Riwaya

 

Wamitila (2002) na Senkoro (2011), wanasema Riwaya ni kisa mchangamano ambacho uweza kuchambuliwa, kwa mapana na marefu kifani na maudhui.Madumla (2009) Riwaya ni masimulizi marefu ya kubuni yalio katika mtindo wa kubuni ya kisawili mtindo maalumu na madhumuni maalumu.kwa ujumla ni masimulizi ya kubuni ya kinathari yenye msuko au mpangilio wa matukio au ploti unaofungamana na wakati au kisawili wakati na yenye visa vingi vinavyotendeka katika Riwaya fulani na yenye mawanda yenye mchangamano wa dhamira, visa na wahusika.Riwaya ya kiswahili ni ile inayofungamana na utamaduni wa waswahili katika lugha ya kiswahili ambayo inapatikana katika nchi ya Afrika Mashariki pia ni Riwaya inaowahusu waswahili wenyewe.Kusadikika ni Riwaya iliyoandikwa na mwandishi Shaaban Robertna kuchapishwa Mkuki wa nyota mwaka 1991.Ngoma ya mianzi imeandikwa na mwandishi M.m.Mulikozi na kuchapishwa na Tanzania pub.House in Dare s salaam mwaka 1991 Mzimu wa watu kale hii ni Riwaya iliyoandikwa na Muhammed Said Abdullah na kuchapishwa na East Africa literature Bureau Nairobi Dare s salaam Kampala mwaka 1960.

 Kwa kuzingatia swali linalosema "katika Riwaya ya kiswahili anayedhaniwa kuwa ni msimulizi na msimulizi mwenyewe mara nyingi huchanganywa na mtunzi".yafuatayo no maelezo yanayodhibitisha dai hili kwa kutumia vitabu mbalimbali Kama vile Kusadikika, Mzimu wa watu wa kale na Ngoma ya mianzi. Nikianza na Kusadikika naeleza kama ifuatavyo

Kwa kutumia Riwaya ya Kusadikika nikweli kwamba mwandishi ndio msimulizi wa Riwaya kuanzia ukurasa wa (1)mpaka ukurasa wa (10) mfano pale aliposema "wazili wa Kusadikika alikua mtu mwenye haiba kubwa na uhodari mwingi.uwaziri wake ulianza zaman sana .alikua waziri wa wafalme watatu katika nyakati mbalimbali"hivyo kupitia hayo maelezo inaonesha dhairi kuwa mwandishi ndio msimulizi lakini pia kupitia hii Riwaya mwandishi anoenekana kupotea na mhusika anakua ndio msimulizi wa Riwaya kwa mfano kuanzia (uk)11hadi wa 49 tunamuona mhusika Karama ndiye anakuwa msimulizi rejea pale anaposema ninazo sababu sita za kusema.ya kwanza iliyotia azima katika moyo wangu wa kuanzisha uanasheria katika nchi hii labda itaelezeka vema sana Kama nikitaja mkasa wa mjumbe wa kaskazini". Kupitia hayo malejeo na dhairi kuwa Karama ndie alikua ndio msimulizi wa Riwaya na usimulizi wake ulikoma baadae baada ya kutaka kutoa hukumu ndio mtunzi alionekana tena anasimulia kwa kumuonesha mfalme anatoa hukumu kwa kusema kuwa Karama atakua huru kwanibameshinda kesi.

Ni kweli kwamba msimulizi wa hadithi amechanganywa na mtunzi mfano katika Riwaya ya mzimu wa watu kale msimulizi wa hadithi amechanganywa na mtunzi pale nafsi ya kwanza na nafsi ya tatu katika usimulizi wake hii unadhihirisha pale kipwerere alipandwa na shetani na kueleza kwa lugha isiyofahamika na bwana musa.hivyo bwana Musa alisema tofauti yetu hasa labda ni hii kwamba wewe unadhani kwamba wanavyodhani watu wengine kwamba mtu akichagawa hujiwa na shetani au uoandwa na pepo alietoka bahari ya sabaau aridhi ya Saba yaani yule binadamu kwa wakati hule huwa kama kiti chake.vyema lakini kiti Cha shetanini binadamu na pia binadamu ana sehemu mbili kiwiliwili na roho. Sasa mtu akichagawa shetani hukaa wapi hasa mwili au rohoni mwake anaulizwa na najumu.najumu aliduwaa hakuwa na kusema. bwana Musa akaendelea kusema "natuseme anampanda mwilini na rohoni kwa wakati mmoja. lakini Kama nilivyosema binadamu ni kiwiliwili na roho pamoja.mimi aona kwa hiyo shetani ni yeye meenyewe binadamu labda wakati anapochanganywa labda huwa amerukwa roho hujua analosema Wala analofanya.hapa najumu alipata kipengele kidogo akaruka na kusema yaani yule Bibi alikua anasema maneno ovyo tu siyo? Bwana Musa alijibu Aaa! nimesema ameruka roho na roho ikiruka Najum hufika mbali hivyo kwa majibizano hayo kati ya bwana Musa na Najum hudhihirisha kuwa kuwa bwana Musa ni msimuliaji lakini muda mwingine huwa muhusika wa hadithi lakini pia mtunzi wa hadithi yenyewe kwa sababu Kuna muda anasimulia matukio kwa kutumia nafsi ya kwanza na muda mwingine anasimulia kwa nafsi ya pili.

Matumizi ya nafsi ya kwanza . Mwandishi ameonesha matumizi. ya kwanza katika kitabu cha ngoma ya mianzi  ambapo mtunzi na msimulizi wanaposema tulienda tukajificha tulipowaona hiii inadhihirisha uwepo wa nafsi ya kwanza pia katika Riwaya hii tunamuona mtunzi amesimulia yeye peke mwanzo adi mwisho wa riwaya.

Hivyo basi ni dhairi kwamba katika Riwaya ya kiswahili anayedhaniwa ni msimulizi na mwandishi wanachanganywa Kama ilivyoelezwa katika maelezo hapo juu na sio mara zote kwamba msimulizi na mtunzi wanachanganywa bali Kuna vitabu au riwaya msimulizi na mtunzi huchanganywa.

Comments

Popular posts from this blog

Information technology

MKATABA WA KUPANGA NYUMBA

Unominishaji,