Saruf


Saluhaya (2010). Anasema dhana ya sarufi ni kanuni, sheria na taratibu zinazotawala lugha katika matumizi yake ambayo hujumuisha matamshi, maumbo na maana
 Masamba  (2004 ) Sarufi ni taaluma ya lugha inayohusu uchunguzi na uchanganuzi  wa kanuni za vipengele mbalimbali vya lugha.
 Masamba na wenzake ( 1999 ).Sarufi ni kanuni na sheria au taratibu zinazo tawala kila moja katika viwango vine vya lugha yaani;Fonolojia (umbo sauti ) umbo neon ambayo huitwa  Mofolojia, Miundo maneno ( sintakisia ) na Umbo maana ambayo ni Semantiki.
 Sarufi ni taaluma ya lugha inayochunguza na kuchanganua vipashio na kanuni mbalimbali zinazo tawala  muundo wa lugha (Matinde 2012 ).
 Sarufi inaweza kuelezwa kama kanuni,sheria na taratibu zinazomwongoza mzungumzaji au mwandishi kuzungumza au kutunga tungo sahihi zinazoeleweka kwa msikilizaji wa lugha ileile.
 Kwaujumla sarufi inaweza kuelezwa kama kanuni, sheria na taratibu zinazo muongoza mzungumzaji au mwandishi kuzungumza au kuandika tungo au sentensi sahihi zinazoeleweka kwa msikilizaji wa lugha husika.Kama ni mzawa wa lugha, mtumiaji huwa tayari anazo kanuni hizo ( hata katika uzungumzaji), yaani kanuni anakuwa nazo akilini baada ya kusoma au kuishi na watu wanaozungumza lugha hiyo.
 Kwamujibu wa Masamba na wenzake (1999 ) wameeleza kuwa sarufi mapokeo ni sarufi elekezi ikisisitiza  usahihi wa lugha ikionyesha sheria ambazo hazina budi kufuatwa, mathalani kufanya muundo fulani wa sentensi usomeke kwa usahihi au sheria ambazo hazina budi kufuatwa ili kufanya matamshi Fulani yakubalike kuwa ndio sahihi.
 Sarufi mapokeo inaainisha aina tatu za sentensi kwa kuzingatia uamilifu wake ambao aina hizo ni , sentensi taarifa, sentensi ulizi na sentensi agizi. Mfano, sentensi taarifa; Baba ameondoka leo asubuhi, Sentensi ulizi; Nani amekula chakula changu?. Sentensi agizi;Lete hiyo kalamu!.  wakati sarufi ya kileo inaainisha aina nne za sentensi kwa kuzingatia muundo au umbo la sentensi hiyo, sentensi hizo ni sentensi sahili, mfano; James anacheka.  sentensi ambatano, mfano, wanachuo wa mwaka wa kwanza wanafagia viwanja huku wanachuo wa mwaka wa pili wanafyeka. sentensi changamani, mfano; Aliporudi nyumbani alitukuta tumelala. na sentensi shurutia mfano;Angekuja leo tungeondoka leo..
 Wanasarufi mapokeo wanasema kuna aina saba za maneno na wengine wanasema kuwa kuna aina kumi za maneno. Mfano; Habwe na Karanja (2004 ) wao wanaainisha aina kumi za maneno ambazo ni nomino, vitenzi, viwakilishi, vivumishi,vielezi, vihusishi, viunganishi, vionyeshi,vihisishi na vibainishi.Wakati wanasarufi wa kileo/muundo wao wanaainisha aina saba kama vile; nomino, viwakilishi, vihusishi, vitenzi, vielezi, viunganishi na vihisishi.
 Kwamujibu wa  Khamisi na Kiango ( 2002 ). Sarufi mapokeo ni sarufi ya kale, wataalamu wanaohusishwa na mkabala huu walijitokeza kuanzia karne ya tano kabla ya Kristo na katika karne ya 18 na 19 baada ya Kristo.Mfano; wataalamu hao ni Plato, Aristotle Panin na Plotagoras, wakati sarufi ya kileo imekuja baada ya sarufi mapokeo na wafuasi wa sarufi ya kileo na miongoni mwa wafuasi wa sarufi ya kileo ni Noam Chomsky.
Utofauti katika uchanganuzi wa sentensi. katika sarufi mapokeo sentensi huchanganuliwa katika kiima na kiarifu pia hutumia istilaihi chagizo badalaya kirai kielezi(KE), shamilisho badala ya kirai nomino(KN) na prediketa badala ya kirai kitennzi (KT). wakati sarufi za kileo huchanganuliwa sentensi katika kundi nomino na kundi kitenzi na pia hutumia istilahi za kawaida za virai. Mfano wa uchambuzi wa sentensi kama ifuatavyo
Mwalimu aliyefukuzwa jana shuleni amerudi kwao.

(a) Uchanganuzi wa kimuundo au kileo
S.Changamano
KN
KT
N
βV
T
E
Mwalimu
Aliyefukuzwa
jana
shuleni

Amerudi
Kwao
N
Ts
E1
E2
T
E

(b) Uchanganuzi wa kimapokeo.
S.changamano
K
A
N
βV
Pr
Ch
Mwalimu
aliyefukuzwa
Jana 
shuleni
Amerudi
Kwao
N
Ts
E1
E2
T
E

Utofauti katika lengo. katika sarufi mapokeo lengo lilikua ni kuelekeza watu jinsi ya kutumia lugha pia zilisisitiza kanuni na nini cha kusema na wajua lugha wakati katika sarufi za kileo lengo lao lilikuwa ni kufafanua vipengere vyote vya lugha fulani kama vilivyo na wanafafanua jinsi watu wanavyozungumza lugha na sio kuwaelekeza waizungumze vipi lugha yao.
Sarufi mapokeo ilikua baguzi kwani ilijikita zaidi katika lugha za kiulaya kama vile kiyunani na kilatini. Wakati sarufi za kileo/muundo zimejikita katika lugha zote zinazotumiwa na mwanadamu kama vile kiswahil,kinyakyusa, na kimakonde.
Sarufi mapokeo ilijikita zaidi katika taratibu na kanuni za uchanganuzi wa lugha kwa kuzingatia hasa lugha ya maandishi na kutozingatia lugha ya mazungumzo. Hivyo basi ni dhahili kwamba mkabala huu ulikua na mitazamo ya kifalsafa, kidi, nafasihi Habwe na Karaja (2004). wakati sarufi za kileo/ sarufi muundo yenyewe imejikita katika uchanganuzi wa lugha kwa kuzingatia kanuni na taratibu zinazo husisha aina zote mbili za lugha yaani lugha ya mazungumzo na lugha ya maandishi.
Hivyo basi mbali na kuwepo kwa utofauti kadha wa kadha baina ya sarufi za kimapokeo na za kileo pia hufanana katika nyanja mbalimbali kama vile mikabala hii miwili yote imekua ikijihusisha na kanuni, sheria pamoja na taratibu za uchanganuzi na uchambuzi wa lugha.

MAREJELEO.
Habwe, J. na Karanja, P. ( 2004 ). Misingi ya Sarufi ya Kiswahili. Nairobi. Phonex Publisher.
Habwe,J. na Karanja P. ( 2007 ). Misingi ya Sarufi ya  Kiswahili. Nairobi. Phonex Publisher.
Masamba na wenzake ( 1999 )  Sarufi Miundo ya Kiswahili Sanifu .( SAMIKISA ):Sekondari na
                                     Vyuo,Dar es Salaam.TUKI.
Matinde,R,S. (2012 ). Dafina ya Lugha,Isimu na Nadharia:Kwa Sekondari,Vyuo vya Kati na                                            Vyuo Vikuu. Mwanza: Serengeti Publishers.
Saluhaya (2010 ). Nadharia ya Lugha: Kidato cha Tano na Sita.Dar es Salaam. Children Education Society ( CHESO ). 

 .


Comments

Popular posts from this blog

International Law

KATIBA YA KIKUNDI