Sanaa


Sanaa ni ufundi  anaotumia mwanadamu ili kufikisha fikra au mawazo yaliyo  ndani ya akAAili yake vilivile sanaa ni uzuri unaojidhihirisha katika umbo lililosanifiwa, hivyo kazi yoyote ya sanaa inategemea ioneshe ufundi wa hali ya juu ili iwe na mvuto kwa hadhira yake. Kuna aina nane za sanaa ambazo ni sanaa za maonesho, sanaa za uchongaji, sanaa za uchoraji, sanaa za ufinyanzi,  sanaa za ufumaji,  sanaa za ushonaji,sanaa za ususi na sanaa za utarizi, pia kimsingi fasihi ni aina moja wapo ya kazi ya sanaa ambayo inatumia lugha.
Ni kweli kwamba sanaa si halisi zaidi kuliko uhalisia wenyewe na haina ukweli zaidi kuliko ukweli wenyewe, kwa hoja zifuatazo kama zilivyo ainishwa hapo chini,
Wahusika, wahusika ni viumbe vyovyote vinavyotumika katika  ya sanaa, msanii huwachora wahusika katika sura mbalimbali akirejelea tabia ama hulka za watu kutoka katika jamii husika, mfano katika tamthiliya ya Kilio chetu msanii amemchora Joti kama mhusika mwenye tabia ya umalaya lakini tabia  hii inapatikana katika jamii zetu, hivyo sanaa si halisi kuliko uhalisia wenyewe  na pia haina ukweli zaidi kuliko ukweli wenyewe kwa sababu kwa huiga  tabia za watu kutoka katka jamii zetu na kuwachora wahusika katka kazi yake.
Mandhari, ni mahali popote ambapo tukio la kifasihi hutendeka , masanii huchora mandhari mbalimbali  kaitka  kazi zake akirejelea mandhari  halisi katika mazingira halisi yanayo patikana katika jamii, mfano katika riwaya  Usiku utakapokwisha msanii ametumia mandhari halisi, mandhari hayo yanapatikana katika jiji la Dar ES Salaam kama eneo linalojulikana kwa jina la Tandika na Manzese, hivyo sanaa si halisi kuliko uhalisia wenyewe na pia haina ukweli zaidi kuliko ukweli wenyewe kwa sababu  hutaja maeneo halisi katika kazi zao
Mtindo, ni upekee wa mwandishi, upekee huo ambao humtofautisha na watunzi wengine, mtindo hutofautiana kati ya mtunzi mmoja na mtunzi mwingine, msanii huiga mitindo mbali mbali ambayo inapatikana katika jamii zetu mfano katika tamthiliya ya orodha msanii ametumia mbinu ya barua, kiuhalisia mbinu hii hupatikana katika mazingira yetu halisi , hivyo sanaa si halisi kuiliko uhalisia wenyewew na pia haina ukweli zaidi kuliko ukweli wenyewe kwasababu mitindo kadhaa ambayo hutumiwa  hutoka katika jamii zetu
Muundo, ni mpangilio wa kiufundi anaoutumia mtunzi kupangilia kazi yake , kuna aina tatu za miundo ambazo ni muundo wa moja kwa moja, muundo wa rejea ama kioo, muundo rukia, kwa mfano katika riwaya ya takadini msanii ametumia muundo wa moja kwa moja,  hivyo sanaa si halisi kuliko uhalisia wenyewe na pia haina ukweli zaidi kuliko ukweli wenyewe kwa sababu miundo yote hii inapatikana katika jamii zetu halisi na sanaa uiga tu.
Matumizi ya lugha, matumizi ya lugha ndio mzizi wa fasihi. Matumizi ya lugha ni ustadi wa kuyaibua mawazo yaliyomo katika jamii kwa kuisuka na kuifuma lugha kiufundi na kuifanya ionekane ya kifasihi, matumizi ya lugha hujidhihirisha kwa namna tatu ambazo ni tamathali za semi, semi na mbinu nyingine za kisanaa, wasanii katika kazi zao hutumia lugha na lugha hizo hupatikana katika jamii zetu, mfano katika tamthilya ya kilio chetu msanii ametumia tamathali za semi , hivyo sanaa si halisi kuliko uhalisia wenyewew na pia haina ukweli zaidi kuliko ukweli wenyewe kwa sababu tuhumia lugha ambazo msingi wake binadam anaepatikana katika mazingira halisi.
HITIMISHO
Kwa ujumla sanaa si halisi na wala haina ukweli zaidi kuliko ukweli wenyewe kwa kuwa huiga kila kitu katika jamii husika, msanii hurejerea mambo halisi ambayo hupatikana katika mazingira halisi, na kwa kiasi fulani huongeza ubunifu katika utunzi wa kazi zake.

 MAREJELEO
Bakari, Juma A.,& Mterego, Gonche R. 2008. Sanaa kwa Maendeleo :Stadi, Mbinu na Mazoezi. Moshi:Viva Productions



Comments

Popular posts from this blog

International Law

KATIBA YA KIKUNDI