Dhana ya Mabadiliko


Dhana ya Mabadiliko, ni uwingi wa nomino Badiliko ambalo kwa mujibu wa TUKI (2004).Ni hali inayokuwepo baada ya kutokea  mageuzo fulani.ni hali ya kuwa na tabia tofauti na mwanzo.Kila kitu katika ulimwengu huwa kipo katika hali ya mabadiliko.
 Mabadiliko ya Maana,ni kubadilika kwa maana ya neno katika lugha  kutegemeana na muktadha na matumizi ya neno husika katika lugha fulani,lugha zote ulimwenguni hubadilika kutokana na wakati. Heiko Narrog (2012).
Kwa ujumla mabadiliko ya maana ni muundo wa mabadiliko ya lugha kutegemeana na maneno yanavyotumika katika lugha,pia hutegemeana na  muktadha na matumizi ya neno husika katika lugha.Mawazo ya Heiko Narrog (2012). Ya mabadiliko ya maana katika lugha ya Kiswahili yanajitokeza kama ifuatavyo;
 Heiko Narrog (2012). Anadai kuwa mabadiliko ya maana huenda sambambana na dhana ya polisemia, kuwa dhana ya Polisemia hutumika pale neno moja lina maana zaidi ya moja kimsingi katika uzungumzaji wa binadamu. Mwanadamu hulazimika kutafuta dhana zenye chimbuko moja au zinazohusiana kimaana akazipa neno moja tu liziwakilishe. Hivyo katika lugha tunapata neno moja tu likiwakilisha dhana kadhaa zilizo na uhusiano wa namna fulani. Pia unaweza kuchukua maneno ambayo hapo zamani yalikuwa yakiwakiliza dhana fulani yakaweza sasa kuwakilisha dhana mpya.
Mifano ya maneno; kichwa
                                Sehemu ya mwili
                                Dhana ya uongozi
                                Cha insha
 Anadai kuwa mabadiliko ya maana hujihusisha na upanuaji wa maana ya neno, Heiko Narrog (2012).anasema kuwa mabadiliko ya kisemantiki au ya maana huenda sambamba na  kupanua wigo wa mpana wa maana ya neno na kutumika katika nyanja mbalimbali ,mwanaisimu huyu alitoa mifano kutoka lugha mbalimbali kama vile kingereza ,kihindi na kigiriki.mfano katika lugha ya kingereza;
 Neno mbwa (dog) mala ya kwanza lilikuwa linatumika ni kama jina la mndege mwenye nguvu,baadae maana likabadilika na kutumika kwa ndege wote bila kujali nguvu hivyo ni kutokana na mabadiliko ya maana.katika lugha ya Kiswahili mawazo haya yanadhihilika kutokana na neno kama vile;
Shoga;kwa mala ya kwanza neno hili lilitumika kama rafiki wa kike kutokana na kupanuka kwa maana tunapata maana nyingine ambayo ni mwanaume anaejihusisha na mapenzi ya jinsia moja.
Anadai kuwa mabadiliko ya maana hujihusisha na ufupishaji wa maana ya neno, Haiko Narrog (2012).anasema kuwa mabadiliko ya kisemantiki au ya maana huenda sambamba na  kupunguza wigo wa mpana wa maana ya neno na kutumika katika kiwango kidogo ,mwanaisimu huyu alitoa mifano kutoka lugha mbalimbali kama vile kingereza na kigiriki.mfano katika lugha ya kingereza;
Neno; undertaker,kwa mala ya kwanza lilikua linatumika kama mtu mwenye nguvu nyingi sana kutokana na mabadiliko ya maana wamefupisha na kupata mazishi.(funeral).Pia katika lugha ya Kiswahili kuna msamiati ambao umefupishwa na kupata maana maana mpya mfano;
Discontinue ;kwa mala ya kwanza walitumia kama kutoendelea na masomo ya chuo kutokana na kushindwa ,lakini kutokana na mabadiliko huita Kudisko.
 Heiko Narrog (2012). Anadai kuwa mabadiliko ya maana hushughulika kubadili misamiati ya lugha inayohusika,,mwanaisimu huyu katika kitabu chake anasema kwamba suala la mabadiliko ya maana linahusu kubadili misamiati ya lugha husika kwani kila lugha ina misamiati mahususi ambapo inapofanyiwa mabadiliko misamiati hiyo hubadilika na kupata maana zingine katika neno hilohilo kwa mfano;
Kifaru;misamiati au maana zake ni,kifaa cha kivita, kipande cha mti ,mnyama.
 Mawazo ya Heiko Narrog (2012).  Anadai kuwa mabadiliko ya maana yana uhusiano mkubwa na maisha na utamaduni wa wanajamii,mwanaisimu huyu husisitiza kuwa ili mabadiliko ya maana yaweze kutokea ni lazima uwepo uhusiano na maisha mila na tamaduni ya lugha maalumu ambayo inatumika sehemu husika hivyo mabadiliko ya maana ya lugha ya Kiswahili hutegemeana na maisha na mila na desturi za watu wanaozungumza lugha hiyo na wanaotumia kingereza hutegemea maisha na mila na desturi za waingereza.
 Anadai kuwa mabadiliko ya maana hujihusisha na kuazima maneno kutoka lugha nyingine, uazimaji wa misamiati kutoka lugha nyingine hii ni njia mojawapo ya uundaji wa misamiati mipya katika lugha mbalimbali mwanaisimu huyu  anadai kuwa unaweza kuchukua maneno na kuyaingiza katika watumiaji wapya kwa maana mpya ya neno hilo pasipo kuzuwiliwa na kitu chochote , Heiko Narrog (2012).  Ametoa mfano kuwa kitenzi wasili (arrive) kutoka lugha ya kingereza kimeazimwa kutoka lugha ya kifaransa hivyo hata lugha ya Kiswahili hufanya mabadiliko ya maana kutoka lugha zingine mfano misamiati kama vile; ikulu,kimori,ng”atuka na kitivo.

Hivyo basi Heiko Narrog (2012).ametoa mchango mkubwa sana katika lugha  ya Kiswahili na zingine kwa ujumla kwani amefanikiwa kuonesha mabadiliko mbalimbali ya maana katika lugha ya kingereza na amejaribu kuangalia kwa upana kidogo lugha za kifaransa ,kihindi,na kigiriki hivyo kutokana na mawazo yake pia katika Kiswahili yametusaidia kwa mapana zaidi.
 Marejeo
Narrog, H.( 2012). Modality, Subjectivity, and Semantic Change. A Cross-Linguistic Perspective

TUKI(2004),Kamusi sanifu ya isimu na lugha. Chuo Kikuu Dar es salaam

Comments

Popular posts from this blog

International Law

KATIBA YA KIKUNDI