TUKI
Kazi yetu imegawanyika Katia sehemu tatu, ambapo Kuna
utangulizi, kiini cha swali na hitimisho. Pia Katika utangulizi tumeelezea
maana ya lugha, Katika kiini cha swali
tumeonyesha jinsi usemitiki wa
lugha ya binadamu unavyojitokeza na mwisho tumemalizia na hitimisho la kazi.
UTANGULIZI
Lugha imeweza kufasiliwa na wataalam mbalimbali
kulingana na uelewa wa kila mmoja kuhusu dhana ya lugha. Baadhi ya wataalam hao
ni kama wafuatao;
Sapir. (1921) anaeleza dhana ya lugha kuwa, ni mfumo
ambao binadamu anajifunza ili atumie
kuwasilisha mawazo na maoni . Anasema mfumo huu hutumia ishara ambazo hutolewa kwa hiari, na anaendelea
kusema kuwa ili binadamu waweze kuwasiliana iliwabidi wabuni mfumo Fulani wa ki ishara ambao
wangetumia kuwasiliana miongoni mwao
katika jamii. Fasili hii ina udhaifu katika kufasili dhana ya lugha
Kwa kuwa
imeegemea zaidi katika matumizi ya ishara na hivyo kuonesha kwamba suala la
sauti halikutiliwa maanani ilihali sauti ndio msingi mkubwa katika lugha.
Pia TUKI (2004), wanatoa fasili kuwa lugha ni
mpangilio wa sauti na maneno unaoleta maana ambao hutumiwa na watu wa kabila au
taifa Fulani kwaajili ya mawasiliano.Tuki nao wana udhaifu katika kueleza maana ya lugha kwani wamejikita zaidi katika kuzingatia suala la
sauti na maneno na kusahau matumizi ya ishara kuwa ni sehemu ya lugha katika
mawasiliano.
Kwa ujumla kutokana na fasili hizo tunaweza kusema
kwamba lugha ni mfumo wa ishara na sauti za nasibu ambazo zimekubaliwa na watu
wa jamii Fulani ili ziweze kutumika katika mawasiliano yao ya kila siku katika nyanja mbalimbali za maisha,
kisiasa, kiuchumi, kijamii na kiutamaduni.
SEMITIKI
Kwa mujibu wa
Lyons,J. (1977), anafasili semitiki kuwa ni sayansi ya alama, ishara au
na mfumo wa mawasiliano.
Pia tunaweza kufasili semitiki kuwa ni taaluma ya
ishara,alama na mawasiliano.
wazo la msingi katika fasili ya semitiki ni matumizi
ya ishara, alama na sauti katika
kukamilisha mawasiliano.
Ferdinand
de Saussure (1974), anaeleza
kuwa ishara ndio kipashio cha kimsingi
cha mawasiliano katika jamii, ambapo yeye aliita ishara ya neno kiashiria na
aliita maana ya ishara hiyo kiashiriwa,dhana au kitajwa.
Mfano.
a) -(kiashiria)
➡️
kipepeo-(kiashiriwa)
b) -(kiashiria) maua-(kiashiriwa)
Uhusiano uliopo baina ya dhana hizi mbili siyo wa moja
kwa moja bali ni wa kidhahania tu. Maana haiwezi kuwepo bila umbo
linalohusIshwa nalo. De Saussure alisisitiza kwamba maana ya neno kama ishara
ya kiisimu hujengwa kutokana na
mahusiano ya maana iliyopo .
Mtu anayejifunza semitiki anakuwa anahusika na mambo
matatu ambayo ni;
i)Semantiki,
yaani uhusiano baina ya ishara,
alama na vitu vinavyorejelewa na ishara hizo.
ii)Sintaksia, hii inahusisha uhusiano baina ya ishara
pamoja na alama katika muundo maalum.
iii)Pragmatiki, ni mahusiano baina ya alama, ishara na
fasili zake kwa watumiaji wa ishara na alama hizo.
USEMITIKI WA LUGHA YA MWANADAMU
Usemitiki wa lugha ya mwanadamu unaweza kuthibitika
kwa kurejelea fasili za wataalam
mbalimbali ambao wameelezea dhana ya lugha
kwa namna ifuatayo;
A)Sapir (1921), ) anaeleza dhana ya lugha kuwa ni
mfumo ambao binadamu anajifunza ili
atumie kuwasilisha mawazo na maoni . Anasema mfumo huu hutumia ishara ambazo hutolewa kwa hiari, na anaendelea
kusema kuwa ili binadamu waweze kuwasiliana iliwabidi wabuni mfumo fulani wa ki- ishara ambao
wangeutumia kuwasiliana miongoni mwao
katika jamii.
B)Barton D. (2004 ),
Lugha ni mfumo wa ishara ambao huunganisha yaliyomo akilini au kichwani
mwa mtu na nje ya mazingira ya kawaida.
Kwa kurejelea fasili za wataalam hao,tunaona vitu vya
msingi vinavyojitokeza ni matumizi ya sauti(maneno) na alama au ishara katika
mawasiliano.
Pia, kwa mujibu wa Charles F. Hockett (1948), usemitiki wa lugha
unatokana na matumizi ya ishara au alama za kinasibu na sauti zitumikazo katika
mawasiliano kama ifuatavyo;
Hivyo basi usemitiki wa lugha ya mwanadamu upo katika
matumizi ya Sauti na alama au ishara katika mawasiliano.
Sauti (maneno); Data za utafiti wa semitiki kiisimu ni
maneno, binadamu wanapowasiliana huweza kutumia maneno au sauti.kwa mujibu wa
Wood,(2019) maneno (sauti) hizo zitumiwazo ni alama za kiisimu(fonetiki),na
hivyo ndivyo unavyotokea usemitiki was lugha ya mwanadamu.
Mfano,I)-kiswahili.
Sauti za
kawaida Alama za sauti hizo kifonetiki
t [t]
d [d]
k [k]
ii)kiingereza:
See/si:/
Say/seI/
Katika mifano hapo juu sauti na maneno
katika lugha huweza kuandikwa kawaida au huweza kuwakilishwa na alama za
kiisimu ambazo kwa kawaida hurejelea kitu kimoja,matumizi ya alama hizo za
kiisimu ndio usemitiki wenyewe.Lakini pia zipo sauti ambazo hazihusishi
matamshi au maneno nazo huashiria kitu husika,mfano ni kupiga mluzi,filimbi na
hata ngoma pia nI njia mojawapo ya kuwasiliana.
Matumizi ya ishara;
Radford pamoja na
Seeger (2008) wanasema, ishara
inahusisha mielekeo na mienendo ya viungo katika mwili wa binadamu, kama vile
mikono, mabega, kichwa, uso na pia sehemu nzima ya mwili badala ya kuhusisha
sauti.Upo uwezekano wa wanadamu kuwasiliana kwa kutumia ishara na wakaelewana
vizuri pasipo kutoa sauti.
Mfano;
Kutikisa mabega, ni ishara ya kukataa kitu au jambo Fulani.
Kupunga mkono, huashiria ishara ya kutoa salamu au kuagana .
Kutikisa kichwa, hii ni ishara ya kukubali au kukataa.
Namna ya uwekaji wa
macho, inaonesha kusitisha au kulificha jambo Fulani lisitamkwe au kitu Fulani
kisifanyike.
Pia uso , unaweza
hali ya kufurahi au kukwazika na jambo
au kutokubaliana.
Matumizi ya alama ;
Usemitiki wa lugha ya mwanadamu pia
unajidhihirisha katika matumizi ya alama
kama nyenzo mojawapo ya mawasliano . Alama hujumuisha kitu, mchoro, au kifaa
ambacho hutambulisha kingine au kutoa tarifa juu ya jambo fulani. Kama vile
tukio au kuonesha sehemu. Alama zinaweza kuwa za kiuandishi au maandishi na
alama za kuchorwa.
a)Alama za maandishi
au uandishi , hizi hujumuisha alama zinazotumika katika uandishi. Mfano
nukta ( . ), alama ya
mshangao ( ! ), alama ya kuuliza ( ? ) na alama zinazoandikwa sehemu mbalimbali
kwa lengo la kutoa taarifa fulani au kuonesha mahali kama vile ofisini, chooni
na kadhalika.
b)Alama za michoro;
Hizi huchorwa kwa lengo la kutoa taarifa
fulani au kuzuia au kukumbusha jambo fulani. Mfano wa alama au michoro ni kama
vile alama za usalama barabarani ambazo zinakusudia kutoa taarifa kwa watumiaji
wa barabarani na kutoa maelezo ili
kuepusha ajali. Pia alama zinazochorwa katika nguo ambazo zinakuwa na lengo la
kumtarifu dobi nguo hiyo ipigwe pasi kwa moto mkali au kwa moto wa kawaida au kwa moto mdogo au isipigwe pasi
kabisa.
Hii ni Alama ya
mshale am ;
bayo unatumika
kuonesha sehemu au mahali mtu anapotaka kwenda kama vile chooni, ofisini na
sehemu nyininezo kutokana na sifa Fulani. Hivyo Katika Alama hutoa taarifa
Fulani pasipo kuhusisha sauti Katika muktadha hiyo.
pembe nane
a)
Simama
kabisa kwenye mstari mweupe, kwenye njia ya wanaopita kwa mguu au usawa wa
kibao. Subiri
b) magari
yapite, na watu wapite kabla ya kuendelea.
c)
Kuna junksheni zingine ni FOUR WAY STOP,
kuna vibao vya kusimama kila kona. Kwenye
junksheni hizo,
d)
lazima
magari yote yasimame kabisa. Kama magari mawili au zaidi yanafika kwa pamoja,
lazima
e)
usimame
kabisa na gari lilipo mkono wako wa kulia ana haki ya kupita kwanza.
Pembe tatu
a)
Lazima
upunguze mwendo, uwe tayari kusimama.
b)
Achie
magari, mabaiskeli na wanaopita kwa mguu wapite kwanza, halafu uendelee.
Pembe nne ndefu, Sheria na Taarifa
a) Kama
kibao kimesimama ina maelekezo ya sheria.
b) Kama
kibao kimelala ina maelekezo ya taarifa.
Pembe nne
a)
Tahadhari,
mabadiliko au hatari iko mbele
b)
Punguza
mwendo na uwe tayari kusimama.
Pembe tano
a) Eneo
ya shule- zinatoa taarifa ya eneo ya wapita kwa mguu karibu na shule
Hitimisho
Kwa ujumla, taaluma ya semitiki ina mchango mkubwa sana
katika lugha ya mwanadamu, haskatika lengo kuu la kurahisisha mawasiliano kwa
mbinu mbalimbali kama vile ishara,alama na sauti,kulingana na mawasiliano
yenyewe na wahusika wa mawasiliano hayo,mfano iwapo wahusika wa mawasiliano
hayo ni bubu au viziwi ishara na alama zitatumika kuwasilisha ujumbe
uliokusudiwa kufikiwa na wahusika hao.
MAREJELEO;
Barton D. (2013), Language
Online Canada; Routledge
Ferdinand de
Saussure, (1974), Course in General Linguistic ; Semiotic London; Sage Publications.
Radford G. & F. Seeger (2008); Semiotics in Mathematics Education;
Epistemology, History, Classroom and
Culture. Serve Publisher
Sapir E.
(1921), Language ; An Introduction to the Study of
speech New York ; Harwat Bracea company Publishers
TUKI, (2004), Kamusi ya Kiswahili Sanifu, Dar-Es-Salaam;
Oxford University Press.
Wood S.K (2019), Sign
Languages Structures and Contexts; Boutledge.
Comments
Post a Comment