SWALI: “Ili pawe na Riwaya ya Kiswahili hapana budi pawepo na jamii yenye lugha hiyo’’.Huku ukizingatia kauli hiyo,ijadili hali ya riwaya nchini Tanzania. 1.0: UTANGULIZI.
SWALI: “Ili pawe na Riwaya ya Kiswahili hapana budi
pawepo na jamii yenye lugha hiyo’’.Huku ukizingatia kauli hiyo,ijadili hali ya
riwaya nchini Tanzania.
1.0:
UTANGULIZI.
Riwaya;
Ni hadithi ya kubuni na
iliyojengwa juu ya tukio la kihistoria na kuandikwa kwa mtindo wa ushairi
iendayo katika mfululizo wa kinaganaga katika kuelezea maisha ya mtu,watu na
hata taifa .
Kutokana
na maana ya Riwaya wataalamu mbalimbali wameweza kutoa fasili tofauti tofauti juu ya
dhana nzima ya Riwaya nchini Tanzania kama ifuatavyo,
Riwaya,
ni kazi ya sanaa ya kubuni yenye nathari (ujazo) yanayosimulia hadithi ambayo kwa kawaida ina uzito, upana
na urefu wa kutosha mara nyingi huwa wahusika mbalimbali, wahusika wanatabia
aina nyingi,huwa na migogoro mikubwa na midogo ndani yake.Mbunda M.(1992).
Wamitila,(2003), Riwaya ni hadithi ya kinathali au
bunilizi ambayo huwa na urefu wa kutosha msuko uliyojengeka vizuri, wahusika
wengi waliondelezwa kwa kina yenye kuchukua muda mwingi katika maandalizi yake
ikihusisha madhari maalumu.
Madumulla, (2009), Riwaya ni masimulizi ya kubuni yaliyo
katika mtindo wa kubuni yakisawili mtindo maalumu na madhumuni maalumu.Mhusika
katika riwaya anakuwa kipaza sauti cha maandishi.
Kwa ujumla;
Riwaya,
ni masimulizi ya kubuni ya kinathari yenye msuko au mpangilio fulani wa matukio
au ploti inayofungamana na wakati au kusawili wakati na yenye visa vyingi
vinavyotendeka katika wakati Fulani na
yenye mawanda mapana yenye mchangamano wa dhamira visa na wahusika pia riwaya
ni hadithi ndefu yenye uwezo wa kutosha kufanya kitabu kimoja au zaid.i
Riwaya ya Kiswahili,ni
Riwaya ambayo inayofungamana na
utamaduni wa jamii wa Kiswahili katika lugha ya Kiswahili asili ambayo
hupatikana katika nchi ya Afrika mashariki,pia ni ile Riwaya ambayo inawahusu
waswahili wenyewe.
1.2 Historia katika Riwaya ya Kiswahili;
Tanzu za asili
zinaonyesha kuwa Riwaya ndio zilichangia
kwa kiasi kikubwa riwaya za Kiswahili.kuna wataalamu mbalimbali wamejadili
kuhusu historia ya riwaya kama ifuatavyo,
Madumilla(2009), ameeleza kuwa chimbuko la riwaya lilitokana na nathari bunifu simulizi kama
vile hadithi, hekaya na ngano
inayosimuliwa kwa mdomo.Anaendelea kusema kuwa fasihi ilitokana na maandiko ya
fani ya ushairi hususani ni tendi za
Kiswahili katika hati za kiarabu kwa sababu ndiyo maandishi yaliyotamba katika
pwani ya Afrika mashariki,wazungu na waarabu hawakubadilishana maarifa kwa
urahisi na hivyo pakapelekea kuwa na majilio ya taratibu za maandiko ya
kinathari,mwanzani Riwaya zilitafsiriwa toka katika lugha za ulaya na kufanya
Riwaya za za Kiswahili kutokea.Mfano wa riwaya hizo ni kama vile,Habari za
mlima iliyoandikwa na Sheikh Ali Bin Hemed (1980).
Mulokozi,(1996)
anaeleza kuwa riwaya Kiswahili ipo katika mambo makuu mawili ambayo ni fani za
kijadi za fasihi mfano Riwaya za
kingano,tendi,hekaya,visakale,historia,sira,masimulizi ya wasafiri,insha na
tafsiri.Pia riwaya ya kiswahili imetokana na mazingira ya kijamii mfano
njaa,migogoro,masuala ya kisiasa pamoja na kiuchumi.
Hali ya riwaya nchini Tanzania kisiasa,
Waandishi
mbalimbali wameandika kazi mbalimbali zinazozungumzia maswala ya kisiasa
riwaya zinazoeleza hali ya watu kutaka kupinga au kukubaliana na uongozi fulani
mfano, Shabani Robert katika riwaya yake ya Kusadikika ameeleza dhamira
mbalimbali zinazohusika katika jamii mfano, uongozi mzuri.amemtumia Bunihari
kama kiongozi bora anayesimamia haki za
jamii.uongozi mbaya pia katika riwaya ya
Kusadikika, amemchora waziri mkuu kama kiongozi mbaya. Hivyo ndivyo hali riwaya ilivyo kisiasa katika nchi ya
Tanzania.
Kiutamaduni;
Hali ya riwaya ya Kiswahili nchini Tanzania
kiutamaduni, riwaya mbalimbali zimeandikwa kueleza hali mbalimbali za
kiutamaduni nchini Tanzania ambapo riwaya hizo zimeelezea uhusiano baina ya
mila na desturi , mfano Mung’ong’o,C.G. katika kitabu chake cha Mirathi Ya
Hatari k ameelezea mila na tamaduni za jamii katika kurithisha tamaduni amemtumia mhusika wake Guston ambae ameeleza kuhusu mila na tamaduni
za kichawi baada ya wazazi wake kufariki hii inaeleza uhalisia hata watu
watanzania walio wengi wanarithishana tamaduni hizo mfano kabila la Wasukuma,Wamasai
huwarithisha mila zao ili waweze kuishi
na kuuenzi utamaduni wao.
Kijamii;
Riwaya
mbalimbali zimeandikwa kuelezea hali ya matatizo yanayowakumba wananchi katika
maisha halisi ya kila siku mfano ukosefu wa maji, hali duni ya maisha,
mazingira magumu ya kufanyia kazi, mazingira mabaya ya kuishi na hali ya
umaskini.mfano, mwandishi Muhammed S. Abdulah katika kitabu chake cha Mzimu wa
Watu wa Kale,(1996) ameeleza masuala mbalimbali ya kijamii. mwandishi ameeleza
maisha ya bwana Musa ambae anaishi katika hali duni pia anaishi kwa kujibana,
nyumba anayoishi ni ya kimasikin vitu vimejipanga ovyo ovyo hii inaonesha uhalisia
wa maisha na kuonesha watanzania wanavyo pambana na kutokana na hali ngumu ya
maisha kujiweka katika hali nzuri ya maisha.
Hali ya riwaya kiuchumi;
Riwaya nchini Tanzania
imeonesha pia maendeleo makubwa katika nyanja mbalimbali za kiuchumi.mfano
katika kitabu cha Mzimu wa Watu wa Kale kilichoandikwa na Mohammedi S. Abdullah
amejaribu kuonesha suala la kiuchumi jinsi lilivyo katika jamii, mfano,
tunamuona Bwana mussa alipokuwa akiishi maisha duni kama vile kukosa chakula
pia hata nyumba aliyokuwa anaishi haikuwa bora .pia tunamwona bwana Alli
alimposa mwanamke akashindwa kutoa mahari na kuishia kutoa ahadi tu, hivyo basi
imenajidhihirisha wazi kuwa hali ya kiuchumi haikuwa nzuri.
Mandhari
au mazingira; Riwaya nyingi za Kiswahili zinaandikwa kwa kuzingatia mazingira
ya jamii husika ya watanzania .pia katika matumizi ya madhari riwaya
nyingizinatumia madhari ya kubuni riwaya nyingi zinatumia madhari kama maisha
mbani mito makaburi jangwani mfano katika riwaya ya nagona ametumia madhari ya
kubuni na halisi kama makaburi jangwani na za kimaujiza.
Matumizi ya lugha ; riwaya nyingi za Kiswahili zinatumia
lugha ya Kiswahili ambayo inaeeleweka na jamii nyingi za watanzania katika
kufikisha ujumbe wakusudiwa kwa jamii husika mfano riwaya za Kusadikika,Mzimu
wa Kale na Moto wa Mianzi zimetumia lugha ya Kiswahili ambayo inaeleweka na
jamii za watanzania.
Kutokana na hali ya
riwaya nchini Tanzania kwa miaka kadhaa iliyopita na tokea muda wa kupata uhuru
riwaya ya Kiswahili imeweza kuleta mabadiliko mbalimbali katika nyanja za
kijamii,kisiasa,kiutamaduni pamoja na kiuchumi.Japokuwa riwaya ya Kiswahili
imeweza kuleta mabadiliko hayo lakini zipo changamoto mbalimbali ambazo
zinaikumba riwaya ya Kiswahili nchini Tanzania matatiza hayo hujitokeza kupitia
suala la uandaaji,uchapishaji,usambazaji pamoja na usomaji wa kazi mbalimbali
za riwaya ya Kiswahili.
Comments
Post a Comment