na hadhira wanahusiana katika kukamilisha kazi hiyo.



MAREJEO
Baraza la sanaa la taifa  (1982) falsafayasanaatanzania . Dar- es-salama
Mhando,J. naBalisidya, N. (1976) Fasihi , Tanzania Publishing House, Dar es salaam.
Mulokozi, M.M. (1989:5) “TanzuzaFasihiSimulizi” Katika MULIKA Na. 21, D.SM.
Muhando, P &Balisidya, N (1976) FasihinaSanaazaMaonyesho. Tanzania Publishing    
House(TPH) Dar es Salaam.

Comments

Popular posts from this blog

International Law

KATIBA YA KIKUNDI