Kategoria za kimuundo

 

Katika kazi hii kuna mgawanyo katika vipengele mbalimbali ikiwemo utangulizi ambao utajikita kutoa nini maana ya kategoria ya muundo ,pia kuna kiini cha swali ambacho kimefafanuliwa kwa kugusa kipengele cha  uhusiano uliopo baina ya kategoria za kimuundo za sarufi miundo ya Kiswahili ,mwisho  ni hitimisho la kazi husika.

     Kategoria za kimuundo ,kwa mujibu wa khamisi na Kiango (2002:9) dhana ya kategoria ilitumiwa na wanasarufi mapokeo kwa namna tofauti na inavyotumiwa na wanasarufi mamboleo . dhana ya kategoria kama ilivyotumika katika sarufi mapokeo ya akina Aristotle limetokana na neno la kigiriki na kutafsiliwa kama ualifu (predication) .wao walitumia dhana ya kategoria kuwa nis sifa bainifu zinazoambatana au zinazo ambikwa kwenye aina za maneno kama vile idadi, nafsi, kauli ,ngeli ,njeo na kadhalika.

Kategoria kwa mtazamo wa kisarufi mambo leo ni jamii, seti ,kundi au makundi yanayofanya kazi ya kufanana.aidha darajia yeyote ya vipashio inayotambuliwa katika uchambuzi wa lugha Fulani huitwa kategoria. Kwa sasa kategoria zipo katika viwango au darajia mbili, zifuatazo;

Kategoria za kikazi

Kategoria za kimuundo.

Kategoria za kimuundo,massamba na wenzake (2009) anaeleza kuwa kategoria za kimuundo ni darajia inayojihusisha na mpangilio wa maneno kstika sentensi na vipashio vyake kwa kua ngalia sharia na kanuni zinazotawala miundo ya Kiswahili.  Miongoni mwa kategoria za kimiundo ni muundo kirai , muundo kishazi na muundo sentensi.

 KIRAI, kwa mujibu wa massamba na wenzake (2009) anasema kirai ni kipashio cha kimuundo chenye neno moja au zaidi lakini hakina muundo wa kiima na kiarifu.

Matei (2008) anafasili kirai kama fungu la maneno ambalo hufanya kazi kama neno moja .kilai hudokeza maana lakini maana hiyo si kamili na hakina muundo wa kiima na kiarifu.

Kutokana na wataalamu hawa tunmabaini kua kirai kinaweza kuwa sehemu ya kiima au kiarifuhivyo tunaweza kuhitimisha kwa kufasili kirai kama ni kipashio cha kimuundo kinachoanzia neno moja na kuendelea ambacho hakina muundo wakiima na kiarifu.

 KISHAZI ,kwa mujibu wa massamba na wenzake (2001) wanasema kishazi ni tungo ndogo yenye uoanifu ndani yake .ambayo ni kubwa kuliko neno lakini iliyo sehemu ya sentensi kubwa.                    

Matinde (2012)anafasili dahana ya kashazi kuwa ni neno au kifungu cha maneno chenye kiima na kiarifu au kiarifu pekeyake ambacho ni sehemu ya sentensi kuu.

Matei (2008) anafasili kuwa  kishazi ni kundi la maneno lenye kiima kimoja na kialifu kimoja .

 Kwa ujumla tunaweza kusema kuwa kishazi nitungo ambayo ina kiima na kiarifu na inaweza kusimama pekee na kukamilisha maana au inaweza isisimame yenyewe na kukamilisha maana.

Wahiga (1990) anasema sentensi ni tungo iliyo kamili kisarufi ambayo inajitegemea kimaana. Kwahiyo kutokana na fasili hiyo tunaweza kusema kwamba ,sentensi ni tungo kubwa yenye muundo wa kiima na kiarifu inayojitosheleza kimaana.

 

Baadhi ya hoja zinazoonesha uhusiano wa kategoria za kimuundo za sarufi miundo ya Kiswahili ni kama zifuatazo;

       Hukamilishana kimuundo,taaluma ya sarufi miundo huzingatia uhusiano uliopo wa kategoria za kimuundo ili kujenga tungo yenye mantiki au mtiririko mzuri wa kimawazo mfano, “baba analima”  tungo hii imeundwa na kategoria mbili za  yaani kategoria ya kirai nomino “baba” na kategoria ya kishazi  kitenzi “analima”. 

        Pia kategoria za kimuundo hukamilishana kimaana, uhusiano mkubwa katika sarufi miundo ya Kiswahili  huzingatia sana swala la uhusiano wa maneno yaliopo katika tungop na namna yanavyo poangiliwa kwa kuzingatia sharia na kanuni za lugha husika mfano,  wanafunzi wanasoma     tungo hii imekamilika kimaana kutokana na mpangilio mzuri wa maneno kimuundo yaani wanafunzi ni kirai na wanasoma ni kirai kitenzi au tunaweza kuita kishazi kwa ujumla .kwa kawaida tungo ya Kiswahili katika uundaji wake wa tungo wenye maana kama hioyo huzingatia huizingatria uhusiano wa kategoria za kimuundo.

         Uhusiano wa kategoria za kimuundo pia huzingatia uhusiano wa kisarufi, kwa kawaida kategoria za kimuundo za sarufi miundo ya Kiswahili  huzingatia zaidi upatanisho wa kisarufi  uliopo kati ya nomino  na kiambishi awali cha kitenzi,mfano

                     Motto anakula chakula.”   Katika tungo hiyo nomino inahusiana moja kwa moja na kiambishi awali cha kitenzi ankula  hivyo endapo kiambishi cha kitenzi kitabadilika kitapoteza uhusiano baina yake  kati ya nomino na kitenzi.Mfano , Mtoto  wanakula chakula. Tungo hiyo haina kabisa upatanisho wa kisarufi ,hivyo basin i wazi kusema kwamba sarufi miundo ya Kiswahili huundwa kwa kjuzingatia uhusiano wa kategoria za kisarufi miundo.

        Hukamilishana katika uhundaji wa tungo zenye mantiki, neno mantiki ni neno lenye maana ya mtiririko na mpoangilio  katika kuunda tungo yenye maana inayojitosheleza.hivyo uhusiano wa kategoria za sarufi miundo ya Kiswahili ni pamoja na kuwezesahna katika kuandaa tungo zenye mantiki  , mfano   mwalimu atasafili kesho asubuhi”  katika tungo hii upo mtiriliko mzuri unaokamilisha tungo kimantiki. Lakini pia tungo hii inaweza kukosa mantiki endapo mpangilio wa kategoria za kimuundo hazitawekwa katika mpangilio mzuri au kuto kuwepo kabisa .mfano “mwalimu atasafili” bado kuna kuwa na maswali mengi ya kimantiki miongoni m,wa wasomaji kama muda atakaosafili , na kadharika.

 

 

Kwa ujumla sintaksia taaluma ya sintaksia ni taalauma ya sarufi ambayo ndio msingi wa taaluma ya juu kabisa ya sarufi ambayo ni semantiki kwani semantiki ambayo huchunguza maana ya maneno katika tungo ,maana hizo haziwezi kuwa na mantiki endapo uchambuzi wa kina wa miundo wa maneno hautazingatiwa katika taaluma ya sintaksia.

 

Comments

Popular posts from this blog

International Law

KATIBA YA KIKUNDI