Tafuta utendi wowote kisha onesha mfumo wake wakupagawisha kama unavyoelezwa na plato .




UTANGULIZI
Mulokozi: (1994) anaeleza  kwamba utendi  ni ushairi wa  matendo. Ni utango  mrefu  wenye  kusimulia  matukio  yakishuja awenye  uzito  wa kijamii  au kitaifa .matokoe  hayo  yanaweza  kuwa  ya  historia  ya kisale.
ufafanuzi huu wa mlokozi,, umepiga  hatua mbele kwa  kueleza  utendi  kama  ushauri wa matendo . Utendaji  hufungamana na matendo wakati  wa utendaji  wake , matendo  hayo  huathirika utendi unapokuwa  katika  maandishi .
Plato alizaliwa 427 bk kabla ya kristo alitoke katika ukoo wa kasomi, alikuwa mshairi  maarufu  sana huko ugiriki, plato alisoma falsafa chini ya mwalimu wake  socrate lakini baadaye  alisoma  hisabati ,sayansi   na sheria .Plato alianzisha academia yake mwaka 387 na alifundisha masomo
sheria, na  sayansi.Kazi alizozitioa  ni kama vile   the republic pamoja na law, Plato alifariki  347 kk
Kwa   kutumia  utendi  wa  fumo  Liyongo uliotungwa na bwana  Muhamadi  Bin  Abubakar  bin  Omar  Al  Bakry   aliyejulikana  jina Muhamadi Kijumwa  mwaka 1913, umeweza kudhihirisha  dhana  ya kupagwisha (mfumo  wake  kupagawisha) kama  iliyoelewa  na Plato.
i)Dhana ya kimungu ; kwa  mujibu  wa plato anaamini  kwamba mshairi anapata uwezo  wa  kuandika  mashairi  kutokana  kwa mungu  wa sanaa  anayeitwa "muses" ambaye ndiye anawapa jaziba  ya kutunga  au  kuandika mashairi au  tendi mbalimbali .- Waashairi wengi katika  kazi zao huaneza  kwa kumshukuru mungu wao katika beti zao mwanzo .mfano katika utendi wa fumo  liyongo  ulioandikwa  na Mohamedi   Kijumwa  katika beti za mwanzo aliweza   kumushukuru  mungu .
1 . Bismillahi nabutadi
kwa ina la muhamadi
nandikie au ladi
nyuma watakao kuya.


2.Unipe wino mweusi
 na ya shamu karatasi
na kalama la unyasi
umpe kuyandikiya

ii) Tungo ndefu; Ni idadi ya uwingi wa beti katita tungo, kwa mujibu wa plato, anasema  kwamba mwandishi  akisha  pagawishwa au  kupata  jazibu ,ndipo  anapata  ufunuo  au uwezo wa  kutunga  tungo  ndefu  zaidi .mfano   mwandishi   Mohamedi  Kijumwa (1913)kutokana  na  kupagawishwa aliweza kutunga  tungo  ndefu  zenye  zaidi  ya  beti  elfu moja  katika utendaji  wa fumo  liyongo .
iii)kujirudia rudia kwa tungo  au mistari  katika  beti  .plato  anaeleza  kwamba  kutokana  na mwandishi  kupagawisha na mungu  wa sanaa  anayeitwa moses  anapata  uwezo   wa  kuandika  kazi  wa  msisitizo  wa jambo  Fulani,  hali imejitokeza  katika  utendi  wa  fumo liyongo  katika  beti  na  190   na  191
190.     Mamakwe wabanwendeya
kwa lyongo wufe piya
mama cheri sikiliza
ruhu zimo hupotera
191      Mamakwe  wakamwendeya
Naye  mana  baridhia
Wakatoka  kwa umoja
nde wala sikiliya
katika, beti hisi mbili msitari  wa kwanza  wa  kila  beti  umeweza kufanana

iv) Msani  alishapagawishwa na  mungu  moses" - huweza kuandika  mambo  mabilmbali  ambayo   wanajamii  hukumbana  nayo   .mfano  wa  mambo  hayo ni  kama vile  mapenzi  ,utawala  matabaka  dhumuna  na rushwa .Mwandishi  huandika  mambo hayo  ili  kuwaelimisha  wanajamii  kuhusu  mambo  hayo  na pia huonesha  ni ki vipi  jamii  itaweza  kutatua matatizo  hayo .katika utendaji  wa  fumo  liyongo  tunaona  linatokea ,Mohamedi kijumwa amewewza  kueleza  masuala  ya mapenzi  katika ubeti  wa  47 .
47. kamuyeya kimtunda
Kwa  mahaba kimpenda
Kama wa matoni wanda
Na kwa f`unu na kidaya
Pia  Mohamed kijumwi  ameweza kueleza  masuala  ya  dhuruma  katika ubeti  wa  101
101 .     Na mamake kwa hakika
            Chakula cherna  kipika
Asikari humpoka
Chakula wakailiya .
HITIMISHO
Kwa  ujumla plato amefanikiwa kueleza  ushairi  kwa kiasi kikubwa na kutoa maoni na mapendekezo kuhusu ushairi au utendi, na ametoa  mchango   kuhusu sanaa na  kuonesha ni jinsi  wasanii  walio wengi huweza  kupagawishwa  na  mungu wao  wa sanaa  moses.  kwa mfano  msaanii  Mohamedi  Kijumwa  katika  utendaji  wake  wa  fumo  liyongo  amedhihikisha  mawazo  ya plato .

MAREJEO.
Kijumwa, M. (1913), Utenzi  wa fumo liyongo . Da- r es salaam :  IKR
Mulokozim.,M.M ( 1999 ) , Utenzi  Tatu za Kale : Chuo  kikuu  cha Dares salaam .TUKI


Comments

Popular posts from this blog

International Law

KATIBA YA KIKUNDI