Mofimu

 

UTANGULIZI.

Mofimu

Kihore (2017), akimnukuu Kamusi San if u ya Isimu na Lugha (1990). Mofimu ni kipashio kidogo amilifu katika maumbo ya maneno. Kipashio kidogo kina maana ya umbo la neno au umbo katika neno ambalo haliwezi kugawika katika sehemu nyingine ndogo zaidi. Mfano mtu ni kipashio kidogo kabisa katika neno mtu ni 'm'.

Aidha kipashio kuwa amilifu maana yake ni kwamba kina kazi maalumu kisarufi kazi hizo zinaweza kuwa kubeba maana ya msingi katika neno au kiambishi kinachowakilisha dhana au kipashio cha kisarufi kwa mfano mtoto, 'M' ni mofimu yenye kazi ya kwanza kuonesha umoja, pili kubainisha kundi la nomino ambamo nomino hiyo imo wakati kipashio toto ni mofimu inayobeba maana ya msingi.

ALOMOFU.

Matinde, 2012. Alomofu ni maumbo mawili au zaidi yanayowakilisha mofimu moja na hutokea katika mazingira maalumu ya utokeaji. Kwa mfano mti, mchawi, mtoto, hizo ni alomofu, pia mwana, mwenge, mwangaza, muuguzi, muungano, muumba, hiyo ma, mwa na mu ni Alomofu zinazowakilisha mofimu kiambishi Mu katika mazingira tofauti ( Kihore, 2007).

MOFU.

Matinde, 2012, akimnukuu TUKI, 1990. Wanasema mofu ni kipashio cha isimu maumbo kiwakilishacho mofimu. Hivyo basi mofu ni kipashio cha kimuumbo au umbo ambalo huwakilisha mofimu, huweza kuandikwa au hata kuandikwa na linalitumiwa kuwakilisha maana fulani katika neno. Mofu ndio umbo ambalo hubeba mofimu. Mofu hubainishwa vizuri kwa kuzingatia maumbo ya maneno ya ndani badala ya maumbo ya nje. Hii kwa sababu maumbo ya nje yanaweza kuathiriwa na mifanyiko ya kifonolojia na kimofolojia ambayo inaweza kudondoa, kuchopeka au hata kuunganisha viambishi katika neno. Mofu huwakilishwa na ishara ya mabano {  }. Mfano

          Neno                  Mofu

           Mtu                   { m },  { tu }

           Analima            { a } { na } {lim } { a }.

Ubainisho wa mofimu katika lugha umetegemezwa katika dhana kwamba umbo la neno huweza kugawanyika katika vipande ( Kihore, 2007).

Seti, ni kundi la vifaa au vitu vya aina moja vinavyohusiana katika kukamilisha shughuli ( TUKI, 2014). Hivyo basi mofimu zilizosetiliwa katika mofu au alomofu ni kwamba kundi la vipashio vidogo amilifu katika maumbo ya maneno. Kimsingi kundi hilo la mofimu ( mofimu zilizosetiliwa ) huwa na uamilifu fulani katika maneno.

Kwakua, mofimu huweza kusetiliwa katika maumbo ya maumbo ya maneno hivyo pia huweza kugawika ( Kihore, 2007 ) anadai kuwa ubainisho wa mofimu katika lugha umetengenezwa katika dhana kwamba umbo la neno huweza kugawanyika katika vipande. Kwa kuzingatia maelezo hayo ya Kihore hivyo basi tunaweza kubaini mofimu zilizosetiwa katika mofu au alomofu za maneno kwa kugawanya maneno hayo katika vipashio vidogo zaidi vya kiuamilifu katika neno kama inavyojidhihirisha katika maneno yafuatayo:

( a) Mkono =  m- kono

Hili neno ni nomino

Hili neno lina mofimu mbili  m- kono

M - imetumika kuonyesha umoja

     - kubainisha kundi la nomino ambayo nomino hiyo imo. Nomino hii ipo kwenye kundi la  

       nomino U - I mfano Mkono umevunjika - mikono imevunjika.

Kono - hubeba maana ya msingi.

( b ) Ujana =  U - Jana

         Ujana - ni nomino dhahania kwa maana hufikirika tu hauwezi kushikika.

         Neno hili lina mofimu mbili   U - jana

       U - Ni mofimu tegemezi ambayo imesetiliwa katika mofu jina na kubadilisha kategoria ya neno kutoka kielezi cha wakati na kuwa nomino dhahania.

      Jana - maana ya msingi.

( c ) Uzeeni = u- zee - ni

           Ni kielelezo cha hali

           U - ni mofu inayoonesha hali ya kuzeeka

               - imetumika kubadilisha kundi la nomino ambayo nomino hiyo imo. Nomino hii ipo katika kundi la  U - U ( Matinde, 2012 ).

            Zee = hubeba maana ya msingi

            ni = mofu inayobadilisha neno kuwa kielezi.

(d ) Wachezaji = wa - chez - a - ji

              Ni nomino

   Wa - hudokeza nafsi ya tatu wingi yaani wao

   Chez - ni mzizi wa neno

     a - ni mofu tamati kijenzi cha shina

      ji - ni mofu tamati kijenzi cha maana

         - ni kiambishi cha nomino. Mofu tamati 'ji' huingiza dhana kama vile kurudiwarudiwa kwa tendo ( Kihore, 2007 ).

( e ) Anatupenda = a - na - tu - pend - a

          Ni kitenzi

            a - ni mofu ambayo hudokeza nafsi ya tatu umoja

            na - ni mofimu ambayo hudokeza njeo au wakati ( wakati uliopo endelevu )

             tu - ni mofimu ambayo hudokeza urejeshi wa mtenda yaani anayetupenda sisi

              pend - ni mzizi wa neno anatupenda

               a - mofimu tamati maana

( f ) Ogofya = ogo - fy - a

           Neno hili ni tendo au kitenzi

            Ogo - ni mofimu ambayo hubeba maana ya msingi

             fy - ni mofimu kiambishi cha utendeshi

              a - kiambishi tamati maana

( g ) Levya = le - vy - a

          Neno hili ni kitenzi

          le - mzizi wa neno

          vy - ni mofimu kiambishi ambayo hubeba dhana ya utendeshi

           a - ni mofimu kiambishi tamati

( h ) Vitabu = vi - tabu

             Ni nomino

              Vi - mofimu kiambishi cha wingi

                - hubainisha kundi la nomino ambalo nomino vitabu imo ( KI - VI )

                tabu - ni mofu ambayo hudokeza maana ya msingi ya neno

 

 

  

    HITIMISHO

Hivyo basi maneno haya yamesetiliwa kwa kuzingatia mofu na alomofu kwa kuzingatia uamilifu au kazi ya kila neno na kuligawanya neno katika vipande kuanzia kipashio kikubwa mpaka kipashio kidogo kabisa cha neno.

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

MAREJEREO.

Kihore, M. na Wenzake (2007). Sarufi\ Maumbo ya Kiswahili Sanifu ( SAMAKISA ) Sekondari na Vyuo. Dar es salaam: TUKI

Matinde, R. S. ( 2012 ). Dafina ya Lugha, Isimu na Nadharia: Kwa Sekondari, Vyuo vya Kati na             Vyuo Vikuu. Mwanza: Serengeti Educational Publishers ( T ) Ltd.

TUKI ( 2014 ). Kamusi ya Kiswahili Sanifu. Oxford University Press.

Comments

Popular posts from this blog

International Law

KATIBA YA KIKUNDI