mofolojia ni utanzu wa isimu ambao huchunguza , hupambanua na kuchanganua maumbo maneno na aina zak


UTANGULIZI
Kuna baadhi ya wataalamu mbalimbali wamefafanua au  wamefasili dhana ya mofolojia kama ifuatavyo
Matinde (2012) anasema kuwa mofolojia ni utanzu wa isimu ambao huchunguza , hupambanua na kuchanganua maumbo maneno na aina zake.
Rubanza (1996:1) anasema Mofolojia ni taaluma inayojishughulisha na vipashio vya lugha na mpangilio wake katika uundaji wa maneno .  Anaongeza kwamba mofolojia huzingatia namna vipashio vinavyotumika katika kupangilia  mfumo wa muundo wa maneno katika lugha.
Habwe na Karanja (2004) wanasema kuwa"Mofolojia " Ni tafsiri ya neon la kiingereza "Morphology" ambalo limetokana na na neno la kiyunani "Morphe " lenye maana ya muundo au umbo, hivyo basi mofolojia ni neno linalotumika kumaanisha kiwango cha isimu kinachoshughulikia muundo wa ndani wa  maneno.
Kwa ujumla , Mofolojia ni taaluma au kiwango cha isimu au sarufi ya lugha ambacho huchanganua maumbo  ya maneno katika lugha husika. Hivyo mofolojia huchunguza muundo wa ndani na ule wa nje wa maneno katika lugha fulani
MAWANDA YA MOFOLOJIA
Mofolojia ina mawanda mawili ambayo ni
Mawanda ya mofolojia minyambuliko ya maneno, tawi hili hushughulikia minyumbuliko mbalimbali ambayo huwekwa kwenye mizizi ya maneno bila kubadili aina au kategoria ya neno, kwa maana kwamba kama litakuwa ni kitenzi , hata baada ya mnayumbuliko neno hilo litabaki kuwa kitenzi.
Mfano, -imb-  imbia, imbisha, imbiana
                -pig-  pigia, pigisha, pigana, pigwa
Katika mifano hiyo maneno yote yametokana na na mizizi {-imb-} na {-pig-} ni vitenzi , licha ya kuwa na maumbo tofautitofautiyenye  dhima na maana tofauti.
Mawanda ya mofolojia ya uundaji wa maneno, hili ni tawi la isimu maumbo ambalo hushughulikia michakato mbalimbali ya uundaji wa maneno katika lugha husika. Kila lugha huwa na utaratibu maalumu wa maneno. Tawi hili hushughulikia minyambuliko mbalimbali ambayo huwekwa kwenye mizizi ya maneno na ama kubadili au kutobadili aina au kategoria ya neno.
Mfano, Kitenz                              Nomino
                Imba                               wimbo
                 Lima                                kilimo
                    Piga                                  pigo
Ufuatao ni msigano wa mawanda ya mofolojia kama ifutavyo:
Mofolojia minyambuliko ya maneno haibadili aina au kategoria ya neno, kwani hushughulikia minyambuliko mbalimbali ambayo huwekwa kwenye mizizi ya maneno bila ya kubadili neno hilo, yaani kwamba maneno hubakia katika kategoria ileile ya mwanzo hata baada ya kufanyiwa minyambuliko
 Mfano, {chez-} chezea, chezesha, chezeana
                {som-} soma, somesha, someana
Lakini mofolojia ya uundaji  wa maneno hubadili aina au kategoria ya neno au maneno
Mfano,Kivumishi                        Kitenzi
                Safi                                safisha
                 Dogo                             dogosha
                 Tulivu                             tuliza
                  Erevu                             Erevusha
Mawanda ya mofofolojia minyambuliko ya maneno, viambishi huongezwa baada ya mzizi wa neno
Mfano, {lia-}, lilia, liliana
               {lim-}, limia, limisha, limiana
Lakini mofolojia ya uundaji wamaneno, viambishi hupachikwa mwanzo au mwisho mwa mzizi wa neno
Mfano, {-chez-}, A-na-chez-a
Hivyo kiambishi  A- huonesha nafsi , -na- njeo, -chez- mzizi , -a maana
Mofolojia minyambuliko ya maneno huzalisha maumbo mbalimbali ya maneno yaliyo katika kategoria moja au ileile
Mfano, Kimb-  kimbiana, kimbizwa, kimbilia
               Pit- pitiana, pitiwa, pitiana
Hivyo basi  maumbo ya awali ni vitenzi lakini pia maumbo yote yaliyozalishwa baada ya mnyambuliko ni vitenzi. Lakini katika mofolojia ya uundaji wa maneno huzalisha maumbo mbalimbali yaliyopo kwenye kategoria tofautitofauti
Mfano, Kitenzi            Nomino
               Lia                  kilio au mlio
               Cheza             mchezo au mchezaji
               Hakiki              mhakiki
               Utumwa          mtumwa
Hivyo huo ni msigano mojawapo wa mawanda haya mofolojia.
Mofolojia mnyumbuliko wa maneno huwakilisha dhana mbalimbali kama vile njeo, nafsi, udogoshi, ukubushi, hali, ukanushi, urejeshi, upatanisho wa kisarufi na idadi.
Mfano, njeo neno Anakimbia linaonesha wakati uliopo.
Lakini mofolojia ya uundaji wa maneno haiwezi kuwakilishwa dhana hizo, bali hubeba kategoria tu.
Mfano, Kitenzi kuwa nomino
                                           Pika                  Mpishi
                                           Ubepari             Bepari
                                          Linda                   Lindo
Mofolojia ya  uundaji wa maneno huhusisha kanuni  mbalimbali  kama uyeyushaji, udondoshaji,
Mfano, uyeyushaji  Nomino   Nomino
                                  Muaka     mwaka
                                  Muembe     mwembe
             Udondoshaji  Nomino    Nomino
                                      Mutu          mtu
                                      Mufalme       mfalme
Wakati mofolojia ya minyumbuliko ya maneno haihusishi kanuni hizo, isiopokuwa ni utaratibu wa kisarufi.
Hitimisho
Kwa ujumla mawanda ya mofolojia yanamchango mkubwa katika lugha, kwani huongeza msamiati katika lugha husika kwa kupitia kanuni mbalimbali hususani katika mofolojia  ya uundaji wa maneno ambapo neno moja hubadilika kuntoka kategoria moja hadi nyingine, kwani pia hata kwenye minyambuliko husaidia kuongeza msamiati katika luha.


MAREJEO.
Rubanza, Y.T. (1996) Mofolojia ya Kiswahili. Dar es salaam: Chuo Kikuu Huria Cha Tanzania.
Habwe, J. & Karanja, P. (2004) Misingi ya Sarufi ya Kiswahili. Nairobi: Phoenex Press.
Matinde, S. (2012) Dafina Lugha, Isimu na Nadharia: Kwa Sekondari, Vyuo Vya Kati n Vyuo Vikuu. Mwanza, Tanzania: Serengeti Publisher Ltd.

Comments

Popular posts from this blog

International Law

KATIBA YA KIKUNDI