Riwaya ya kiswahili

 

UTANGULIZI

Riwaya ya kiswahili ni ile ambayo inafungamana na utamaduni wa jamii ya kiswahili maana watunzi wengi wamekuwa wakiandaa kazi zao wakirejea utamaduni na Mila wanazozifuata au kuziamini (wamitila,2003).

Kanar,(2001) amesema kuwa usimulizi ni mtindo wa mpangilio unaotumiwa na waandisui wa hotuba,habari na utunzi wa kibunilizi kueleleza matukio.Anaendelea kufafanua kuwa unahusisha hadithi inayosimuliwa na msimulizi kulingana na mtaalamu huyu Kuna kaidu muhimu ambazo sharti msimuliaji azitilie maanani wakati wa kutoa masimulizi yake Kwan kuwa hadhira yake huzitarajia na huwa wanazisaka wanaposoma au kusikiliza kiss nazo ni kina Nani wanaohusika ni Nini kinatokea ni oini yanatokea na kwanini yanatokea.

Msimulizi ni wakala au nyenzo inayotumiwa na mtunzi kusimulia hadithi.kwahiyo Kila Hadithi in msimulizi ambaye anaweza kuwa mtunzi au mtu mwingine ambaye ameteua awe msimulizi.Hadithi inamfikia msomaji kupitia kwa msimulizi.msimulizihumpitisha msomaji au mskilizaji katika masafa ,maeneo,nyakati,na katika mawasiliano ya wahusika,hali na saikolojia zao.kwahyo msimulizi kupitia usimuliaji anajenga mkabala ambao unamwezesha msomaji au mtazamaji kuyatazama yanayotendeka na kuyasikia yanayosimuliwa(Msokile,1993).

Mtunzi wa Hadithi,ni mtu yeyote anayejishughulisha na utunzi au uandishi wa kazi za Hadithi mfano hekaya,Ngano,Tarihi,soga,Visa sili na nyinginezo.

Tunajibu swali let Kwa kutumia vitabu vya riwaya ya kiswahili ambazo ni MZIMU WA WATU WA KALE kilichoandikwa na M.S.Abdullah,KUSADIKIKA kilichoandikwa na Shabaan Robert na NGOMA YA MIANZI kilichoandikwa na mulokozi M.M. Hoja ya kwanza tumeanza na kitabu au riwaya ya "ngoma ya mianzi",hoja ya pili tumetumia"mzimu wa watu wa kale"na hoja ya mwisho tumetumia"kusadikika"kutetea hoja hii.

Ni kweli kwamba katika riwaya ya kiswahili anayedhaniwa kuwa ni msimulizi na msimulizi mwenyewe mara nyingi huchanganywa na mtunzi wa Hadithi kwa sababu zifuatazo.

Katika kujibu swali hili tunajikita katika kuangalia aina za usimuliaji wa riwaya ya kiswahili.

Mwandishi hujifanya ndiye msimulizi/msimuliaji, usimulizi huu hujikita au hutumia nafsi ya tatu pale mwandishi hutumia mtindo was insha kufafanua Jambo kwa jinsi atakavyo yeye na kuweka au kutumia ubunifu kujitenga na Hadithi mfano katika riwaya ya"Ngoma ya mianzi"katika riwaya hii mwandishi amejifanya kuwa ndiye msimulizi kwani hueleza wazo la mhusika mkuu Kama vile yeye ni muhusika.katika riwaya hii ya Ngoma ya mianzi mwandishi ndiye msimulizi/msimuliaji mfano katika (uk 1-3) mwandishi anasimulia jinsi muhusika chulu anaota ndoto ambayo ni ya hatari,anafanikiwa kukimbia yeye,mbuni na Bibi yake ili kujihami na hatari hiyo.kwahyo usimulizi huu mwandishi ndiye huchukua uhusika katika matukio yote kwa kutumia nafsi ya tatu.kwahiyo ni kweli msimulizi na msimulizi mwenyewe huchanganywa na mtunzi wa Hadithi.

Mmoja wa wahusika kuwa ndiye msimulizi, usimulizi huu huusisha nafsi ya tatu ambapo muhusika mkuu husimulia matukio yote katika Hadithi pia tunamjua wahusika wengine kupitia yeye.katika riwaya ya " mzimu wa watu wa kale"mhusika mkuu ambaye ni bwana Musa amekuwa msimulizi katika riwaya hii pia kupitia yeye tunapata kumjua mhusika Najum mfano (uk 13) bwana Musa anasema kumwambia Najum kuwa "bwana musa akaendelea kusema na tuseme anapanda mwilini na rohoni kwa wakati mmoja lakini kama mlivyosema binadamu ni kiwiliwili na roho pamoja.mimi naona kwahiyo shetani ni yeye mwenyewe binadamu, lakini wakati anapachagawa labda huwa amerukwa na roho hujua analosema wala analofanya. Hapa Najum alipata kipengee kidogo". Kwahiyo tunaona hapa bwana Musa ambaye ni muhusika mkuu huwa ni msimulizi ambaye anasimulia kiss hiki najum. Kwahiyo msimulizi na msimulizi mwenyewe huchanganywa na mtunzi wa hadithi.

Mwandishi na msimulizi wanakua kitu kimoja. Katika hoja hii mwandishi na msimulizi huwa kitu kimoja kwani mwandishi anakuwa karibu na msomaji lakini pia msomaji anakuwa karibu na mwandishi pia mwandishi au msimulizi anakuwa na uwezo wa kujipa jina lolote katika riwaya au hadithi ambayo huwa na sifa ya kitawasifu. Usimulizi huu hutumia nafsi ya Kwanza ambapo mwandishi au msimulizi hujisimulia yeye binafsi. Mfano katika riwaya ya "kusadikika" ya shabaan Robert. Mhusika karama ndiye ana sifa hii ya kitawasifu kwani anajisimulia yeye kama yeye.mfano wa ushahidi huu tunaupata katika (uk 11) ambapo karama anajaribu kujitetea mahakamani baada ya kufungwa na mfalme majivuno kwa kosa la kusambaza sheria kwa wananchi ili watambue haki zao. Mfano katika kitabu karama anasema "Ninazo sababu ya kusema.sababu ya Kwanza iliyotia azima katika moyo wangu ya kuanzisha uanasheria katika nchi hi labda itaelezeka vema Sana kama nikitaja mkasa wa wajumbe wa kaskazini ................................". Hi ni sifa ya kitawasifu ambayo hujaribu kuelezea maisha ya mtu binafsi kwa kutumia nafsi ya Kwanza.

Hitimisho,aina hizi za usimulizi Zina changamoto zake katika hadithi au riwaya.mfano msimulizi na mwandishi kuwa kitu kimoja, changamoto yake ni kuwa mwandishi au msimulizi husimulia Yale yaliyo mazuri tu kwa sababu yumo ndani ya .mmoja wa wahusika kuwa ndiye msimulizi wa hoja hii ni changamoto kwani msimuliaji lazima awe na ramani vinginevyo atapotea.

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

REFERENCES

Abdullah, M.S. (1971). Mzimu Wa watu Wa Kale. Dae es salaam: East African Liteture Bureau.

Msokile, M.  (1993). Kunga Za Fasihi na Lugha. Indian University: Educational Publishers and Distributors, Limited.

Mulokozi, M.M (2003). Ngoma Ya Mianzi. Dar es salaam: Tanzania Publishing House.

Shaaban, R. ( 1991). Kusadikika. Dar es salaam: Mkuki na Nyota Publisher.

Wamitila, K.(2003). Kamusi ya Fasihi. Nairobi, Kenya: focus Publication.

B

ADERICK MARCO

STE/BAED/164098

 

ALEX LEONARD

STE/BAED/164400

 

BARAKA G MALAMBUGI

STE/BAED/164158

 

GHANIMA S. PONGWA

STE/BAED/164192

 

HAPPYNESS CHARLES

STE/BAED/164005

 

LILIAN F. NGOWI

STE/BAED/164652

 

LUCY B MKONDYA

STE/BAED/164081

 

MICHEAL JOSEPH

STE/BAED/16437

 

NOELY G. NGONYANI

STE/BAED/164243

 

 

 

 

 

 

 

CHUO KIKUU KISHIRIKISHI CHA STELLA MARIS MTWARA

m16iogGbWPwXXcZAW903nm19OsmTWgEw9OZZAlWlFxMBgRcR-afV-fr6VYYl8X6hpAq1FduMX-nfkYzBPGyvQoeqIqDvYeW74xFch6wk=w228-h228-nc-3(Chuo Kishirikishi cha Chuo Kikuu cha Mtakatifu Agustino-Tanzania)

 

 

 

IDARA:                                                   KISWAHILI   

KITIVO:                                                 ELIMU NA SAYANSI

KOZI:                                                      USHAIRI WA KISWAHILI

MSIMBO WA KOZI:                             SW 312

AINA YA KAZI:                                    KAZI YA KUNDI

NAMBA YA KUNDI                              NAMBA 17

JINA LA MHADHIRI:                          MWL, CHITIMBE

Na

MAJINA

NAMBA ZA USAJILI

SAHIHI

1.       

s

 

2.       

 

3.       

 

4.       

 

5.       

 

6.       

 

7.       

 

8.       

 

9.       

 

10.   

 

Swali: Tunga shairi kutoka bahari yoyote ile lenye kichwa cha habari “KUMBE NI UZANDIKI” lenye beti 20 na kipande kimoja kwa kuzingatia urari wa vina na mizani.

 

 

Comments

Popular posts from this blog

International Law

KATIBA YA KIKUNDI