SWALI Fafanua kwa kina msigano wa mawanda ya mofolojia
SWALI Fafanua kwa kina msigano wa mawanda ya mofolojia
Kuna
wataalamu mbalimbali wamejaribu kutoa fasili mbalimbali kuhusu dhana
unominishaji na mnyumbuliko kama ifuatavyo;
Unominishaji Ni ule utaratibu wa kuunda nomino
kutokana na maneno mengine ambayo si nomino. Lugha ya kiswahili huunda nomino
nyingi kutokan na vitenzi, vivumishi na nomino yenyewe. (Mgulu 1999: 141).
Habwe na
Karanja (2004) wanasema kuwa Unominishaji ni hali ya kuunda nomino kutoka
katika kategoria nyingine ya neno.
Kwa ujumla unominishaji ni kitendo cha kibadili
kategoria mbalimbali za maneno kua nomino. Mfano wa kategoria hizo ni kitenzi
kivumishi na nomino yenyewe.
Unyambulishaji ni utaratibu katika lugha wa kupachika
au kuongeza viambishi kwenye mzizi wa neno ili kuunda maneno mapya ( Massebo
2012 : 127).
Unyambulishaji ni mbinu ya uundaji wa hivi kwamba
viambishi mbalimbali huambikwa kwenye mzizi husika na kuunda neno jipya (
Matinde 2012:119).
Kwa ujumla, unyambulishaji ni kitendo cha kupachika au
kuweka viambishi kwenye mzizi wa neno ili kuunda maneno mapya.
Ifutayo ni
michakato ya unomiishaji ya minyumuliko geuzi ya kateria ya lugha ya kiswahili
Nomino
Kutoka Kwa Vitenzi
Nomino za Kiswahili zinaweza kuundwa kutoka kwa
vitenzi. Katika hali hii, viambishi awali na viambishi tamati vya umominishaji
huambikwa kwenye mizizi au mashina ya vitenzi. Baadhi ya viambishi awali vya
unominishaji ni kama vile: {mu}, {m}, {ki}, {u} na {Ø} na vya wingi ni {wa},
{vi}, {ma}, {u} na {Ø}. Kwa upande mwingine viambishi tamati vya unominishaji
ni kama vile: {ji}, {zi}, {fu}, {o} na {i}. Ifuatayo ni michato mbalimbali ya
unominishaji inayohusu mashina na mizizi ya vitenzi: Kutumia viambishi awali
vya unominishaji {m} au {mu} katika umoja na {wa} katika wingi pamoja na shina
la kitenzi na kiambishi tamati cha unominishaji {ji}.
{m} +
{shina-T} + {ji}
{wa}
Kwa
mfano
Kimbia{mu}+{imb}+{a}+{ji}
> mwimbaji
Winda
{mu}+{wind}+{a}+{ji} > mwindaji
Ua
{mu}+{u}+{a}+{ji} > mwuaji
Cheza
{mu}+{chez}+{a}+{ji} > mchezaji
Tangaza
{mu}+{tangaz}+{a}+{ji} > mtangazaji
Chora
{mu}+{chor}+{a}+{ji} > mchoraji
Kutumia
kiambishi awali cha unominishaji {m} na {mu} pamoja na mzizi wa
{wa}
{ifu}
Kwa
mfano
Simamia
{m}+{simami}+{zi} > msimamizi
Kimbia{m}+{kimbi}+{zi}
> mkimbizi
Kagua
{m}+{kagu}+{zi} > mkaguzi
Lea
{m}+{le}+{zi} > mlezi
Danganya
{m}+{dangany}+{i}+{fu} > mdanganyifu
Komboa
{m}+{kombo}+{zi} > mkombozi
{ki}
+ {mzizi-T} + {O}
{wa}
{vi}
Kwa
mfano
Cheza
{m}+{chez}+{o} > Mchezo
Kopa
{m}+{kop}+{o} > Mkopo
Chora
{m}+{chor}+{o} > Mchoro
Lia
{m}+{li}+{o} > Mlio
Panga
{m}+{pang}+{o} > Mpango
Koma
{ki}+{kom}+{o} > Kikomo
Kwaza
{ki}+{kwaz}+{o} > Kikwazo
Lima
{ki}+{lim}+{o} > Kilimo
Vuka
{ki}+{vuk}+{o} > Kivuko
Lia
{ki}+{li}+{o} > Kilio
Kutumia
kiambishi awali cha unominishaji {mu} au {mi} pamoja na mzizi wa kitenzi na
kiambishi tamati {o} cha unominishaji
{mi}
Kwa
mfano
Enda
{mu}+{end}+{o} > mwendo
Alika
{mu}+{alik}+{o} > mwaliko
Ita
{mu}+{it}+{o} > mwito
Isha
{mu}+{ish}+{o} > mwisho
Unda
{mu}+{und}+{o} > muundo
Ungana
{mu}+{ungan}+{o} > muungano
Kutumia
kiambishi awali cha unominishaji {Ø} pamoja na mzizi wa kitenzi na
{Ø} + {mzizi-T} + {O}
{ma}
Kwa
mfano
Pamba
{Ø}+{pamb}+{o} > Pambo
Pinda
{Ø}+{pind}+{o} > Pindo
Soma
{Ø+{som}+{o} > Soma
Tenda
{Ø}+{tend}+{o} > tendo
Tatiza
{Ø}+{tatiz}+{o} > tatizo
Tangaza
{Ø}+{tangaz}+{o} > tangazo
Umba
{Ø}+{umb}+{o} > umbo
Tamka
{Ø}+{tamk}+{o} > tamko
Pambana
{Ø}+{pamban}+{o} > pambano
Kutumia
kiambishi awali {Ø} katika umoja pamoja na mzizi wa kitenzi na kiambishi tamati
cha unominishaji {a}
{ma}
Kwa
mfano
Shitaki
{Ø}+{shitak}+{a} > shitaka
Sifu
{Ø}+{sif}+{a} > sifa
Subiri
{Ø}+{subir}+{a} > subira
Kutumia
kiambishi awali {u} cha unominishaji pamoja na mzizi wa kitenzi na kiambishi
tamati cha unominishaji {zi}
Kwa
mfano
Bagua
{u}+{bagu}+{zi} > ubaguzi
Chagua
{u}+{chagu}+{zi} > uchaguzi
Chochea
{u}+{choche}+{zi} > uchochezi
Chukua
{u}+{chuku}+{zi} > uchuku
Fafanua
{u}+{fafanu}+{zi}
Komboa
{u}+{kombo}+{zi}
Fumbua
{u}+{fumbu}+{zi}
Pekua
{u}+{peku}+{zi}
Kutumia
kiambishi awali {u} cha unominishaji pamoja na mzizi wa kitenzi na viambishi
tamati vya unominishaji {o} na {i}
{wa}
Kwa
mfano
Bisha
{u}+{bish}+{i} > ubishi
Shinda
{u}+{shind}+{i} > ushindi
Penda
{u}+{pend}+{o} > upendo
Batiza
{u}+{batiz}+{o} > ubatizo
Ita
{u}+{it}+{o} > wito
Imba
{u}+{imb}+{o} > wimbo
Nomino Kutoka kwa Vivumishi
Tunaweza
kuunda nomino kutoka kwa vivumishi kwa kutumia kiambishi awali {u} cha
unominishaji pamoja na shina la kivumishi.
{u}
+ {shina-V}
Kwa
mfano
{baya}
{u}+{baya} > ubaya
{bovu}
{u}+{bovu} > ubovu
{fupi}
{u}+{fupi} > ufupi
{kubwa}
{u}+{kubwa} > ukubwa
{dhaifu}
{u}+{dhaifu} > udhaifu
{katili}
{u}+{katili} > ukatili
{bora}
{u}+{bora} > ubora
Nomino kutoka kwa Nomino Zingine
Tunaweza
kuunda nomino kutoka kwa nomino zingine kwa kutumia kiambishi awali {u} cha
unominishaji pamoja na mzizi wa nomino.
{u}
+ {mzizi-N}
Kwa
mfano
Rafiki
{u}+{rafiki} > urafiki
Balozi
{u}+{balozi} > ubalozi
Bingwa
{u}+{bingwa} > ubingwa
Chachu
{u}+{chachu} > uchachu
Bepari
{u}+{bepari} > ubepari
Fundi
{u}+{fundi} > ufundi
Seremala
{u}+{seremala}
HITIMISHO
Kwa
ujumla michakato ya unomiishaji ya mnyumbuliko geuzi ya kategoria ya lugha ya
Kiswahili inatusaidia katika kunadili kategoria mbalimbali za maneno na kuwa
nomino. Hivyo maneno mbalimbali ya lugha ya Kiswahili kama vile vitenzi
vivumishi na nomino yenyewe tunaweza kubadili kategoria hizo na kuwa nomino.
MAREJELEO
Habwe
na Karanja ( 2004). Misingi ya Sarufi ya
Kiswahili; Nairobi Kenya: Phoenix Publishers.
Massebo,
J.A (2012). Nadharia ya Lugha Kiswahili.
Dar es Salaam.Nyambari Nyangwine Publishers.
Mgullu,
R.S (2012). Mtaala wa Isimu: Fonetiki, Fonolojia na Mofolojia ya Kiswahili;
Longman publishers.
Matinde,
S ( 2012). Dafina ya Lugha, Isimu na
Nadharia kwa Shule za Sekondari, Vyuo vya kati
na Vyuo Vikuu.
Comments
Post a Comment