Utendi
wamitila (2003) Uk 333 ," Utendi; Ni shairi
refu la kisimulizi linalozungumzia kwa mapana na mtindo wa hali ya juu mateso
ya mashujaa au shujaa".
Mulokozi (1996) uk 85, " Utendi ; Ni utungo
mrefu wenye kusimulia matukio ya kishujaa kwenye jamii au taifa.
Utendi simulizi:
Ni utungo simulizi wenye mtindo wa kifomula unaohusu mambo ya ajabu ya
watu wasio wa kawaida (mashujaa) na masimulizi hayo husimuliwa kwa njia ya
mdomo. Ili hali, Utendi andishi; Ni ushairi wenye kusimulia matendo ya shujaa
au mashujaa kwa njia ya maandishi.
Hivyo basi, Utendi ni maktaba ya jadi ya historia ya
jamii fulani ambayo kupitia tendi mbalimbali jamii inatambua historia yake,
mashujaa wao pamoja na mila na desturi zao.
Na zifuatazo ni hoja zinazotofautisha kati ya utendi simulizi na utendi
andishi;
Utendaji_uwasilishaji;
Ni kitendo cha kuelezea mtu ama kitu namna kilivyo kwa kuonyesha sifa zake
. Hivyo basi utendaji_uwasilishaji ni
dhana inayoweza kututofautishia kati ya utendi simulizi na utendi andishi
ambapo;
Utendi simulizi huwasilishwa kwa njia ya kunenwa au kuimbwa na ala za muziki. Tendi
nyingi za Kiafrika hutumia mbinu mbalimbali katika uwasilishaji wake miongoni
mwa njia hizo ambapo utendi huweza kusimuliwa ni pamoja na njia ya ushairi au nudhumu yaani kuimbwa.
Mfano , Katita utendi wa Sara wa jamii ya Manika ameonyesha wimbo aliouimba Sara pamoja na
Kaka yake Yamuri Jabate, ambapo unajitokeza urudiaji rudiaji wa chorus. Mfano;
5. Chorus : Ah!
Sara is sung for those of one voice.
Dońt you see it?
Sira Mori: Sara! sara is sung for those with promises.
Dońt you see it?
Wakati utendi andishi utendaji au uwasilishaji wake
hufanyika kwa njia ya usomaji (kusomwa) bila kuwepo kwa ala za muziki ambapo mtu yeyote anayejua kusoma na kuandika huwa na ruhusa ya kusoma kitabu ama kazi hiyo. Mfano utendi wa Fumo
Liyongo .
Wahusika: Ni watu, wanyama au vitu vitumikavyo
katika kazi ya kisanaa ya kifasihi, ( Msokile 1999:32). Vile vile dhana ya wahusika ndiyo hutuwezesha kutambua
utofauti uliopo kati ya utendi simulizi na utendi andishi ambapo:
Utendi simulizi,
hutumia wahusika changamano ( wanyama, watu, mazimwi, miungu). Mfano katika
Utendi wa Rasi ÌGhuli msimulizi ametumia
wahusika mbali mbali walio binadamu na wasio binadamu ambao ndio wameijenga
na kuikamilisha hadithi nzima. Wahusika
hao ni kama vile ; wahusika binadamu
ambao wanaongozwa na Mtume Muhamadi na Masahaba wa wafuasi wa Kiislamu. Pia
kuna binadamu Makafiri wanaoongozwa na Rasi 'lGhuli. Vile vile wahusika wasio
binadamu ni kama vile Malaika, miungu na Ibilisi ambako wahusika hawa wamejitokeza katika Uk
13-19 katika ubeti wa 350-362.
mfano: ubeti wa 354.
“Kiswahili
jiburili
359. Akusalamu jalali
Kanituma nikujiye
Tuma mtu amwendee
Akamwambia Rasuli
Salamu nyingi kathiri
Na
maneno nikwambiye.
Sultani wa kufari
ubeti
wa 473." Ibilisi maluuni 475. Akangia sanamuni
Sikuzaa sikuzawa
Naumba nikiumbua
Achondoka iyo hini
Sultani kumghuni
Naua na kufufua
Ndimi wahidi Quhari
Wakati, utendi andishi hutumia wahusika wanadamu kuiumba kazi hiyo ya utendi andishi ili iweze
kufikisha ujumbe wake kwa hadhira ama jamii iliyokusudiwa. Mfano katika Utendi
wa Fumo Liyongo mwamdishi ametumia wahusika binadamu wengi miongoni mwao ni
pamoja na ; Sultani Daudi Mringwari ambaye aliyepanga kumuua Liyongo, Kijakazi
Saada aliyekua anampelekea Liyongo chakula gerezani pia muhusika Liyongo ambaye ndiye mhusika mkuu na mwanaume
mwenye nguvu ya uganga au sihiri. Hilo linajidhihirisha katika muujiza wa nguvu
zake zilizokuwa katika
kitovu chake, ambapo hapakuwa na kitu cha kumdhuru ila kudungwa sindano
ya shaba kitovuni. Yamejitokeza shairi
la Fumo Liyongo ubeti wa 143-144;
143. " Nisikiya
wangu baba
144. "Jamii silaha piya
Liniuwalo ni haba
Haziniuwi swabiya
Ni msumari wa shaba
Ila nimezokwambiya
Kitovuni nikitiya. Ni ya kweli
yote piya.
Uhifadhi: Ni kitendo cha kutunza kazi za kisanaa za
kifasihi ili zidumu kwa mdaa mrefu na ziweze kutumiwa na vizazi vingine. Hivyo
basi uhifadhi ni dhana inayotutofautishia kati ya utendi simulizi na utendi
andishi ambapo;
Utendi
simulizi huhifadhiwa kichwani. Kazi ya msanii hukaa kwenye ubongo wa msanii
naye huweza kuiwasilisha kazi hiyo wakati wowote, mahali popote na bila gharama
yeyote. Kazi ya utendi iliyohifadhiwa
kichwani ni hai kwasababu msanii anakuwa ana kwa ana na hadhira yake. Pia
kutokana na matumizi ya mbinu tofauti za kisanaa kama vile kucheza, kubadili
sauti, na hata miondoko ambapo mbinu hizo
huifanya kazi yake ipate uhalisia
zaidi mbele ya hadhira. Mfano katika Utendi wa Fumo Liyongo msanii ameonyesha
mbinu hizo kama vile "kucheza" ambapo watu walikusanyika kucheza
ngoma ya Gungu iliyopigwa kwa lengo la kumkamata Liyongo ili wamuue , vile vile
walicheza pale Liyongo alipoambiwa aombe ombi la mwisho ili auawe naye akaomba apigiwe
ngoma ya Mwao na Gungu ili wacheze wote. Haya yanajitokeza katika ubeti wa
80_81 pamoja na ubeti wa 112 na 117.
80. Sulutwani kabaini
81. "Kwa wanaume na wake
Ma-Shaha walo muini na Liyongo,
mumwalike
kawambiya kwa sirini
naazimu nimshike
"Pijana," gungu
hwambiya
ni siri nimewambiya.
112.Na
ngoma na nyingi kusi 117.
Wakiinuka kuteza
kusisalie unasi
Liyongo akatokeza
ikawa kama harusi khaufu zaliwakaza
watu wakiangaliya.
mbio zikawapoteya.
Wakati utendi
andishi huhifadhiwa kwenye maandishi ( Vitabuni)ambapo kazi ya msanii huwa
katika makala ama kitabu maalumu na kazi hii haipotezi fani na maudhu yake bali huendelea kuwa katika
asili yake ya awali hadi msanii atakapoamua kuibadilisha. Mfano utendi wa
Mwanakupona ambao unatoa mawaidha kwa msichana kuhusu unyumba na maisha kwa
ujumla katika jamii ya waswahili wa tabaka
la juu. Hivyo mbali na Mwanakupona Binti Mshamu
kuuandika utendi huu kwa mwanae Mwana Hashimu Binti Mataka kwa lengo la kumpa wosia kuhusu kumheshimu mmewe
katika ndoa ambapo alimwita mjinga katika ubeti wa 92
92 . Na sababu ya kutunga
Si shairi ni malenga
Nina kijana muinga
Napenda kumuusia.
Vilevile
aliandika kwa kuwataka vijana wengine wa kike wausome pia ili wawatii waume wao
katika ubeti wa 94 _95. Ambapo pia wanawake wengine wa Kenya waliupenda wosia
huo na wakaufanyia kazi na hata leo wanaendelea kufunzwa pale wanaposoma utendi huo.
94. Someni nyute huramu 95. Somani mite ya
nganu
maana muyafahamu
mutii waume zenu
musitukue laumu
musipatwe na zitunu
mbee za mola Jalia za
akhera na dunia.
Mazingira (mandhari) na wakati: Wamitila (2002),
" Mandhari ni ile arki au elementi ambayo hutufichilia wapi na lini
matukio yalifanyika . Anaongezea kusema kuwa, neno hili hutufichilia wakati na
sehemu matukio yalipotokea . Nafasi ya mandhari katika utendi huwa ni
uendelezwaji wa maudhui ya utungo. Hivyo basi mandhari na wakati
hututofautishia kati ya utendi simulizi na andishi ambapo;
Utendi simulizi hubadilika kulingana na wakati na
mazingira. Hii ni kwasababu hadithi iliyosimuliwa mwaka jana haiweze kufanan na
itakayosimuliwa mwaka huu kwani baadhi ya vitu hutoweka katika mazingila na
vingine huongezeka. Pia matukio katika
utendi simulizi huhadithiwa kwa kutaja mazingira halisi na penginepo mhusika
husimulia tukio hilo akiwa katika sehemu ile inayozungumziwa. Mfano katika
utendi wa Fumo Liyongo msanii
ametuonyesha mazingira yaliyotumika wakati wa matukio maalumu kama vile ;
Gerezani_ mahali ambapo Sultani Daudi Mringwari aliamuru Liyongo atiwe ili aje auwawe kwa kuhofia kuwa
atamnyang'anya madaraka kutokana na ushujaa aliokuwa nao Liyongo, mazingira
mengine ni Kisimani_ mahali ambapo Liyongo
alipiga goti na kutia mshale katika upinde huku kauelekeza mjini na
kukata roho , hii ilitokea mara baada ya mtoto wake kutumwa na Sultani akamwue
kwa kumchoma sindano ya shaba (Ubeti wa 181_182).
181. " Akapija ondo lake
182. Na hapo nami t'asema
katambika chembe chake
ni karibu ya kisima
kama hai ada yake
watu hawakusimama
chembe utani katiya.
kwa wut'e walikimbiya.
Wakati,
utendi andishi haubadiliki kulingana na wakati na mazingira kutokana na kuwa
katika kitabu au makala maalumu hivyo ni vigumu kabadilika mahali popote pale
watakapo usoma watasoma yale yale yaliyomo kitabuni na katika wakati wowote ule
labda hadi pale mwandishi atakapoamua kubadilisha mwenyewe na kuandika upya ile
sehemu aliyotaka kufanya marekebisho . Mfano katika utendi wa Mwana Kupona
Binti Mshamu Nabhnany ambapo inasemekana aliutunga utenzi huo akiwa
mgonjwa (inasemekana aliugua maradhi ya tumbo la uzazi). Alihisi kuwa
asingepona , hivyo akaamua kutunga utenzi ili uwe ni wosia kwa binti yake
ambaye angebaki bila ya uongozi wa mama( Ubeti wa 2 na 90_91). Hivyo basi
utenzi huo haujabafilika bado unasomwa hivo na watu mbali na kwamba wengine
hauwahusu ( wazazi wao sio wagonjwa).
2.
Maradhi yamenishika
hatta yametimua mwaka
sikupata kutamka
neno lema kukwambia.
90.
Ntungile utungo hunu 91. Ntungile
nili saqimu
kwa zehemu na zitunu moyo
usina fahamu
kwa qadha yako Dayyanu usomeni
Islamu
na hukumuzo Jalia.
mkiongozana ndia
Hitimisho:
Pamoja na kuwepo kwa tofauti kati ya
tendi hizi mbili ( utendi simulizi na utendi andishi) , tendi hizi ni muhimu kwa jamii kwan
hutuwezesha kujua mambo mbali mbali kutokana na majukumu yake kama vile ; kutoa wasifu wa shujaa mfano Shujaa Liyongo,
kukuza uzalendo kwa kuhimiza wengine kutoogopa kwa kuwaiga mashujaa, pia kukuza
vipaji vya utunzi wa kazi hizi hususani
kwa wanawake kwa kuiga mfano wa Mwanakupona Binti Mshamu.
MAREJEO.
Mulokozi, M.M.(1996). Fasihi ya kiswahili. Chuo
Kikuu Huria cha Tanzania : Dar es salaam.
Mulokozi, M.M.(Mh) (1999). Tenzi Tatu za kale. TUKI:
Dar es salaamu.
Msokile.(1999): Tafsiri ya dhana ya wahusika katika
kazi ya kifasihi ya kisanaa.
Wamitila .(2002): Tafsiri ya dhana ya
mandhari/mazingira na wakati katika kazi ya kifasihi ya
kisanaa.
Wamitila. (2003): Tafsiri ya dhana ya utendi.
Comments
Post a Comment