MKATABA WA KUPANGA NYUMBA


MKATABA WA KUPANGA NYUMBA/ CHUMBA KATIKA NYUMBA YA BI ZAINABU MUSSA M’BISI ILIYOKO ENEO LA KISUTU MTWARA MJINI.

Makubaliano yaliyobainishwa hapo chini yamefanyika hapa Mtwara siku ya tarehe……….mwezi wa…………….mwaka…………………

Baina ya
Bi Zainabu M. M’bisi ambaye katika mkataba huu anajulikana kama mmiliki halali wa nyumba iliyoko katika mtaa wa kisutu kiwanja namba…………………Mtwara.
Na
Bw/Bi………………………………………………….atakayejulikana katika mkataba huu kama mpangaji kwa mwenye nyumba kwa kuwa nia ya mwenye nyumba ni kupangisha watu/mtu katika nyumba yake, kwa mpangaji aliyetajwa hapo juu ambaye ameomba apate nafasi ya chumba/ nyumba hii. Kwa kuwa mpangaji ameomba apange chumba/ nyumba kwa matumizi ya kuishi/ kulala humo na mwenye nyumba amekubali kumpangisha mpangaji kama alivyoomba.
Hivyo basi kwa mkataba huu pande zote mbili zimekubaliana kama ifuatavyo;-
1.     Kwa malipo ya pango yaliyoainishwa hapa chini mwenye nyumba anampangisha mpangaji chumba/ nyumba.
2.     Kipindi cha upangaji kwa mujibu wa mkataba huu ni muda wa miezi sita (6), kuanzia tarehe……….. mwezi wa………………..hadi tarehe…………. Mwezi wa…………….. na iwapo mpangaji anataka kuongeza kipindi kingine cha upangaji anatakiwa kumtaarifu mwenye nyumba miezi miwili kabla ya kipindi cha mwanzo kumalizika na kulipa upya. Asipofanya hivyo mwenye nyumba/mmiliki wa nyumba ana uhuru wa kumpokea mpangaji mwingine na kumpangisha ili aingie chumba hicho kwa kuzingatia makubaliano ya mkataba uliopo kati ya mwenye nyumba/mmiliki wa nyumba na mpangaji unasemaje.
3.     Upande wowote unaweza kukatisha mkataba huu kwa kutoa ILANI (Notice), isiyopungua miezi tatu (3) kwa upande mwingine.
4.     Imekubaliwa na pande zote mbili kwamba kodi ya kila mpangaji itakuwa kiasi cha shilingi Elfu ishirini na tano tu.Tsh.(25000/=) kwa mwezi ambazo zinapaswa kulipwa kwa mara moja kwa hesabu ya miezi sita (6) kabla ya kupewa/ kukabidhiwa chumba.

malipo ya gharama za umeme na maji ni juu ya mpangaji/wapangaji kulipia katika ofisi husika kwa kuchangiana wao wenyewe kadiri ya matumizi yao katika nishati hizo (Bill) watayoletewa kutoka ofisi husika.
5.     Mpangaji/wapangaji hawaruhusiwi kuchora/ kutoboatoboa kuta za nyumba na kubandika karakatasi kwa gundi wala kubandika ukutani picha za magazeti.
6.     Mpangaji/wapangaji hawaruhusiwi kufanya marekebisho katika miundombinu ya umeme na maji.
7.     Mpangaji anapohama chumba/ nyumba kwa sababu yoyote ile anapaswa kuiacha nyumba/ chumba katika hali ya usafi, haruhusiwi kubomoa au kung’oa kitu au sehemu ya jengo husika au kufanya uharibifu wa aina yoyote ile.
8.     Mpangaji sharti/aweke saini ya makubaliano kuthibitisha kuwa anaipokea nyumba/ chumba ikiwa safi na salama na chumba atakabidhiwa tu endapo mpangaji ameshakamilisha malipo ya miezi sita (6) na kusaini mkataba huu. Nae pia anapomaliza muda wake wa kuishi katika chumba / nyumba ataikabidhi nyumba/ chumba kwa mwenye nyumba katika hali ya usafi mwisho wa mkataba huu au wakati wowote akitaka kuhama kabla ya kufikia mwisho wa mkataba.
9.     Mpangaji haruhusiwi kupangisha chumba/ nyumba kwa mtu mwingine au kuingia ubia na mtu mwingine au kumkabidhi mtu mwingine chumba/ nyumba kabla au baada ya kwisha mkataba bila au pasipo idhini na kibali cha mwenye nyumba.
10.            Mpangaji haruhusiwi kuunganisha umeme kwa njia zake nje ya soketi na holda zilizowekwa katika jengo kulingana na ramani ya jingo. Haruhusiwi kutumia jiko la umeme.
11.            Endapo litatokea tatizo lolote lile katika chumba/ nyumba mpangaji anatakiwa kutoa taarifa mara moja kwa mwenye nyumba. Kwa mfano kuvuja kipindi cha masika.
12.            Mpangaji atagharamia mwenyewe matengenezo ya vifaa vifuatavyo;- vitasa, kuungua balbu, kuharibika kwa bomba la maji, kupoteza au kuvunja ufunguo, kuvunja madirisha,  kuchimba shimo la taka. Matengenezo makubwa na matatizo ambayo yanahitaji matengenezo kutokana na kimbunga, mvua kali au hali ya hewa ya pekee sana yatafanywa na kulipwa na mwenye nyumba.
13.            Mpangaji/wapangaji watafanya/ atafanya usafi kwenye chumba chake/ nyumba yake usafi wa juu na chini ya sakafu. Usafi wa choo, bafu na kiwanja watapeana zamu. Taka kavu zichomwe moto shimoni na zisizochomeka zitupwe shimoni.
14.            Mpanngaji akivunja sharti lolote la mkataba huu mwenye nyumba atakuwa na haki ya kukatisha mkataba huu mara moja.
15.            Ulevi na kuvuruga wengine hakutakiwi kabisa kwa mkaaji wa nyumba hii muziki wa redio, TV, simu ziwe na milio ya chini/ sauti ndogo hasa muda wa usiku ili kuzuia kusumbua jirani zako unaoishi nao ambao labda wamechoka na wanahitaji kupumzika kwa utulivu na ukimya.
16.            Kwa kuthibitisha yote yaliyotangulia pande zote mbili zimeweka sahihi zao leo tarehe………. Mwezi………… mwaka…………… mbele ya mwenyekiti wa mtaa wa kisutu na mashahidi wengine kama inavyoneka hapo chini.

Jina la Mmiliki wa nyumba…………………………….....Sahihi………………
Jina la Mpangaji………………………………………..Sahihi…………………
Jina la msimamizi kwa niaba ya mwenye nyumba……………………………Sahihi………….
Jina la shahidi wa mwenye nyumba…………………………………….Sahihi…………………
Jina la shahidi wa mpangaji………………………………………….Sahihi………………………
Jina la M/kiti wa mtaa wa Kisutu..………………………………..…..Sahihi…………………..

                   Muhuri………………………………..





MALIPO YA PANGO LA CHUMBA/ NYUMBA/ CHUMBA NA UKUMBI

Mimi………………………………………………..kwa niaba ya Bi Zainabu M M’bisi nimepokea malipo ya pango la chumba na kiasi cha ……………………………………………………….. Tsh.(………………) kutoka kwa Bw./Bi…………………………………… malipo ya miezi sita (6) toka tarehe ……………….. mpaka tarehe………………………… nyumba iliyoko katika Mtaa wa Kisutu Kiwanja Namba 448.
Sahihi kwa niaba ya mwenye nyumba.
Jina la Mpokeaji……………………………………..Sahihi……………………
Jina la shahidi wa mpokeaji…………………………………….Sahihi…………………..
Jina la Mpangaji/ Mlipaji…………………………………………Sahihi………………….
Jina la shahdi wa mpangaji/ Mlipaji…………………………………..Sahihi………………
Tarehe…………………………….
Makabidhiano yote yamefanyika na kusimamiwa na M/kiti wa Mtaa  wa kisutu.
Jina na sahihi ya M/kiti wa Mtaa………………………………..... Sahihi……………….
                  
Muhuri…………………………………

Comments

Popular posts from this blog

Information technology

Unominishaji,