. Semantiki

 

Kazi hii imegawanyika katika sehemu kuu tatu, sehemu ya kwanza ni utangulizi, sehemu ya pili ni kiini cha kazi na sehemu ya tatu ni hitimisho la kazi kwa ujumla.

Massamba (2004:75) anafasili dhana ya semantiki kuwa ni taaluma ya isimu inayojishughulisha na uchunguzi na uchambuzi wa maana za maneno na tungo katika lugha. Semantiki imegawanyika katika makundi manne ambayo ni leksika, mantiki, muundo na nadharia.

hata hivyo hakuna ufafanuzi wa kutosha kuhusu maana ingawa katika hali ya kawaida tunaishia kutoa sifa za kitu na siyo maana.

Kwa mujibu wa Crystal, D (1987) semantiki ni utanzu wa isimu unaochunguza maana katika lugha. Kwa mukhtasari, semantiki hutalii maana katika vipashio vyote vya kiisimu katika viwango vyote vya lugha mathalan fonolojia, mofolojia na sintakisia.

Aidha, semantiki inaweza kufasiliwa kwa namna mbalimbali jinsi ifuatavyo:

Maana anuwai za dhana ya semantiki

1.       Semantiki ni stadi ya maana

2.       Semantiki ni utanzu wa isimu unaongalia maana ya maana.

Semantiki ni taaluma katika isimu ambayo hushughulikia maana ya maumbo au sentensi katika lugha. Taaluma hii ilianza enzi za Aristotle na Plato ambao walizingatia zaidi sifa za maana, katika kipindi hicho walitaka kujua sifa na tabia za maana. Leech (1981).

 

Habwe na Karanja wakimnukuu Richard na Wenzake (1985) wanasema “Semantiki ni stadi ya maana. Semantiki ni utanzu unaochunguza maana katika lugha ya mwandamu”. Wanaendelea kusema semantiki hutafiti maana za fonimu, mofimu, maneno na tungo. Hivyo kutokana na fasili hii maana hushughulikiwa katika vitengo au viwango vyote vya lugha ambavyo ni fonolojia, mofolojia na sintaksia.

Hivyo kutokana na maana zilizotolewa na wataalamu mbali mbali happy juu wanakundi tumetoa maana ya semantiki kuwa,

Semantiki.ni utanzu wa isimu ambao unajishugulisha na uchunguzi,uchambuzi na kutafiti maana za lugha ya binadamu kutoka kiwango Cha neno mpaka kiwango Cha tungo.

 

Hivyo  kwa ujumla  Semantiki ni taaluma katika isimu ambayo hushughulikia maana ya maumbo au sentensi katika lugha. Taaluma hii ilianza enzi za Aristotle na Plato ambao walizingatia zaidi sifa za maana, katika kipindi hicho walitaka kujua sifa na tabia za maana. Hii inamaanisha kwamba semantiki hutalii maana katika vipashio vyote vya kiisimu katika  viwango vyote vya lugha yaani fonolojia, mofolojia na sintakisia.

Kwa sababu hii ni sawa kusema kuwa maana hujishugulikiwa katika tanzu za isimu Kama fonolojia ,mofolojia,na sintaksia .semantiki inakuwa ndio makutano ya taaluma nyingine

 

Semantiki kama taaluma nyingine ina mahusiano na taauma nyingine kama ifuatavyo katika mchoro na hatimaye katika maelezo yanayo eleza vipengele mbalimbali vya lugha:-

Mchoro kuonesha  mahusiano ya semantiki na vipengele vingine vya lugha kama sintaksia,mofolojia na fonolojia.Kuwepo kwa semantiki katikati inamaana kwamba tawi hili ni muhimili wa matawi mengine.

 

Oval: Mofolojia
Isosceles Triangle: Semantiki
 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 


  Fonolojia ni tawi la isimu ambalo hujishughulisha na uchunguzi na uchambuzi wa mfumo wa sauti katika lugha, huchunguza jinsi ambayo vitamkwa au sauti za lugha zinavyoungana ili kujenga maneno yanayokubalika katika lugha ya mawasiliano. Ili lugha ya mawasiliano iwe kamili ni dhahiri kwamba mpangilio wa sauti lazima uwe na maana ili kufikisha ujumbe, hivyo semantiki inauhusiano mkubwa na fonolojia.

Mfano: Neno “UA” linamaanisha sehemu ya mmea  maalumu kwa kutoa mbegu na kuvutia wadudu kwa ajili ya uchavushaji lakini ikibadiliswa vitamkwa na kuwa ‘au’ huleta maana tofauti na maana ya  awali.

  Mofolojia ni taaluma inayoshughulikia vipashio vya lugha katika kuunda maneno. Tawi hili la isimu huchunguzi na kuchambuzi wa maumbo ya maneno na jinsi maumbo hayo yanavyotumika katika lugha. Jukumu la neno husika katika sentensi hubainika vyema kulingana na uhusiano baina ya maneno mengine katika tungo. Maumbo ya kimofolojia huathiri vipengele vingine vya kisemantiki. Hivyo semantiki ina mahusiano na taaluma ya mofolojia kwa kuwa ili lugha iweze kueleweka lazima iwe na mpangilio na muundo mzuri wa vipashio vya sentensi ili kuleta maana katika mawasiliano.

Mfano:     Mwalimu anaimba

                     Walimu wanaimba

Katika mfano huu katika upande wa kiima kiambishi m kinaashiria  umoja na wa  inaashiri wingi,  katika upande wa kiarifu viambishi a katika upande wa kiima vinaashiria nafsi ya tatu umoja na wa vinaashiria nafsi ya tatu wingi, hivyo maumbo ya maneno lazima yawe na maana.

 

  Sintaksia, ni utanzu wa sarufi unaojihusisha na uchunguzi wa mpangilio wa maneno katika sentensi na uhusiano wa vipasho vyake. Utanzu huu huchunguza sheria  au kanuni zinazofuatwa katika kuyapanga maneno ili yalete maana inayokubalika na kueleweka katika lugha husika, . Kwa mantiki hii, kwa kuwa semantiki hushughulikia viwango vyote vya lugha, basi hushughulikia pia kiwango cha sintaksia ambapo huangalia maana za tungo, kwani tungo lazima ikubalike kwa wazungumzaji pia tungo lazima ilete maana.   

         Kwa mfano,

Pana huimba vizuri akiwa mubashara

Mubashara huimba vizuri akiwa pana.

Vizuri huimba pana akiwa mubashara.

Katika mifano hii sentensi (1) inampangilio sahihi katika lugha ya Kiswahili hivyo inamaana na inawezesha mawasiliano, na sentesi zilizobaki hazijafuata mpangilio sahihi wa kimuundo wa  lugha ya Kiswahili hivyo hazina maana na hazifanikishi mawasiliano.

    

 

Kwa ujumla semantiki ni tawi la isimu kama matawi mengine ya isimu ambalo haliwezi kujikamilisha lenyewe pasipo kuhusiana na matawi mengine ili kukamilisha mawasiliano. Lakini semantiki inaweza kutofautiana na matawi mengine kwa kuanza na tafsiri yake ambayo inajieleza na imetofautiana kabisa kidhima na matawi mengine ambayo ni fonolojia, sintaksia, na mofolojia. Pia dhima zake hazifanani na matawi mengine ya isimu.

 

           

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

          MAREJEO

Habwe, J na P. Karanja (2004). Misingi ya Sarufi ya Kiswahili. Nairobi: Phoenix Publishers Ltd.

Massamba P. B. D (2004) Kamusi ya Isimu na Falsafa ya Lugha. Dar es Salaam: TUKI

 

Massamba, D.P.B na wenzake (1999). Sarufi Miundo ya Kiswahili Sanifu: Sekondari na Vyuo.          Dar essalaam: TUKI.

 

Massamba (2004) anafasili dhana ya semantiki kuwa ni taaluma ya isimu inayojishughulisha na uchunguzi na uchambuzi wa maana za maneno na tungo katika lugha.

Comments

Popular posts from this blog

International Law

KATIBA YA KIKUNDI