Shaaban Robert

 

UTANGULIZI

Shaaban Robert alikuwa mwandishi mashuhuri wa kazi za fasihi ambazo ni Ushairi  na nathali. Alizaliwa tarehe 01-01-1909 huko vibambani kusini  mwa machui mkoani Tanga,Tanzania .Alifariki tarehe 22-06-1962 na akazikwa mwachui.ni miongoni  mwa watanzania waliokuza na kueneza lugha ya Kiswahili kupitia kazi zao za kifasihi. Alipata elimu ya dini ya kiislamu hukohuko mkoani Tanga mpaka alipohamia Dar es salaam wakati huo ikijulikana kama Mzizima.Alijiunga na kisomo cha darasani kuanzia mwaka 1922-1926 na akafaulu vizuri  katika masomo yake na kupewa shahada ya kuhitimu.

Kutokana na juhudi zake aliweza kuwa mwanachama wa kamati ya lugha ya Afrika Mashariki, bodi ya lugha Tanganyika, chama cha wanafasihi wa Afrika mashariki, pia mwanachama wa mamlaka ya jiji la Tanga,.katika maisha yake pia aliwahi kufanya kazi idara ya forodha Pangani, idara ya Wanyama ofisi ya Mkuu wa Jimbo Tanga na ofisi ya kupima nchi.

Kazi iliyompa jina ni kazi ya uandishi wa natharina ushairi,

Wamitila (2003:43), anaeleza kuwa falsafa ya mwandishi ni mawazo au wazo alilonalo juu ya kile anachokiamini  kuwa kina msingi unaotawala maisha. Tunapotaja falsafa tunarejelea  juu ya mawazo aliyonayo juu ya maisha ambayo yanajitokeza katika maandishi yake.

Sadipo (1973), anaeleza kuwa mawazo,fikra na udadisi kuhusu dhana na kanuni  zinazotusaidia kuongeza udhaifu kuhusu maadili,dini,maisha ya kisiasa,sheria, saikolojia, historian na sayansi na jamii.

Kwa ujumla tunaweza kueleza kuwa,  falsafa ni mawazo ya busara yenye kutawaliwa na misingi mahususi juu ya asili na maana ya ulimwengu na maisha ya mwanadamu. Ni msimamo wa msanii katika maisha juu ya utatuzi  wa matatizo katika jamii.

Kwa kutumia diwani mbili ambazo ni Mapenzi bora na Pambo la Lugha zilizoandikwa na Shaaban Robert. Falsafa ya mwandishi inajadiliwa kama ifuatavyo kwa kuanza na  diwani ya mapenzi bora;

Mapenzi bora ni utenzi ulioandikwa na Shaaban Robert mwaka 1958. Utenzi huu una beti 700 lengo lake ni kujadili jamii juu ya maana, sifa, faida na hasara za kukosa mapenzi bora. Mwandishi wa kitabu hiki anasema kusudi ni kuandalia mahitaji ya watu waliofikia fahamu ya kuwaza na kuhoji neno au kitu au tendo kwa akili ingawa haitakuwa vibaya kikisomwa na watu wowote ambao hawajafikia upeo kama huo wa kupenda kujiweka tayari kwa zamu yao pia kwa watu amabo wanadhani  kwamba mapenzi si kitu cha maana wanaonywa kuwa wanapata hasara kubwa kwa kupitwa na bila kujua uzuri wa fahari, heshima  na utukufu ambao hustahili wao wenyewe. Anawaandikia watu wanaodai kuwa mapenzi karaha kuzungumzwa anadai wanachekesha si kidogo mwisho anasisitiza kuwa mapenzi ni jambo moja kati ya mambo yaliyo muhimu katka wajibu wa mwanadamu. Falsafa ya Shaaban Robert katika diwani  ya mapenzi bora;

Mwandishi anaamini kuwa mapenzi bora yaani mapenzi ya kupendana wanajamii wote bila kujali tofauti zetu za rangi, dini, kabila na tofauti nyingine pamoja na kumpenda mwenyezi Mungu yataifanya dunia iwe mahali pazuri sana pakuishi na pia mwenyezi Mungu atatupatia thwawabu,

Mfano,

Mwandishi anasema katika ubeti wa 123

“Tupendane na wenyewe

 Tofauti tuondoe

 Amani itushukie

 Mapenzi tufanye ngazi”

Pia katika ubeti wa 467 anasema,

“Mapenzi pambo la moyo

 Ni furaha kuwa nayo

 Mapenzi hushinda cheo

 Hata pato la ghawazi”

Hivyo mapenzi ni kitu cha thamani kubwa na endapo tukiyapoteza tutaingiwa na gharama kubwa sana kuyarudish.

Kwa kutumia diwani nyingine ambayo ni pambo la lugha. Pambo la lugha ni miongoni mwa diwani iliyoandikwa na nguli wa fasihi za Kiswahili Shaaban Robert (1946), katika utangulizi wake anasema kuwa kitabu chaitwa Pambo la Lugha kwa vile ambavyo mashairi yasimulivyo habari zake kwa maneno ya vina au mlingano wa sauti ipendezayo masikio.

Diwani hii ina mashairi 43 yanayozungumzia kuhusu maisha, lugha na siasa.Katika diwani hii mwandishi anaamini kuhusu ukombozi wa mwanamke na kifo ni masula ambayo hatuwezi kuyaepuka kwa kuwa kifo kwa mwanadamu hakiwezi kukwepeka na suala la ukommbozi wa mwanamke ni suala muhimu katika jamii zetu. Falsafa ya Mwandishi katika diwani ya Pambo la Lugha mwandishi  anaamini Suala la Kifo na Ukombozi wa Mwanamke

Suala la kifo, Mwandishi hakusita kujadili suala la kifo kwani ni sehemu anayopitia kila mwanadamu katika maisha yake. Pia mwandishi hakusita kutumia ufundi wake kuongelea suala  kifo  katika shairi lake la “mauti” anasema

“Ugonjwa hutibika, mauti hayana dawa

 Kizima huharibika, kuja na kupotea

 Umbile likuweka, mauti yanaondoa

 Hili hufanyika pote, katika dunia” Uk 3

Katika shairi hili mwandishi anatilia mkazo kuwa kifo hakikwepeki mahali popote duniani na kuona kuwa kila nafsi itaonja mauti.

Ukombozi wa mwanamke, falsafa ya mwandishi juu ya ukombozi wa mwanamke imejitokeza sana katika ushairi. Yeye anamuona mwanamke ni kiumbe dhalili anayehitaji kusaidiwa kuthaminiwa na kuheshimiwa. Hali hiyo ya unyanyasaji wa mwanamke imekithili sana katika jamii nyingi ulimenguni, katika pambo la lugha mwaandishi anamtetea mwanamke anasema

“Mwanamke  anahaja, ya usawa wa hali

 Mke hazai kiloja, ila kwa mbegu dhalili”

HITIMISHO

Hivyo, Mwandishi Shaaban Robert katika diwani yake ya Mapenzi bora, ameweza kuonesha kuwa mapenzi ndio kila kitu katika maisha sababu kukiwa na mapenzi bora hakutokuwa na wizi, usaliti, vita, uongozi mbaya, rushwa. Hivyo mapenzi ni kitu muhimu katika maisha ya wanadamu. Pia katika diwani yake ya “pambo la lugha” falsafa yake kuu ni ukombozi dhidi ya ya mwanamke ambayo ni kweli kuwa mwanamke akikombolewa dunia nzima imekombolewa. Hivyo  ni muhimu kuachana na mila potofu za kumnyanyasa mwanamke.

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

MAREJEO

Gibbe, AG (1974).Shaaban Robert Mshairi,dar es S alaam, Taasisi ya uchunguzi

Wamitila K.W (2003).kichocheo cha fasihi, simulizi na andishi;Nairobi focus publication ltd

Samwel, M na wenzake (2013).Ushairi wa Kiswahili,mwongozo kwa walimu wa Kiswahili na diyani ya MEA, Dar es Salaam mevailli, publishers and method Samweli

Robert S, (1958).Mapenzi bora,Dar es Salaam;Mkuki na nyota publishers limited

Sadipo (1973).Woman and Afrikan society, france strabourg

Robert S, (1966).pambo la lugha,Nairobi;Oxford university press ,1966

Comments

Popular posts from this blog

Information technology

MKATABA WA KUPANGA NYUMBA

Unominishaji,