SW111: UTANGULIZI WA MISINGI YA ISIMU


CHUO KIKUU KISHIRIKI CHA STELLA MARIS MTWARA
(Chuo Kishiriki cha Chuo Kikuu cha Mtakatifu Agustino - Tanzania)
Anwani:
S.L.P. 674
MTWARA
TANZANIA
 
Simu : +255 232 334 482
Faksi: +255 232 334 483
 
STEMMUCO 2
KITIVO CHA ELIMU
IDARA YA KISWAHILI

SW111: UTANGULIZI WA MISINGI YA ISIMU
SEMISTA YA KWANZA: 2019/2020

Utangulizi
Hii ni kozi ya utangulizi inayoweka msingi wa kumwezesha mwanafunzi kuielewa isimu kama taaluma; muundo wa mfumo wa lugha na jinsi lugha inavyofanya kazi. Ni kozi inayolenga hasa kumwezesha mwanafunzi kuelewa uchangamano wa lugha ya binadamu kama mfumo unaoongozwa na kanuni za lugha kwa jumla na kanuni za lugha maalumu.

Malengo ya Kozi
Kozi hii imenuiwa kumwezesha mwanafunzi:
a)      Kuieleza isimu kwa kufafanua viwango na matawi yake.
b)      Kueleza kitaaluma maana ya lugha, sifa zake, na kutathmini nadharia mbalimbali za asili ya lugha.
c)      Kuchambua, kuchanganua na kuziainisha sauti zinazopatikana katika lugha za binadamu; usikiaji na  utamkaji wake.
d)     Kuchunguza kuchambua na kuainisha sauti pambanuzi ambazo hutumika katika mifumo mbalimbali ya sauti za lugha za binadamu.
Matokeo ya Ujifunzaji
Kufikia mwisho wa kozi hii, mwanafunzi ataweza:
a)      Kueleza kitaaluma maana na sifa za lugha.
b)      Kufafanua viwango na matawi ya isimu.
c)      Kutathmini nadharia mbalimbali za asili ya lugha.
d)     Kuainisha sauti zote za lugha ya binadamu katika makundi na kuzitolea sifa ambazo zinaweza kutofautisha sauti moja na nyingine.
e)      Kuainisha sauti pambanuzi ambazo hutumika katika mifumo mbalimbali ya sauti za binadamu.


Kiunzi cha kozi
1.0 Utangulizi
1.1 Maana na sifa za lugha
1.2 Asili ya lugha
1.3 Sifa bia za lugha
1.4 Maana na malengo ya Isimu
1.5 Usayansi wa Isimu
1.6 Historia ya taaluma ya Isimu

2.0 Tanzu za Isimu
2.1 Viwango vya simu
            2.1.1 Fonetiki
            2.1.2 Fonolojia
            2.1.3 Mofolojia
            2.1.4 Sintaksia
            2.1.5 Semantiki na Pragmatiki

2.2. Matawi ya Isimu
            2.2.1.Isimu Historia
a)   Isimu Elekezi
b)      Isimu Elezi
            2.2.2 Isimu Jamii
            2.2.3 Isimu Linganishi
            2.2.4 Isimu Tumizi n.k

3.0 Fonetiki
    3.1 Dnana ya Fonetiki
    3.2 Matawi ya Fonetiki
    3.3 Fonetiki Matamshi
    3.4 Ala za Matamshi
    3.5 Uanishaji wa sauti za lugha
    3.6 Alfabeti ya Kifonetiki ya Kimataifa (AKIKI)

4.0 Fonolojia 
    4.1 Dhana ya Fonolojia
    4.2 Vipashio vya kifonolojia: Fonimu na Alofoni
    4.3 Majukumu ya Fonolojia
    4.4 Uhusiano kati ya Fonetiki na Fonolojia
    4.5 Tofauti kati ya Fonetiki na Fonolojia


Marejeo
Habwe, J.H. na Karanja, P. (2004), Misingi ya Sarufi ya Kiswahili. Nairobi: Phoenix Publishers
Massamba, D.P.B., Kihore, Y.M., & Msanjila, Y.P. (2004). Fonolojia ya Kiswahili Sanifu. Dar es Salaam: TUKI.
Mdee, J.S. (1988). Sarufi ya Kiswahili: Sekondary na Vyuo. Dar es Salaam: Dar es Salaam University Press.
Mohammed, M.A. (2001). Modern Swahili Grammar. Dar es Salaam: East African Educational Publishers.
Mgullu, R. S. (2002). Mtalaa wa Isimu, Fonolojia, na Mofolojia ya Kiswahili.
Nairobi: Longhorn.
Njogu, K. et al. (2006). Sarufi ya Kiswahili: Uchanganuzi na Matumizi. Nairobi: The Jomo Kenyatta Foundation.
Nkwera, F. (1978). Sarufi na Fasihi: Sekondari na Vyuo. Dar es Salaam: Tanzania Publishing House.
O’Grady, W. et al. (1996). Contemporary Linguistics: An Introduction. London: Longman.
Oduor, J.A. (2012). Teaching Pronunciation in Secondary Schools in Kenya: The Necessity to Use the Right Information and Descriptive Tools. The University of Nairobi Journal of Language and Linguistics, Vol. 2. June, 2012. Kurasa 1 – 41.
Robins, R. (1984). A Short History of Linguistics. New York: Longman.
TUKI (1990). Kamusi Sanifu ya Isimu na Lugha. Dar es Salaam: Taasisi ya Uchunguzi wa Kiswahili, Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.
Yule, G. (1996). The Study of Language. Cambridge: Cambridge University Press.


Tathmini
Tathmini ya somo itahusisha mahudhurio ya wanafunzi katika mihadhara, insha, alama za majaribio (40%) na alama za mtihani wa mwisho (60%)




Comments

Popular posts from this blog

International Law

KATIBA YA KIKUNDI