Zifuatazo ni hoja zinazoonesha hali ya riwaya nchini Tanzania.


Riwayani hadithi ndefu ya kubuni yenye wahusika wengi na yenye kueleza maisha ya watu katika jamii yenye mazingira maalumu yanayochaguliwa na mwandishi, kwa kawaida huwa na visa vingi na hutumia lugha ya kinathari. Ili hali riwaya ya Kiswahili ni riwaya ambayo imeandikwa kwa lugha ya Kiswahili, huandikwa katika utamaduni wa mswahili na katika eneo la mswahili. Chimbuko la riwaya ya Kiswahili lilitokana na mambo makuu mawili ambayo ni fani za kijadi na mazingira mahususi ya kijamii, hizi ni riwaya zinazohusisha fani mbalimbali za kijadi kama vile ngano, hekaya, utendi, visasili, insha, sira na masimulizi ya kihistoria. Hivyo riwaya ziliendelea kutoka masimulizi hadi kuandikwa, hivyo basi riwaya ya kwanza kuandikwa ni riwaya ya UHURU WA WATUMWA (Mbotela 1934). Kwa ujumla ni kweli kuwa ili pawe na riwaya ya Kiswahili hapana budi pawepo na jamii ya lugha hiyo.
Zifuatazo ni hoja zinazoonesha hali ya riwaya nchini Tanzania. 
Wahusika ni viumbe hai au visivyohai ambao hutumika kuwakilisha matendo, mwenendo au tabia za binadamu wa kweli katika jamii, viumbe hawa ni wale wanaopatikana katika kazi ya fasihi. Mfano: fisi anaweza kuwa mhusika katika kazi ya Fasihi ambapo huweza kuwakilisha binadamu waroho na wajinga, waandishi wengi wa riwaya ya Kiswahili hutumia wahusika ambao majina yao hupatikana katika jamii ya watanzania na kuweza kusawiiri yaliyomo katika jamii. Pia matendo yao na majina yao ni yale ambayo yanapatikana katika jamii ya Tanzania. Mfano: Katika riwaya ya “rosa mistika” iliyoandikwa na Euphrase Kezilahaba pamoja na riwaya ya “MIRATHI YA HATARI”iliyoandikwa na C.G Mung’ong’o waandishi hawa wametumia majina ya wahusika ambayo yapo katika jamii zeu, kama vile, Rosa, Nandi, Rina, Gusto, Zakaria, Deogratius ambapo wahusika hawa wamebeba uhasika wa kutenda mambo yanayo sawiri katika jamii. Pia riwaya ya “WATOTO WA MAMANTILIE” iliyoandikwa na Emmanuel Mboga, tunapata wahusika kama Musa, Zainabu, Kurwa na Doto, Peter na mzee Lomolomo kupitia uhusika wao tunaweza kupata dhamira inayo sawiri hali halisi ya jamii ya Tanzania.
Hivyo basi riwaya za sasa zinazidi kuendelea kutokana na kwamba huonyesha moja kwa moja tofauti na riwaya za zamani ambapo zilikuwa zinatumia wahusika wa mficho ambao si wa moja kwa moja. Mfano: katika riwaya ya “KUSADIKIKA” Mwandishi ametumia wahusika kama “Mizimu” wakati riwaya za Kiswahili zilizo kuwa zinaandikwa zamani zilikuwa zinaandikwa kusawiri maisha ya jamii ya kipindi hicho na jinsi zilivyokuwa zinaathiri maisha yao. Mfano: riwaya ya “KUSADIKIKA(1957)” ilikuwa inaelezea jinsi watu walivyo kosa uhuru wa kuzungumza au kuhoji kuhusu masuala mbalimbali ya nchi kama vile kupata nyazifa za uongozi au kuhoji matumizi ya rasilimali za nchi lakini baada ya uhuru, riwaya zinazoandikwa saizi zinaendana na wakati na mabadiliko ya jamii za sasa. Mfano: riwaya ya “ROSA MISTIKA (1997) Inaelezea masuala ya mapenzi na ulevi ambayo ukiyaona yameshamiri jamii zetu za leo. Hivyo waandishi wengi wa riwaya za Kiswahili nchini Tanzania huandika kazi zao za riwaya kulingana  au kufuatana na hali halisi inayoendalea katika kipindi hicho au wakati huo wa maisha ya watanzania. Vipindi hivyo vinaweza kuwa vya kisiasa, kiuchumi, kijamii na kiutamaduni.
            Mandhari ni sehemu ambayo tukio linafanyika katika kazi ya fasihi. Katika kazi ya fasihi mandhari yanaweza kuwa halisi au ya kubuni. Riwaya mbalimbali za Kiswahili hutumia mandhari tofauti tofauti ambayo husadifu mazingira halisi ya Waswahili, waandishi mbalimbali wa riwaya za Kiswahili wametumia madhari mbalimbali. Mfano: mwandishi wa riwaya ya KUSADIKIKA (Shaban Robert 1957) ametumia madhari ya kaburi kama vile madhari ya mbinguni, ambayo yalitokea katika nchi ya kusadikika pia mwandishi wa riwaya ya WATOTO WA MAMA N’TILIE (Emmanuel Mboga 2002) ametumia mandhari halisi yanayopatikana katika jamii ya waswahili nchini Tanzania, mwandishi ametumia madhari ya jiji la Dar es salaam na mitaa yake mbalimbali kama vile kisutu, manzese, kiwanda cha urafiki na dampo la Tabata, hivyo Emmanuel Mboga amefanikiwa kujadili matatizo yanayoikabili jamii kwa kutumia mandhari halisi yaliyojitokeza katika riwaya hiyo. Kwa hiyo hali ya riwaya za Kiswahili nchini Tanzania ni nzuri ukilinganisha na riwaya za zamani kwa sababu waandishi wa riwaya za sasa wanatumia mandhari ambayo yanaendana na utamaduni wa waswahili.
            Ubunulizi ni ujuzi alionao mtunzi kwa kubuni na kuigiza au kutumia kazi yake ili ilete mvuto kwa hadhira. Mbinu hii huakisi kipawa cha utunzi alichonacho mtunzi na kumtofautisha  na watu wengine katika riwaya za Kiswahili waandishi wametumia ubunifu katika kazi zao za fasihi. Mwandishi wa MIRATHI YA HATARI (C.G.Mung’ong’o) ametumia dayalojia katika ukurasa wa 19, mazungumzo kati ya Gusto na Mzee Mavengi yanayohusu usihiri (ushirikina)
            Mzee Mavengi: “unaziona shanga hizi?”
            Gusto: Ndiyo
Pia mwandishi ametumia methali, nahau, matambiko na vyakula asilia kama vile mboga ya kuchemsha na viazi vya kuchemsha (uk. 03). Vilevile katika riwaya ya WATOTO WA MAMA N’TILIE (E.  Mboga) katika kukamilisha kipengele cha ubunifu ameweza kutumia Nahau “kupiga usingizi” tamathali za semi kama vile Tashibiha mfano: akaanguka chini kama mzigo (uk 12)
            Kwa hiyo waandishi wa riwaya za Kiswahili kwa sasa wanaubunifu kama riwaya za  mwanzo hivyo riwaya hizi zimeweza kuwa mwanzo hivyo kutokana na juhudi za waandishi kuwa wabunifu katika kazi zao.
            Usawilishaji ni namna ambayo waandishi wa riwaya za Tanzania wanavyoonesha uhalisia wa maisha ya watu katika jamii mbalimbali mfano: Hali ngumu ya maisha, ulevi, Dhuluma, Unyonyaji, Mapenzi, Matabaka, Mambo ya kisiasa. Mfano: tukiangalia katika riwaya ya Rosa Mistika mwandishi amezungumzia suala la mapenzi jinsi mtu anavyoharibika kutokana na mapenzi. Mfano: Rosa ambaye anajiingiza katika mapenzi na kumletea athari mbalimbali katika masomo yake. Pia katika riwaya ya watoto wa Mama Ntilie (2002) mwandishi anazungumzia hali ngumu ya maisha ambapo wazazi wanashindwa kuwalipia watoto wao ada ya shule pamoja na  kuwanunulia sare za shule, ambapo imepelekea watoto kukosa elimu na kujiingiza katika masuala ambayo yanawaletea athari katika maisha yao. Pia suala la ulevi katika riwaya hii ya Watoto wa Mama ntilie mzee Lomolomo anajihusisha na ulevi na anashindwa kulea familia yake kwa sababu pombe zimemtawala na mwisho wa siku pombe hizohizo zinakuja kumuua. Hivyo waandishi wa riwaya za kitanzania wanasawili maisha halisi ya kitanzania.
Mawanda mapana, riwaya nyingi za Kiswahili huandikwa kwa kuangalia vipengele vingi katika jamii kama vile masuala  ya kiuchumi, kisiasa, kiutamaduni na kijamii. Ili kufikisha ujumbe uliokusudiwa kwenye jamii husika na katika Nyanja zote za maisha katika jamii kwa mfano riwaya ya kusadikika mwaka (1957/58) iliandikwa ili kulenga Nyanja zote za kimaisha kama vile ujenzi wa miundombinu (kiuchumi), ujenzi wa zahanati (kijamii) na kuhusu masuala ya kiutawala (kisiasa) katika masuala ya kiuchumi hii imedhihirishwa katika ukurasa wa 43 mandishi anasema kuwa hii kusadikika ilikuwa haina haja ya kutengeneza bandari wala viwanja kwa ajili ya vyombo ya aridhi. Pia katika riwaya sasa kama vile watoto wa mama Ntilie (2002) mwandishi ametumia mawanda ya kisiasa, kiuchumi na kiutamaduni katika kuandika kazi yake kwani amesawiri hali ngumu za maisha, ulevi ana uchezaji wa ngoma za kiutamaduni, hivyo basi ni dhahili kuwa riwaya ya Kiswahili kwa sas inaandikwa kwa kuangalia Nyanja zote za kimaisha.
Kwa ujumla riwaya ya Kiswahili nchini Tanzania imeendelea kwa kasi sana baada ya kugunduliwa kwa mashine za uchapishaji na kuwepo kwa taasisi mbalimbali za uchapishaji wa kazi hizo. Mbali na kuwepo kwa changamoto mbalimbali ,kwa waandishi kama vile kuyumba kiuchumi na kutumia maneno mengi ya lugha za kigeni, ili hali kazi zinaandikwa kwa watumiaji wa Kiswahili.


REJEA.
Kezilahabi E. (1988) Rosa mistika: Kenya literature Bureau
Mbogo E. (2002) watoto wa mama ntilie: Heko
Mung’ong’o C. G (1977) mirathi ya hatari: Tanzania Publishing house.
Robart S. (1957/58) kusadikika: Mkuki na nyota



Comments

Popular posts from this blog

Information technology

MKATABA WA KUPANGA NYUMBA

Unominishaji,