Kituo, kiishio au kibwagizo
Mashairi ya kisasa ni mashairi yasiyozingatia kanuni za kimapokeo, yaani, hayazingatii kanuni za muwala/urari (ulinganifu) wa mizani, vina, idadi ya mistari katika kila ubeti na kituo katika shairi. Mashairi haya pia huitwa mashairi huru / mashairi ghuni / mashairi ya kisasa / masivina /mapingiti
Muhimu ni kwamba wanausasa wamevunja kaida, kanuni,
sheria na mitindo ya uandishi wa ushairi wa kimapokeo. Hii haimaanishi kwamba
sheria zote zimetupiliwa mbali, bali mtindo mpya unaojitokeza katika uandishi
wa ushairi unafinyanga mbinu za awali na mpya na kutupa taswira mpya kabisa ya
ushairi. Kwa mfano mshairi aweza kutiririsha vina mahala popote katika ushairi,
Idadi yoyote ya mizani inaweza kutumiwa katika tungo tofauti. Kumejitokeza na
mashairi yenye michanganyiko mbalimbali ya maumbo, takriri, mizani maadamu
ufinyanzi tofauti. Mbali na haya utunzi wa ushairi wa kisasa unaegemezwa sana
kwenyematumizi ya lugha kama nyenzo muhimu ya kusanifu ushairi.
Ndipo sasa Mulokozi na Kahigi (1979: 25) ambao ni
wafuasi wa ushairi wa kisasa wanapendekeza fasili ifuatayo: Ushairi ni sanaa inayopambanuliwa kwa
mpangilio maalumu wa maneno fasaha yenye muwala, kwa lugha ya mkato, picha, au
sitiara, au ishara, katika usemi, maandishi, au mahadhi ya wimbo, ili kuelekeza
wazo au mawazo, kufunza au kueleza tukio au hisi fulani kuhusu maisha au
mazingira ya binadamu, kwa njia inayogusa moyo.
Mawazo haya yanatokana na fasili za washairi wa
kisasa kuhusiana na swala la je ushairi wa Kiswahili ni upi. Uteknolojia huu wa
kimchanganyiko ndio namna mwafaka kwao wa kuonyesha usanii, uhodari, ustadi na
ubingwa wa kiutunzi.
Ufuatao ni usasa unaojitokeza katika mashairi ya
kisasa hasa katika muundo wake
Idadi ya mistari/ mishororo katika kila ubeti,
Wanausasa kwa upande wao wakiongozwa na Euphrase
Kezilahabi wanasema kwamba shairi si lazima liwe na mistari mine katika kila
ubeti ndiyo liwe shairi kama wasemavyo wanamapokeo bali Shairi linaweza kuwa na
idadi yoyote ile ya mistari kutegemeana na nia na utaalamu wa mshairi katika
kutunga mashairi yake. Kwa mfano, katika shairi la "Mafuriko"
anasema:
"Nitaandika wimbo juu ya mbawa za inzi
Utoe muziki arukapo wa usikie walio wengi
Ushairi wa jalalani utaimbwa
Juu ya vidonda vya wakulima
Na usaha ulio jasho lao
Nitaandika juu ya mbawa za wadudu
wote warukao".
"Juu ya mistari ya pundamilia
na masikio makubwa ya tembo,
Juu ya kuta vyooni, maofisini, madarasani
Juu ya paa za nyumba na kuta za Ikulu!
Na juu ya khanga na tisheti
Nitaandika wimbo huu".
Katika shairi hili Euphrase Kezilahabi ametumia
mistari saba katika ubeti wa kwanza
na mistari sita katika ubeti wa pili.
Idadi ya vipande katika kila ubeti, mashairi ya
kisasa mengi huwa idadi kamili ya vipande yaweza kuwa kimoja, au hata vitatu
ambapo huwa ni kinyume na yale mashairi ya kimapokeo ambayo huwa na vipande
viwili.kwa mfano katika shairi la "mama angu" la Said Ahmed Mohammed
(2002: 24-27) ni moja ya shairi la kisasa ambalo lina kipande kimoja. Mfano
"Una siri mama’ngu!
Umezongwa kitandawili!
Yaendaje maisha yako?
Hata mimi sikuelewi".
(uk. 25)
Vipande
vitatu Mfano katika shairi la
"Moyo" lililopo katika Wamitila (2005) kwenye ubeti ufuatao:-
"Moyo waniambia ota, kuwa mwizi usiote, siwezi
kaini,
Moyo unaniambia kata, milija yote ikate, mizizini,
Moyo waniambia teta, penye dhuluma patete, andikoni,
Moyo waniambia woga, ndio mwanzo wa maafa"
Katika beti huu, kipande cha kwanza huitwa ukwapi,
kipande cha pili huitwa utao na kipande cha tatu huitwa mwandamizi.
Kituo,
kiishio au kibwagizo,
Kibwagizo ni yale maneno ambayo mtunzi wa ushairi
anayotumia kama kituo katika
ushairi wake.wana usasa hawandiki beti zao za
ushairi wao kwa kuziwekea kibwagizo
kinachofanana, bali kibwagizo kinakuwa ni tofauti
katika kila ubeti. Isitoshe; kila
kibwagizo ni kipande kimoja tu cha msitari si
vipande viwili kwa msitari kama ilivyo
kuwa wanamapokeo.Kwa mfano Euphrase Kezilahabi
katika shairi la "Dhifa" anaandika:
"Ni chakula cha mchana,
Walanchi wameshafika,
Wazungu, Wahindi, Waarabu
Washateka sehemu zao
Chakula ki mezani
Nidhifa".
"Mawaziri wenye kula,
Wabunge wapewa magari,
Waandishi waliosajiliwa,
Watangazaji wenye yale yale,
Wakereketwa wasokereka,
Kimya wamekaa", (uk. 27).
Hizi ni beti mbili za shairi moja lakini
zinatofautiana katika kibwagizo chake. Kila
ubeti una kibwagizo chake ambacho ni msitari mmoja
tu ama nusu msitari.
Ulali wa vina na mizani katika kila ubeti,
Euphrase Kezilahabi kwa upande wake haandiki ushairi
kwa kufuata urari wa vina
na mizani. Anaandika hivi kwa sababu anaeleza
kwamba, shairi si lazima liandikwe
kwa kuzingatia urari wa vina na mizani ndiyo liitwe
shairi. Mawazo haya yanaungwa
mkono na Mulokozi (1975) pale anaposema kwamba,
"ushairi wa Kiswahili
hautambuliki kwa vina na mizani bali utamaduni na
lugha yake". Katika kuthibitisha
mawazo haya Euphrase Kezilahabi ametunga mashairi
ambayo hayafuati urari na
vina na mizani. Kwa mfano: Katika shairi la
"Mafuriko" anasema:
"Mti mkongwe umelalia upande
Wa nyumba zetu hafifu
Upepo mkali uvumapo
hatulali
Kila kukicha twatazama
mizizi yake
Na mkao wake, na kuta
hafifu za nyumba
Lazima ukatwe kuanzia
matawi hadi shina
Mafuriko ya mwaka huu
yaashiria
Tutabaki kuwasimulia
wajukuu
Mwaka ule wa mafuriko
Miti mingi mikongwe
iliaanguka," (uk.4).
Shairi hili halina urari wa vina wala mizani na
wanusasa wanaliona hili kuwa ni
shairi na si vinginevyo.
Hitimisho, pamoja na usasa katika mashairi ya kisasa yamekusudiwa kuburudisha jamii, kuhamasisha jamii, kukuza sanaa na ukwasi wa lugha, kuliwaza, kuelimisha, kuonya, kutahadharisha, kusifia mtu au kitu na kukemea mambo yanayoenda kinyume na maadili ya jamii.
Marejeleo
Kahigi, Kulikoyela & Mugyabuso Mulokozi. (1973).
Mashairi ya Kisasa. Dar es Salaam:
Tanzania Publishing House.
Kahigi, Kulikoyela & Mugyabuso Mulokozi. (1979).
Kunga za Ushairi na Diwani Yetu. Dar es
Salaam: Tanzania Publishing House.
Mlokozi,M.M na Kahigi,K.K (1979), kunga za ushairi na diwani yetu,Tanzania publishing house; Dar es salaam
Comments
Post a Comment