Utafiti


UTANGULIZI.
Utafiti ni uchunguzi unaotumia mbinu za kisayansi katika kutafuta taarifa juu ya jambo Fulani.Kuna aina mbili za utafiti ambazo ni utafiti wa msingi na utafiti wa matumizi.
Utafiti wa msingi hutumika zaidi na wanasansi kama vile wana falsafa ili kukuza nadharia mbalimbali kwa njia ya ugunduzi wa msingi na kanuni mbalimbali.
Utafiti wa matumizi ni utafiti unao kazia matumizi ya matokeo ya utafiti huo katika kutatua matatizo na kufanya shughuli Fulani iwe bora zaidi.
Katika kazi hii tutatumia aina ya pili ya utafiti ambayo ni utafiti wa matumizi kulingana na suala la utafiti tulilochagua pamoja na malengo ya suala hilo.
SUALA LA UTAFITI
UMUHIMU WA KUWEPO KWA ADHABU SHULENI SHULE YA MSINGI LUPASO MASASI
Mhusika wa suala tunalolitumia katika kuboresha matokeo ya utafiti ni ndugu Eriyo Ismail H.ambaye katika utafiti wake alikuwa na malengo yafuatayo:
Malengo makuu
Utafiti ulijikita katika kubainisha umuhimu wa kuwepo kwa adhabu mashuleni.
Malengo mahususi
Namna ya kutoa adhabu kwa wanafunzi.
Namna adhabu inavyoweza kuamsha ari ya wanafunzi kujifunza.
Baada ya kufanya utafiti matokeo ya ripoti ya utafiti yaliwasilishwa kama ifuatavyo:
·         20% ya sampuli waliunga mkono umuhimu wa kuwepo kwa adhabu mashuleni
·         20% ya sampuli wamesema kuwa ni sahii kutofautisha namna ya kutoa adhabu kwa waschana na wavulana.
·         20% ya sampuli wamesema kuwa huamsha ari ya wanafunzi kujifunza
·         15% ya sampuli wamesema kuwa kuna athari ya kutowepo kwa adhabu shuleni.
·         10% ya sampuli imesema kuwa adhabu zitolewazo mashuleni hazilingani na makossa ya wanafunzi.
·         15% ya sampuli imesema kuwa kuwepo kwa adhabu mashuleni ni chanzo cha watoto kutoendelea na masomo.

Kutokana  na matokeo ya tafiti saidizi tulio yapata tumeweza kuandaa mpango wa kuinua ubora wa ujifunzaji na ufundishaji kwa kuzingatia vipengele vifuatavyo:

MIKAKATI KATIKA UTOAJI WA ADHABU SHULENI.
Kuwepo kwa sheria na kanuni zitakazo ongoza utoaji wa adhabu kwa wanafunzi; serikali pamoja na wadau mbalimbali wa elimu wanapaswa kuona umuhimu wa adhabu na hivyo kutilia mkazo kwa kuweka sheria na kanuni ambazo mtoa adhabu  anapaswa kuzifuata wakati wa kutoa adhabu kwa mfano kuwepo na utaratibu unao tofautisha namna ya kutoa adhabu kwa mvulana na mschana mfano mvulana kuchapwa fimbo matakoni na mschana kuchapwa mkononi aidha utowaji huo wa adhabu hasa ya viboko uzingatie na tofauti za jinsia.
Kuweka wazi malengo ya utoaji wa adhabu shuleni; Walimu wanapaswa wanapotoa adhabu kubainisha kwanini wanampa adhabu mtoto kutokana na kosa lililotendeka ili kuonesha kuwa lengo ni kumuonya au kumuelimisha na si kumkomoa mwanafunzi ili kumuwezesha kufikia malengo ya kielimu.Mfano mwanafunzi atakae feli atarudishwa darasa, hivyo itamjenga katika ari ya kusoma kwa bidii.

Kuanisha aina ya makosa pamoja na adhabu kulingana na kosa hilo;Ili kuwandaa wanafunzi kuwa na nidhamu nzuri wawapo mazingira ya shule au nyumbani ni vyema wanafunzi waambiwe makosa na adhabu yake atakayo paswa kupewa mkosaji.Mfano mwanafunzi akibainika kwa kosa la wizi adhabu ni kusimamishwa masomo kwa muda wa kipindi Fulani.Hii itasaidia watoto kupatiwa adhabu zinazo lingana na kosa husika.

Adhabu kutolewa kwa wakati ;Endapo mwanafunzi amefanya kosa mwalimu anapaswa kutoa adhabu papohapo ili mwanafunzi kutambua kosa alilotenda.Kutofanya hivyo huweza kusababisha kujengeka kwa uhasama baina ya walimu na wanafunzi kwani mwanafunzi atahisi ameonewa endapo atasahau kosa lake.

Kuwepo kwa motisha kwa wanafunzi wenye nidhamu; Uongozi wa shule husika unatakiwa kuweka siku maalum kwaajili ya kutoa zawadi kwa wanafunzi watakao fanya vizuri kinidhamu.Hii itafanya wanafunzi kujiweka mbali na makosa kwa lengo la kuwania zawadi ya nidhamu.Mfano katika shule nyingi kipindi cha mahafali au kufungwa kwa shule wanafunzi waliofanya vizuri klipindi chote cha mafunzo ndipo utunukiwa zawadi.

KUWASHIRIKISHA WADAU KATIKA UTEKELEZAJI WA MIKAKATI YA KUBORESHA MATOKEO YA UTAFITI.
Ili kufanikisha mikakati tuliyo ipanga tunapaswa kushirikisha wadau tofauti tofauti wa elimu kwa namna zifuatazo.

Kuwepo kwa vikao vya mara kwa mara; Uongozi wa shule upange siku za vikao vya shule vya mara kwa mara kwa kila mwezi ili kufanya tathmini za maendeleo ya kinidhamu ya taaluma shuleni na hata nyumbani .Hivyo wadau kwa kupitia vikao huweza kutoa maoni yao katika kudhibiti nidhamu kwa wanafunzi.Mfano kupanga adhabu zinazostahiki kutolewa kwa wanafunzi.

Kuwepo kwa semina elekezi kwa walimu kuhusu utoaji wa adhabu; walimu wapatiwe mafunzo ya ndani yanayohusu namna bora ya kutoa adhabu kwa wanafunzi ili kuzingatia wakati sahihi wa utoaji wa adhabu,namna sahihi,adhabu sahihi kuzingatia jinsia na kuepuka utoaji wa adhabu kwa kuongozwa na hasira.Kwahiyo utoaji wa adhabu uweze kuzingatia sheria na taratibu sahihi kwa mwanadamu.

Kutoa elimu kwa jamii kuhusu umuhimu wa adhabu kwa mwanafunzi;walimu kwa kushirikiana na serikali wanatakiwa kuweka vikao na wanajamii kwa ajili ya kutoa elimu juu ya adhabu kwa wanafunzi kwani kuna wazazi wengine huwa wanakuja juu pale watoto wao wanapopatiwa adhabu shuleni.Mfano kuna wazazi wanadiliki kwenda shuleni kutoa maneno makali kwa walimu pale wanapopata taarifa kuwa mtoto wake kaadhibiwa na hii yote ni kwa sababu huwa hawajui ni kwanini walimu huwa wanatoa adhabu kwa wanafunzi pindi wanapokosea na elimu hii inaweza kuwasaidia wazazi kutoa adhabu pindi watoto wao wanapokosea wawapo nyumbani.
Kuhamasisha vyombo vya habari kuelezea kuhusu adhabu;kwenye vyombo vya habari kama vile redio,magazeti na televisheni viwepo vipindi vinavyotoa mafunzo kuhusu utoaji sahihi wa adhabu au kutoa taarifa kuhusu madhara ya utoaji wa adhabu pasipo kuzingatia sheria na kanuni.Kwa mfano taarifa za mwalimu aliyechapa mwanafunzi hadi kufa zilipotolewa walimu wengi walijifunza kutokana na hilo hivyo imepunguza kasi kwa walimu wenye kutoa adhabu bila mpangilio.

KUSIMAMIA UTEKELEZAJI WA MIKAKATI YA KUBORESHA ELIMU
Kutunga sheria na kuweka kanuni,kuzisambaza kwa watumiaji na kuhuakikisha zinzfuatwa kama zilivyokusudiwa.Ili kusimamia mkakati huu serikali inapaswa kutunga sheria ambazo zitawaongoza walimu katika kutoa adhabu pamoja na kuzisambaza sheria hizo ili ziweze kutumika na kila mtu.

Kutoa adhabu zenye uwiano na makosa;ili kupunguza kasi ya wanafunzi kukimbia shule walimu wanatakiwa kutoa adhabu kulingana na makossa yanayofanywa na wanafunzi,kwa mfano mwanafunzi akipigana na mwenzake asipewe adhabu kubwa kama kuchimba visiki au kukusanya ndoo nyingi za kokoto kwani adhabu kama hizi zinawapelekea wanafunzi kuacha shule na hivyo kutofikia malengo ya elimu.

Kuwaadhibu wanafunzi pale tu wanapokosea ili kutowaharibu kisaikolojia;walimu hawana budi kutoa adhabu pindi tu wanafunzi wanapokosea kwani kuchelewesha adhabu kunaweza kuwaathiri kisaikolojia.kwa mfano mwanafunzi anapokosea na akafahamu kuwa amekosea asipopatiwa adhabu anaweza kukosa amani kwani hajui atapatiwa adhabu gani au muda mwingine anaweza kusahau kosa na atakapopatiwa adhabu atahisi ameonewa na hivyo kuharibiwa kisaikolojia.

Kugawa madaraka kwa walimu ili kurahisisha ufuatiliaji wa nidhamu shuleni;shule inatakiwa kugawa madaraka kwa kuunda kamati mbalimbali kwa kufanya hivyo kutarahisisha ufuatiliaji wa wanafunzi katika sekta mbalimbali.kwa mfano kamati ya nidhamu itafuatilia nidhamu,kamati ya taaluma itafuatilia taaluma,kamati ya afya itafuatilia mambo ya afya hivyo kufanya wanafunzi kuweza kufuatiliwa kwa urahisi katika ngazi zote.



Kuwepo na siku maalumu za kutoa tuzo kwa wanafunzi wenye nidhamu;uongozi wa shule unatakiwa kupanga siku ya kutoa zawadi kwa wanafunzi kwa kufanya hivi kutawasaidia walimu kupata wanafunzi wenye nidhamu na kupunguza wanafunzi wasio na nidhamu.kwa mfano siku za kufunga shule au za mahafali zawadi zikitolewa wanafunzi wanapatwa na hamasa ya wao kuwania zawadi.

KUFANYA TATHMINI YA UTEKELEZAJI WA KUINUA UBORA WA ELIMU
Tathmini ni kitendo cha kutaka kujua ni kwa kiasi gani jambo lilikusudiwa kutekelezwa limefikia mafanikio au la.kuna aina nne za tathmini ambazo ni
Tathmin ya awali
Tathmini endelevu
Tathmini tatuzi
Tathmini tamati
Katika kutathmini matokeo ya utafiti tumetumia tathmini tatuzi na tumetumia tathmini tatuzi kwa lengo la kuboresha matokeo ya utafiti katika kuinua ubora wa elimu na baada ya kutekeleza mikakati iliyopangwa tunapata majibu kuwa adhabu zimeleta mabadiliko baada ya wanafunzi  kuomgeza ari ya kujifunza na hatimae kupanda katika taaluma,kuimarika kimaadili pamoja na kuongeza ushirikiano baina yao na kupunguza utoro mashuleni.

HITIMISHO
Kulingana na mipango ya kuboresha elimu tuliyoipanga ni matarajio yetu kwamba adhabu ni chachu pekee inayoweza kumfanya mwanafunzi kubadilika katika mtazamo chanya na kuwa mzuri kinidhamu taaluma na maadili na hatimaye kuja kuwa mtendaji bora hapo baadae kwa ajili yake na taifa kwa ujumla ikizingatia adhabu hasi au chanya.


MAREJEO.
Pletty rogic.(2009) usimamizi wa nidhamu na maadili kazini.Zanzibzar
Eriyo I.(2018) Umuhimu wa kuwepo kwa adhabu mashuleni.Stemmuco Mtwara.

Comments

Popular posts from this blog

International Law

KATIBA YA KIKUNDI