KAZI: Kutunga shairi lenye kichwa kiitwacho “Tatizo la ajira” lenye beti 20 zenye kipande kimoja katika bahari yoyote ile, kwa kuzingatia urari wa vina na mizani na kuonyesha madhara ya tatizo la ajira katika;
KAZI: Kutunga shairi lenye kichwa kiitwacho “Tatizo la
ajira” lenye beti 20 zenye kipande kimoja katika bahari yoyote ile, kwa
kuzingatia urari wa vina na mizani na kuonyesha madhara ya tatizo la ajira
katika;
a)Ugaidi
b)Wizi
c) Umalaya
TATIZO
LA AJIRA
- Jinamizi
meingia,
Latikisa na dunia,
Vijana walilia,
Ajira meenda wapi.
- Jamii
yajiuliza,
Kwa mliyotueleza,
Watu mkatuagiza,
Ajira meenda wapi.
- Ajira
tukililia,
Wote twaikimbilia,
Maisha twavumilia,
Ajira meenda wapi.
- Nilisoma
kwa bidii,
Nikose kazi vipii
Walimu niliwatii,
Ajira meenda wapi.
- Juhudi
tuliziweka,
Kusoma bila kuchoka,
Mazuri tukiyataka,
Ajira meenda wapi.
- Saluti
wahadhirii,
Nikapata digrii,
Vyeti vyangu vizurii,
Ajira meenda wapi.
- Nasi
tukajisomea,
Ajira kutegemea,
Sasa mnatugomea,
Ajira meenda wapi.
- Vijana
walalamika,
Hasa wanapokumbuka,
Kipindi wakihenyeka,
Ajira meenda wapi.
- Kwa wao
kujiari,
Maovu yanakithiri,
Tena yasiyo nasiri,
Ajira meenda wapi.
- Ubongo
unachemka,
Fikiri tulikotoka,
Vitabu vilisomeka,
Ajira meenda wapi.
- Kina dada
na wakaka,
Sasa mchaka mchaka,
Ajira kuadimika,
Ajira meenda wapi.
- Wasomi
shuka thamani,
Wadada uchochoroni,
Saka pesa kwa uhuni,
Ajira meenda wapi.
- Kijana yu
mtaani,
Mitaani makonani,
Viroba kukabeni,
Ajira meenda wapi.
- Wizi Kama
jeuri,
Imekuwa desturi,
Kwao ndo wataajiri,
Ajira meenda wapi.
- Wajua
tatizo nini,
Ajira kuwa gizani,
Jiuliza akilini,
Ajira meenda wapi.
- Tanzania ya
viwanda,
Wasomi kuranda randa,
Wengi wavuka Uganda,
Ajira meenda wapi.
- Lilikuwa
kimbilio,
Kwa wasomi pata vyeo,
Sasa imekuwa sio,
Ajira meenda wapi.
- Za kunja
Kama folio,
Kuwaza ajira leo,
Ajira si tazamio,
Ajira meenda wapi.
- Nimeuza
yangu mbuzi,
Nyumbani sina makazi,
Natembea bila kazi,
Ajira meenda wapi.
- Ajira mboni
ajiyo,
Ni nyenzo ukiwa nayo,
Popote ukiwa nayo,
Ajira meenda wapi.
Comments
Post a Comment