.Neno Kileksika.

 

2.Neno Kileksika.

Neno ni kipashio kidogo cha Lugha chenye maana. Kwa maana hiyo neno lazima liwe na sifa ya maana inayoeleweka kwa jamii inayotumia lugha hiyo.(Mdee,1977).

Mfano:Baba-Mzazi wa kiume.

 Kifaranga-Mtoto wa kuku.

Mama-Mzazi wa kike.

Ndama-Mtoto wa ngo'mbe.

Sifa hii inamashiko kwa sababu maneno mengi katika Lugha yana sifa ya kueleweka kwa watumiaji wake wa Lugha husika.

3.Kirai ni aina ya tungo ambayo inakuwa haina muundo wa kiima na kiarifu. Virai huundwa na viamba jengo.

Viambajengo ni kikundi cha maneno au hata neno moja pia inayofanya kazi kama kitu kimoja.kirai,kishazi au sentensi mkusanyiko wa viambajengo kadha.

Kirai ni mkusanyiko wa viambajengo kuzunguka neno kuu kwa mfano, KN huundwa na nomino na vivumishi vyake, kwahiyo muundo wa kirai ni maneno yanayokiunda yakiwakilishwa na alama za kategoria za maneno hayo.

a)Baba mdogo

Hiki ni kirai nomino( KN) kilichoundwa na nomino na kivumishi kwa hiyo KN=N +V.

b)anacheza mpira.

Hiki ni kirai kitenzi (KT)chenye kuundwa na Kitenzi (T)na kirai nomino.

4.Sintaksia ni kategoria mojawapo ya sarufi ambao huchunguza muundo na mpangilio unaokubalika wa vipashio katika kuijenga Lugha. Sintaksia hujihusisha na tungo neno,tungo kirai,tungo kishazi na tungo sentensi.

Ni kweeli kwamba wazungumzaji wa kiswahili hawawezi kukubaliana na tungo hii"Mno mzuri mtoto sana" Hii ni kutokana kwamba tungo hiyo haina kwanza mpangilio mzuri wa viambajengo vilivyotumika kuinda sentensi hiyo pia ni kutokana na ukweli kwamba sentesi nyingi za kiswahili huanza na nomino katika kiima tatu imetumia neno "mno" na "sana" yote yanadokeza dhana moja.

6.Sintaksia ni aina ya sarufi ambayo hujishughulisha na muundo wa vipashio jinsi ambayo vinaijenga Lugha.

Kilekiska hujishughulisha na maana ya maneno katika Lugha. Ufuatao ni udhaifu wa kisintaksia katika kuwepo kwa kategoria ya Kilekiska.

Katika ngeli ya kwanza umoja ina viambishi viwili(Yu/A)

Bado kuna ngeli za nomino zinazojirudia mfano ngeli ya 2,6 na 7 umoja zinatumia  "U"

Bado kuna nomino zenye kuleta migogoro katika ngeli mfano Makala,Jambazi,Marashi.

7.Ushahidi huu wa kisintaksia unaonyesha mtawanyo wa virai. Hii inamaana kwamba ukitaka kuhamisha maneno yaundayo virai,hauna budi kuhamisha kirai kizima na si sehemu tu kirai hichp,kudondosha au kuunganisha kirai kizima.

Mfano:Kaka yako mkubwa simpendi.

Simpendi kaka yako mkorofi.

Mkubwa simpendi kaka yako.

Mkorofi kaka yako simpendi.

Kuunganisha virai venye hadhi sawa.Mfano a)Baba analima

Mama analima.

Baba na mama analima.

a)Malambugi anasoma.

Kiti kimevunjika.

Malambugi na kiti kimevunjik/anasoma

Tungo hiyo haijaleta mana kwasababu hadhi siyo sawa pia katika ushahidi wa kisintaksia kuna jaribio LA ubadala kulingana na wanaisimu kama Andrew(2007).

Jaribio LA kiubadala hujihidhirisha pale baadhi ya maneno kuweza kusimama badala ya kirai kizima au kundi la maneno hususani katika kirai nomino na kirai kitenzi. Kwa hiyo sikweli kwamba hakuna kategoria ya virai katika uchanganuzi wa kisintaksia. Kuna kategoria ya virai ambayo imejikita katika neno kuu ambalo kuna aina mbalimbali za virai ambavyo ni kirai nomino,kirai kitenzi,kirai kielezi na kirai kihusishi.

 

 

 

Marejeleo.

Besha,R.M(2007).Utangulizi wa Lugha na Isimu.Dar es salaam:MacMillan Aidan Ltd.

Habwe,J&Karanja,P.(2007).Misingi ya Sarufi ya Kiswahili.Nairobi:Phoenix publishers.

Massamba,D.P.B na Wenzake .(2013).Fonolojia ya Kiswahili Sanifu.Dar as Salaam:TUKI.

Mdee,D.(2007).Nadharia za Leksikografia.Dar es Salaam: TUKI.

Matinde ,R.S.(2012).Dafina ya Lugha Isimu na Nadharia:Kwa Sekondari,Vyuo vya kati na vyuo vikuu.Mwanza:Serengeti Educational Publishers(T)Ltd.

 

 

Comments