Dhana ya kategoria ya kileksika


Dhana ya kategoria ya kileksika; imejadiliwa kwa namna tofauti tofauti:-
 Khamisi na Kiongo (2002); wamegawa kategoria katika mitazamo miwili ambayo ni:-  mtazamo wanamapokeo na wanausasa, ambapo wanamapokeo walitumia dhana ya kategoria ya kileksika kumaanisha sifa bainifu ya vitu na wanausasa wanaona kategoria kuwa ni zile aina za maneno kama vile nomino, kivumishi, vielezi, viunganishi, vihusishi na vitenzi.
   Massamba (2009), anatoa maana ya kategoria ya kilekisika kwa kusema kuwa ni jumla ya maumbo, faridi au vipashio vingine ambavyo huchangia sifa fulani au ambavyo viko katika kiwango kimoja. Maana hii ni ya jumla kwani imeeleza dhana ya kategoria ya kileksika kwa ujumla bila kujikita katika kategoria za miundo ambayo ndiyo sintaksia.
 Kategoria za kileksika katka lugha ya kiswahili zipo kategoria nane za kileksika ambazo ni nomino, vitenzi, viwakilishi, vielezi, viunganishi, vivumishi, vihusishi na vihisishi.
 Kwamjibu wa Massamba, Kihole, Hokororo (2012 uk.67), wanasema tungo ni nomino ambayo imetokana na kitenzi tunga ambacho kinamaana kushikanisha vitu kwa pamoja kwa kutumia kitu Kama uzi, ungwe ndani yake. Hivyo katika taaluma ya sarufi neno tungo lina maana ya kuweka au kupanga vipashio sahihi ili kujenga vipashio vikubwa katika tungo. Katika lugha ya kiswahili Kuna aina nne za tungo ambazo ni tungo neno, tungo kirai, tungo kishazi na tungo sentensi ambapo tungo hizo huundwa na aina mbalimbali za maneno Kama nomino, kiwakilishi, vivumishi, viunganishi,vitenzi,vielezi,vihisishi na vihusishi.                                                  Kamusi teule ya kiswahili (2001); tungo ni kifungu cha maneno kinachoongozwa na kanuni kisarufi, vipashio vinavyo ungana huunda vipashio vikubwa zaidi.
   Kamusi ya kiswahili (2014), tungo ni kipashio cha kimuundo kipatikanacho kwa kuunganisha vipashio sahihi kuweza kupata kipashio kikubwa zaidi, kwa ujumla tungo ni kipashio cha kimuundo ambacho huwekwa pamoja ili kujenga vipashio vikubwa zaidi katika sarufi.
 Kategoria za kileksika na kategoria za tungo ni kweli zinamipaka inayo pitika kwa sababu tungo hujidhihilisha katika miundo minne ambayo ni tungo neno, tungo kirai, tungo sentensi na tungo kishazi. Viwango hivi ndivyo vinavyodhibitisha kupitika kwa kategoria za kilekisika na kategoria za tungo katika lugha.
 Kwa kuanza na muundo wa tungo neno, ni tungo ambayo ina muundo wa vipashio zaidi ya neno ambayo ni mofimu au fonimu, mfano anacheza, kakimbia. Kategoria ya tungo neno inahusisha aina kuu za maneno yanapo undwa, kinacho zingatiwa katika uainishaji wa tungo neno ni aina za maneno ambayo kwa mantiki hiyo huonedha kupitika huko kwa kategoria za kileksika na kategoria za tungo kwa kutumia aina za maneno ambayo pia hupatikana katika kategoria za kilekisika mfano wa kategoria mojawapo ni nomino, kitenzi, kiunganishi, kihisishi, vihusishi, kiwakilishi, na kivumishi.
     Mfano; - Mama anapika

            - Mjomba anapenda kuimba mziki wa kizazi kipya.
            - Mama anapenda kufanya kazi zake vizuri.
Hivyo aina hizi za maneno ambazo zimetumika katka kuunda sentensi hizo pia zinapatikana katika tungo mfano tungo neno, tungo neno kuna nomino ndaniyake hivyo tunasema inapitika katika kategoria za kileksika na kategoria za tungo.
 Miundo ya tungo kirai, kirai ni neno au fungu la maneno ambalo kwapamoja hutoa taarifa fulani. Kirai sikuzote hakitoi taarifa fulani isiyo kamili ukiachilia mbali vitenzi vya lugha za kibantu. Kategoria ya kirai huundwa kwa aina kuu za maneno, virai hivi huwa na neno kuu na ndilo linalo dhibitisha kirai kipewe jina lipi. Hivyo aina izo za maneno pia ndizo hupatikana katika kategoria za kilekisika. Kwamfano wa tungo kirai Kuna kirai nomino mfano, Rahma mrembo, kirai kitenzi kitenzi mfano anapika vibaya, kirai kivumishi mfano kizuri sana, kirai kielezi mfano kizuri sana, kirai kiunganishi mfano kule,walakini, kihusishi mfano kwa gari na wa baba hivyo kupitia aina hizi za virai pia tunaziona kwenye aina za maneno ambayo ndio ni kategoria za kilekisika kwa sababu hihi inaonesha mipaka inayo pitika.
 Miundo ya kishazi, ni fungu la maneno lenye kiima na kiarifu. Matinde (20012), hata hivyo anadai kuwa kishazi lazima kiwe na kitenzi ndaniyake. Kitenzi kinacho kuwepo katika muundo wa kishazi ndicho kinacho amua kishazi kiitwe kishazi huru au kishazi tegemezi na kukifanya kishazi kitoe taarifa kamili au taarifa isiyo kamili. Mfano kishazi kimegawanyika katika Aina mbili, kishazi huru na kishazi tegemezi hivyo kupitia aina za vishazi vinatumia aina za maneno Kama nomino, vitenzi, vielezi, viwakilishi, vihisishi na vihusishi hivyo sababu hii inadhihilisha kupitika kwa kategoria za kileksika na kategoria za tungo kwa mfano:-
   - Mtoto amekuja
      N      T
   - Mtoto analima
      N     T
   - Mtoto aliekuja jana
      N     BV   E
 Miundo ya sentensi, kategoria ya sentensi inahusu kipashio kikubwa kabisa katika taaluma ya sarufi. Sentensi ni tungo inayo toa taarifa iliyo kamili yenye kiima na kiarifu. Kuna aina kuu tatu za sentensi kimuundo ambazo ni:-
 (i). Sentensi sahili, ni Sentensi inayoundwa na kishazi huru kimoja ambacho hutoa taarifa kamili. Kwamfano;
       -Mtoto mkorofi sana.
 (ii).Sentensi changamano,ni Sentensi inayoundwa na kishazi tegemezi kimoja au zaidi na kishazi huru kimoja. kwamfano:-
       - Mtoto aliyekufa Jana.
 (iii).Sentensi ambatano ni aina ya sentensi ambayo huundwa na sentensi mbili kwa kuunganishwa na lakini, na pia alama za uandishi Kama vile nukta, mkato .nk. kwamfano:-
       - Mama anapika na Baba analima
Aina hizi tatu za sentensi muundo wake huundwa na aina za maneno ambayo hupatikana katita kategoria za kileksika hivyo huonesha mipaka inavyo pitika Kati ya kategoria za kileksika na kategoria za tungo kwa mfano wa sentensi ambazo zimetumia aina za maneno ni;
       - Magambo anakuja leo asubuhi.
           N        T       E
       - Tiffa analima.
          N    T
       - Mama na baba wanalima na kaka na mimi tunacheza mpira kiwanjani.
          N   U  N      T     U  N   U  N      T       N     E
 Kwakuhitimisha kategoria za tungo na kategoria za kileksika zote zinategemeana bila tungo hapawezi kuwa na maneno na bila maneno hatuwezi kuunda tungo hivyo kategoria za kileksika na kategoria za tungo zote zina saidia kuonesha uchunguzi sahihi wa maneno na uteuzi wa tungo sahihi katika lugha yoyote ulimwenguni iwe kiswahili, kireno n.k, aina za maneno ndizo zinaamua tungo ipewe jina gani inaweza ikawa sentensi, kirai, kishazi, na neno hivyo kupitia kanuni mbalimbali za kisarufi ndipo tunapata kupitika huko Kati ya kategoria za kileksika na kategoria za tungo Kama tungo neno, kirai, kishazi na sentensi.


MAREJEO.
TUKI, (2004), Kamusi ya Kiswahili Sanifu Chuo Kikuu cha Dar es salaam.
Massamba na Wenzake (20012), Sarufi ya kiswahili sanifu (samakisa) Sekondari na Vyuo  Dar es salaam.
Ndugu, A E, bubwa, H,N, mirkau, S.A, (2014), Kamusi teule ya kiswahili, Nairobi, Kampala, Dar es salaam,Kingali.
Kiwere A.D, (2007) Ukuaji wa Kiswahili na ustawi was Jamii ya wazungumzaji wake Dar es salaam.

Comments

Post a Comment

Popular posts from this blog

Information technology

MKATABA WA KUPANGA NYUMBA

Unominishaji,