Jadili dhana ya neno huku ukitathimini utata uliopo katika kutoa tafsiri hizo ukirejelea mitazamo ya wataalam mbalimbali wa isimu.
UTANGULIZI
Habwe
na Karanja (2004) wamefafanua neno kama kipashio cha kiisimu chenye maana
kinachoundwa na mofimu moja au zaidi.
Katamba
(1994) anasema kuwa neno ni kipashio kidogo chenye maana katika lugha ambacho
kina dhima kisarufi . Neno linaweza kusimama peke yake na kuleta maana bila
kupachikwa vipande vingine.
Mfano
neno ‘childish (utoto) linaweza kutenganishwa na kubaki ‘child` (mtoto) na neno
hili linaweza likatumika kiupwekeupweke kwa sababu ni neno linalojitegemea
lakini hatuwezi kutenganisha kipande ‘-ish` (kama ilivyo katika Kiswahili) kikasimama
peke yake na kuleta maana.
Massamba
na wenzake (2003) wanabainisha kuwa neno linaweza kufafanuliwa katika misingi
ya kiumbo-sauti (yaani kuchunguza sauti zinazounda umbo zima) kiothografia
yaani herufi na kisarufi kile kinachowakilisha umbo husika.
Chomi
(2003) anaeleza kuwa neno ni mzizi tu au ni muundo wa mzizi pamoja na kiambishi
kimoja au zaidi.
Delahunty&Garvey
(2010) wanasema kuwa neno ni vipashio vigumu vinavyoundwa na vipashio kadhaa
vya msingi vinavyoitwa mofimu.
Ni
kweli kwa dhana ya neno ni tata katika
kuifasili utata huu unatokana na vigezo mbalimbali vya kisarufi ambavyo
wahisimu huvitumia kama muongozo wa kufasili dhana hii kama ifuatavyo; kigezo
cha kileksika
Kigezo
hiki hueleza kuwa neno ni kipashio cha kileksia chenye udhahania ambacho huweza
kudhihirika kimaana na kikazi kipashio hiki huweza kuwakilishwa kimaandishi au
kimatamshi kwa mfano; Mdee (2010) akimrejelea Crystal (1980) anaeleza kuwa leksimu ni kipashio
dhahania kinachowakilisha maumbo kadhaa yanayotokana nacho.
Mfano
Refu -ndefu
Mrefu -kirefu
Utata wa kigezo hiki
Hakiweki
bayana juu ya maumbo yatokanayo na leksimu moja kuwa ni maneno tofauti au neno
moja. Kuna maneno yenye umbo moja lakini huwa na maana tofauti, Je maneno hayo
yatakuwa ni neno moja au ni maneno tofauti?
Kwa
mfano Paa -sehemu ya juu ya nyumba –mnyama, enda juu au angani Panga -kifaa cha kukatia
kuni -kitendo cha kuweka vitu sawa
Kigezo cha kiothografia
Kigezo
hiki huchukulia neno kuwa ni maandishi yanayoacha nafasi mwishoni. Neno
hudhihirika katika maandishi tu na
lisiwe na nafasi katikati. kwa
mfano Rubanza (1996) anaeleza kwamba
neno kiothografia ni mfuatano wa maandishi ambao huacha nafasi tupu mwishoni
bila uwepo wa nafasi tupu katikati.
Mfano
katika sentesi; Baba analima shambani. Sentensi hii ina
maneno matatu yaliyopigiwa mstari. Pia maneno kama; mwana-chama, paka-shume huchukuliwa
kama maneno mawili tofauti Katika lugha ya kiingereza maneno kama ‘blackboard’ na
'cannot” yanachukuliwa kama neno moja
Utata wa kigezo hiki
Huchukulia
maneno ambatani kuwa ni maneno mawili tofauti kwa sababu huandikwa kwa kuacha
au kutenga nafasi katikati. Dai hili si kweli kwa sababu maneno ambatano
hurejea dhana moja hivyo hupaswa kuchukuliwa kama neno moja. Mfano Bata mzinga.
Pia
kigezo hiki kimejikita katika lugha ya maandishi tu na kutupilia mbali lugha ya
mazungumzo, kwani tunapoongeza nafasi tupu
huwa hazionekani. Hivyo tunajiuliza
maswali. Je neno ni lile linaloandikwa tu?
Kigezo cha kifonolojia
Kigezo
hiki huchukulia neno kama ni kipande cha lugha kinachotokana na kujengwa na
kipashio kidogo cha kimatamshi. Kutokana na kigezo hiki kuna vigezo fulani
vilivyowekwa ambavyo hutofautiana kutoka lugha moja kwenda lugha nyingine. Rubanza
(1996) anaeleza kuwa zipo lugha ambazo upo uwezekano wa kulitambua neno kwa
kutumia sifa za kimatamshi. Hasa zile lugha zenye kuweka mkazo mahali fulani
maalumu katika maneno wakati wote. Sehemu iyo inaweza kuwa mwanzoni mwa kila silabi
ya kwanza ya neno au silabi ya pili kutoka mwisho. Kwa mfano katika lugha ya kiingereza
“I
didn’t take the test yesterday”.
Sentensi
hii ina maneno matatu yaliokolezwa wino, kwa sababu mkazo huwekwa kwenye maneno
yenye kubeba maana.
Utaratibu
huu si mara zote kwa kuwa kuna wakati hata yale maneno yasiobeba maana
(grammatical words) hubeba mkazo kwa sababu ya msisitizo wa neno au maneno
katika sentensi.
Mfano:
katika sentensi ileile “I
didn’t take the test yesterday” ikiwa
mzungumzaji ataweka mkazo katika “I”atakua akionyesha msisitizo siyo
yeye,”didn’t” hakufanya,na “the” akimaanisha hakufanya jaribio hilo (lililokusudiwa
na muulizaji)
Katika
lugha ya Kiswahili mkazo huwekwa katika silabi ya pili kutoka mwisho.
Mfano:
anacheza, analima.
Kigezo
hiki kinasaulia kutofautisha maneno kwa kutumia mkazo,hususani katika lugha
ambazo mkazo hua na uamilifu wa kubadili kategoria ya neno.Mfano katika lugha
ya kingereza; ‘respect (nomino) respect (kitenzi).
Utata wa kigezo hiki
Kinashindwa
kuweka bayana neno hasa ni lipi,kwani tunaona kuna baadhi ya vipande-Lugha
visivyobeba maana ya msingi kama vile viunganishi na vihusishi katika lugha ya
Kiswahili ambavyo haviwekewi mkazo.Swali ni kwamba,je vipande lugha hivyo ni
maneno au si maneno?
Kigezo cha maana
Katika
kigezo hiki wanaisimu husisitiza maana katika kufasili dhana hii kwa kudai
kuwa neno lazima liwe na maana.Kwa mfano
Mdee (2010) anaeleza kwamba neno ni kipashio kidogo cha lugha chenye maana. Neno
lazima liwe na maana.
Mfano;
Baba
–mzazi wa kiume
Mama-mzazi
wa kike
Hivyo
kwa kutumia kigezo hiki, neno hutambuliwa kuwa ni kipashio cha kiisimu chenye
maana.
Utata wa kigezo hiki.
Kigezo
hiki hakibainishi kuwa ni maneno yapi hulengwa
hasa kwani kwa kiasi kikubwa kinaegemea sana katika maana ya kileksika
na kusahau mambo yenye maana kisarufi kama viunganishi na vihusishi.
Hakiweki
wazi juu ya maneno yenye maana ya mficho.
Kwa
mfano;Amepata jiko -Ameoa
Mkono wa birika -Mchoyo
Pia
maneno yenye maana zaidi ya moja. Kama vile; mbuzi, paa na kata
Maneno
haya yakisimama peke yake huwezi kupata maana moja hivyo lazima yawe katika
mahusiano na mengine katika sentensi ndipo upate maana.
Kigezo cha neno kama kipashio huru
kisichogawanyika
Bloomfield
(1993),anasema neno ni umbo dogo kabisa
lililo huru. Fasili hii ina mambo makuu mawili, kwanza neno liwe “umbo
dogo” pili “umbo huru”. Hapa umbo dogo
humaanisha umbo ambalo haliwezi kugawanyika bila kubadilisha maana yake.
Kwa
mfano; neno Paka-huwezi kuligawa katika “pa” na “ka” bila kupoteza maana yake. Hivyo
umbo dogo ni lile ambalo linashikilia maana.
Kwa
upande wa neno kuwa huru ina maana kwamba neno hilo lazima litamkwe peke yake
bila kutegemea au kuhambisha kwenye neno
lingine.
Mfano;
njoo, lete na jua.
Utata wa kigezo hiki
Neno
linalopewa uzito ni lile lililo katika lugha ya mazungumzo pekee. Katika lugha
ya maandishi tunaweza kuwa na vipande vidogo vya maneno lakini ambavyo vikiwa
huru hatuwezi kusema vina maana kwa kuwa huwa havirejelei kitu au hali yeyote ile.
Mfano
katika lugha ya Kiswahili vipande “kwa”, “cha” na “tu” havina maana vikiwa peke
yake bali hubeba maana vikiambatana na maneno mengine kama vile “kiatu cha
baba”.
Kigezo cha kisemantiki na
kiprogmatiki
Katamba
(1993) anasema ili neno litambulike lazima liwe katika muktadha wa matumizi. Neno
moja linaweza kuwa na dhima
mbalimbali na dhima hugundulika inapokua
ndani ya muktadha wa matumizi kwenye sentensi. Anatoa mfano wa neno la
kiingereza “cut” kwamba likiwa kiupweke upweke huwezi kutambua linarejelea
nini,pamoja na kwamba katika lugha ya kiingereza ni kitenzi “kata” lakini kuna
wakati linaweza kutumika kurejelea
nomino .
Mfano; “I
need my cut” na “I have cut my finger” katika mifano hii neno “cut” katika sentensi ya kwanza rejelea
nomino yaani “nahitaji stahiki yangu”. Katika sentensi inayofuata linarejelea
kitenzi yaani nimekata kidole changu. Neno la Kiswahili “chungwa” huwezi kutambua linarejelea nini. Hii
ina maana kuwa neno hili linaweza kutumika kama nomino au kitenzi.
Kigezo
hiki pia huenda mbali kwa kufafanua kuwa pia maneno kama ; na, tu, si katika Kiswahili na maneno, and, an, the, on katika kiingereza nayo
hayawezi hutambulika yanarejelea nini. Lazima
yawe katika muktadha wa matumizi ndio tunaweza kusema ni aina gani za maneno au
kutambua maana zake.
Utata wa kigezo hiki
Ni
kwamba si lazima maneno yote yawe katika muktadha wa matumizi ndipo tuweze
kubaini maana zake, kwani kuna baadhi ya maneno huweza kutambulika kuwa yana
maana gani hata yasipokua katika muktadha wa matumizi katika sentensi.
Kwa
mfano nomino za mahali kama vile; Dodoma, Mwanza na Morogoro na majina ya watu
kama vile; Amina, Omari, Fatuma na Ali. Swali
la kujiuliza kuwa aina hizi za nomino na nyingine nyingi ambazo ni kama hizi je si maneno? Tunaona pia kigezo hiki hakijajitosheleza
katika kutupatia maana ya “neno” itakayokidhi mahitaji ya taaluma zote
HITIMISHO Pamoja
na vigezo mbalimbali vilivotumika kufasili dhana ya neno kuonekana ndicho kiini
cha ugumu wa fasili ya neno, tofauti ya lugha nazo huchangia kufanya fasili ya
neno kuwa ngumu.
Hii
ni kwa sababu tabia ya lugha
hutofautiana kwani neno linaweza kuwa
neno katika lugha fulani lakini lisiwe neno katika lugha nyingine.
Pia
mitazamo tofauti tofauti ya wataalamu nayo ni sababu nyingine ya ugumu huo. Hivyo
ni muhimu kujifunza mofolojia kwa kuzingatia vigezo na mawazo ya wataalamu
tofautitofauti katika kuielewa dhana ya neno.
Katika
taaluma ya mofolojia neno linaweza kutumika utanzu wa isimu unaoshughulikia
muundo wa maneno. Kimsingi taaluma hii
hushughulikia muundo wa ndani wa neno ambao hujengwa na maumbo yaitwayo mofimu
ambayo hufanyiwa tafiti katika taaluma hii. Dhana hii husisitiza kuwa kitovu
cha uchunguzi wa kimofolojia ni neno. Hivyo
basi dhana ya neno huweza kuwa ni kipashio cha kiisimu chenye maana
kinaundwa na mofimu moja au zaidi
MAREJELEO
Habwe,
J. na Karanja, P. (2004) Misingi ya
Sarufi ya Kiswahili: Phonix Publishers Ltd. Nairobi.
Katamba,
F (1994) English Words Routledge:
London.
Massamba
D.P.B., Kihore, Y & Hokororo, L (2003) Sarufi
Maumbo ya Kiswahili Sanifu (SAMAKISA) Sekondari na Vyuo. Taasisi ya
Uchunguzi wa Kiswahili Chuo Kikuu cha Dar es salaam.
Chomi,
E.W. (2013) Kitangulizi cha Mofolojia ya Kiswahili Taasisi ya Taaluma
za Kiswahili Chuo Kikuu cha Dar es salaam.
Delahunty,
G.P& Garvey, J.J. (2010). The English
Language from Sound to Sense. Collins Colorado.
Comments
Post a Comment