KATIBA YA UMOJA WA WANACHUO STEMMUCO


KATIBA YA UMOJA WA MWANACHUO                      STEMMUCO 2018


1.                 JINA NA OFISI
a.                 JINA.
Katiba hii imaandikwa Kwa taratibu za uanzishaji na uendeshaji wa vikundi na itajulikana kama Kikundi cha UMOJA WA WANACHUO STEMMUCO katika Halmashauri/Manispaa ya mtwara mikindani

b.                LUGHA
Lugha rasmi itakayo tumika katika Kikundi hiki ni Kiswahili na kiingereza

c.                  MUHURI
Kikundi hiki cha UMOJA WA WANACHUO STEMMUCO kitakuwa na muhuri ambao utatumika katika nyaraka zote za Kikundi.


2.                 SHABAHA
2.        Kuanzisha na kuendeleza mifuko ya kukopeshana ambayo ni mfuko wa hisa, Jamii na mifuko mingine ambayo wanachama wataridhia kuianzisha ndani ya kikundi hiki.
1.     Kutoa mikopo kwa wanachama kwa masharti nafuu kama mfumo wa vikundi  unavyo eleza.
2.     Kutoa mafunzo ya kina kwa wanakikundi juu ya kuweka fedha, kukopeshana na faida ya kurejesha mikopo kwa wakati.
3.     Kutoa mikopo kwa wanachama kwa riba nafuu
4.     Kuondoa umaskini wa kipato kwa kuhamasiha kukopa na kurejesha mikopo hiyo kwa wakati.
5.     Kuhamsisha wanakikundi kufanya shughuli zingine za kijamii kama vile kutunza mazingira, kuwahudumia watoto yatima, kutoa mafunzo kwa watu wanaoishi na mambukizi ya virusi vya Ukimwi, kudumisha mahusiano ya dini mbalimbali na kudumisha amani na upendo katika jamii.
6.     Kutafuta wafadhili mbali mbali ilikuweza kusaidia maendeleo ya wanachama wa vikundi vya VICOBA.
7.     Kuanzisha na kuendeleza shughuli yoyote ya ki-uchumi na kijamii kwa manufaa ya kikundi kama itakavyo kubaliwa na vikundi vyote.
8.     Kutoa ushauri/elimu ya ki-uchumi, kifedha, kibiashara kilimo, ufugaji na masuala mtambuka kwa vikundi na hata jamii inayotuzunguka.
9.     Kushirikiana na vikundi vingine na kuuanzisha umoja wa kuimarisha nguvu na ushirikiano.
10.                        Kushirikiana na makundi mengine katika kuandaa na kuendesha makongamano na maonyesho mbalimbali ya shughuli na miradi ya wanavikundi.

SEHEMU YA TATU
3.                 MAMLAKA
Kikundi kitakuwa na malaka yote ya kisheria ya kutunza na kulinda fedha za wanachama wa kikundi hiki na hakutakuwa na chombochochote cha juu kitakacho kuwa na uwezo wa kumiliki au kuhodhi sehemu ya mali za kikundi.

Kikundi kitakuwa na mamlaka ya kupokea rasilimali halali kutoka sehemu mbalimbali ikiwemo hisa za wanachama, mfuko wa jamii, bima za mikopo pamoja na riba za mikopo.

Kikundi kitakuwa na mamlaka ya kuwekeza kwenye kitegauchumi chochote na fedha za kuwekeza zitatokana na michango maalumu kutoka kwa wanachama na makusanyo ya kila wiki ambayo ni Hisa na mfuko wa Jamii hazitahusika katika uwekezeji maana ni fedha za mwanakikundi na atatakiwa kurejeshewa pindi  atakapo jitoa.

Kikundi pia kitakuwa na mamlaka ya kupokea msaada wa kifedha, kuingia kwenye makubaliano yoyote ya kukopeshwa au kukopa au kupata msaada kwa kuzingatia kwamba:
a.                 Msaada au mchango wowote ndani ya Kikundi hiki utatumika kwa manufaa ya wanaKikundi tu.
b.                 Hakuna fedha zozote au rasilimali zitatumiaka kwa maslahi ya mtu binafsi
c.                  Kufanya shughuli za maendeleo kwa manufaa ya wanachama
d.                 Kutoa elimu katika jamii kwa faida ya wanachama na wananchi kwa ujumla.




SEHEMU YA NNE

4.                 WANACHAMA
Wanachama wa UMOJA WA WANACHUO STEMMUCO ni watu waliojiunga katika kikundi hiki na ambao watakuwa na jukumu la kufanya shughuli zao zote kwa kufuata kanuni na taratibu za mfumo wa kikundi.

4.1.         SIFA ZA MWANACHAMA
4.1.1.  Awe mwenye umri usio pungua 18+
4.1.2.  Awe mwenye tabia nzuri mwaminifu na akili timamu.
4.1.3.  Awe mwenye uwezo wa kununua hisa angalau moja kila wiki na mwenye uwezo wa kuudhuria mikutano kila wiki
4.1.4.  Awe tayari kufuata sheria na kanuni za kikundi hiki
4.1.5.  Awe mwenye uwezo wa kusimamia mradi wake kikamilifu
4.1.6.  Awe anahudhuria kila mwisho wa mwezi

4.2.         MAOMBI YA UANACHAMA
4.2.1.  Kila mtu atakaye hitaji kujiunga na kikundi hiki  cha umoja wa wanachuo stemmuco  atatakiwa kuandika barua ya kuomba kujiunga na kuwasilishwa kwa mwenyekiti wa kikundi.
4.2.2.  Baada ya maombi kuwasilishwa katika Kikundi, Barua itasomwa na kujadiliwa na wanakikundi wote na mhusika atapewa taarifa kama amekubaliwa au maombi yake yamekatataliwa na sababu zake.
4.2.3.  Mwenyekiti atamjulisha mhusika na kama atakubaliwa atatakiwa kulipia fedha za kujiunga ndani ya mwezi mmoja tu.
4.2.4.  Mwanachama atakayetaka kujiunga atalipia gharama zote za toka chama kimeanza.

4.3.          HAKI ZA MWANAKIKUNDI
4.3.1.  Kushiriki katika shughuli zote za Kikundi kwa kufuata kanuni na taratibu za Kikundi  hii.
4.3.2.  Kuhudhuria na kutoa maoni yake katika mikutano ya Kikundi.
4.3.3.  Kuchagua au kuchaguliwa kuwa kiongozi katika Kikundi hiki
4.3.4.  Kumkataa mwanakikundi anaye taka kujiunga kwa sababu za msingi ambazo atazieleza na zitakazo wasilishwa kwenye mkutano.
4.3.5.  Kushiriki kwenye mikutano yote ya mwaka
4.3.6.  Kushiriki kwenye shughuli na matukio mbalimbali yatakayo andaliwa na Kikundi hiki.
4.3.7.  Mwanachama anahaki ya kujitoa ambapo atarejeshewa 5% ya uanachama wake
4.3.8.   
4.4.         WAJIBU WA MWANAKIKUNDI
4.4.1.  Kulipa kiingilio, kununua hisa kila mwezi, kuchangia mfuko wa jamii kila mwezi, kulipa bima kila anapochukua mkopo, kumdhamini mwanakikundi mwenzake wakati wa kukopa na kulipa deni la mkopaji iwapo atashindwa kulilipa kwa wakati na kwa mujibu wa taratibu za kikundi.
4.4.2.  Kupewa ripoti ya maendeleo ya Kikundi kila mwezi na kila wiki kusoma majina ya wanakikundi wanaotakiwa kurejesha mikopo yao.
4.4.3.  Kushiriki, kusimamia na kuendesha warsha mbalimbali kwa niaba ya wanakikundi, na wananchi kwa ujumla.
4.4.4.  Kuchukua mikopo na kuirejesha kwa muda wa kati ya miezi mitatu, miezi sita na mwaka mmoja.
4.4.5.  Kuhakikisha analipa kiasi cha fedha kila mwezi kama ambavyo mfumo wa kikundi unaelekeza nah ii itwasaidia wengine nao wapate mikopo kwa wakati.



4.1.         UKOMO WA MWANAKIKUNDI
4.1.1.  Mwanachama yeyote atakaye hitaji kujiondoa atatakiwa kuandika barua kwa mwenyekiti wa kikundi na mwenyekiti ataisoma kwa wanacahama na kuomba mawazo yao.
4.1.2.  Mwanachama yeyote atakaye shindwa kutimiza kanuni, taratibu na katiba au aliyeshindwa kulipa michango yake kama wanachama walivyo kubaliana mwanachama huyo atakuwa amejiondoa mwenyewe na mafao yake atapewa ndani ya siku tisini na iwapo anadaiwa kikundi kitapanga utaratibu kwa kushirikiana na wadhamini wake jinsi ya kulilipa deni lake.
4.1.3.  Mwanachama atakaye fariki au kujiondoa atapewa mafao yake ndani ya siku tisini (90) na ambayo ni Hisa na mfuko wa jamii ambazo ni 50%.
4.1.4.  Mwanachama atakaye fukuzwa ndani ya kikundi hiki kutokana na wizi, kutoa siri za kikundi, kusababisha ugonvi, ubishi wa mara kwa mara, kutofuata sheria na kutohudhuria mara nne mfululizo kwenye vikao vya kikundi atakatwa asilimia 20 ya mafao yake kama adhabu na mafao yatakayo salia atakabidhiwa ndani ya siku tisini.
4.1.5.  Mwanachama atakaye kiuka kanuani na taratibu za mfumo wa kikundi kwa kwenda kinyume na mwongozo unaotumika atakuwa amejiondoa.
4.1.6.  Mwanakikundi atakaye ugua zaidi ya miezi sita kitandani atarudishiwa hisa zake na nafasi yake itaachwa wazi hadi mwishoni mwa mwaka wa kikundi. Kama hali yake itaimarika na atapenda kujiunga tena basi mwanakikundi huyo ataruhusiwa.
4.1.7.  Mwanachana atapomaliza chuo atapata  michango yote aliyetoa na faida itakuwa kama sehemu ya mtaji wake
4.5.         KUTEUA MRITHI
4.5.1.  Kila mwanakikundi atamteua mrithi wake ambaye atakuwa na haki ya kulipwa hisa na mafao yote anayo stahili.
4.5.2.  Mwananakikundi anayo haki ya kubadilisha jina la mrithi kila mwaka na kila uteuzi utaandikwa katika daftari la wanachama na mwanachama mwenyewe ataweka sahihi.



SEHEMU YA TANO

5.                 MUUNDO WA UONGOZI NA MAJUKUMU YAKE
a.     Mkutano mkuu
b.     Kamati ya uongozi

5.1.         MKUTANO MKUU
Mkutano mkuu utahudhuriwa na wanachama wote na ambao wanashiriki kwenye shughuli za kikundi na wanazifuata taratibu na kanuni ambazo wamejipangia ilikuwaongoza.

Kutakuwa na kamati ya uongozi ya kikundi ambayo itakuwa na wajumbe watano. Wajumbe hawa ni Mwenyekiti, Katibu, Mweka hazina na Wahesabu fedha wawili. Majukumu yao ni kuongoza kikundi kila siku na kama hawatakuwepo siku ya kikao mwanachama yeyote atateuliwa kushika nafasi iliyo achwa wazi na atasimamia mambo yote na kikao hicho kitatambulika kuwa ni kikao rasmi na halali.

5.2.         MAJUKUMU YA MKUTANO MKUU

5.2.1.  Kuchagua kamati ya uongozi
5.2.2.  Kupitia na kupitisha mipiango ya Kikundi
5.2.3.  Kupitia na kukubaliana juu ya mapendekezo ya maboresho au mabadiliko ya katiba.
5.2.4.  Chombo cha usulihishi zidi ya mambo yote yatakayojitokeza ndani ya Kikundi
5.2.5.  Kutoa ushaari na maelekezo kwa kamati ya uongozi ya kikundi
5.2.6.  Kushughurikia masuala mengine yote yanayo husu kikundi hiki.




5.3.         KAMATI YA UONGOZI
Kamati ya uongozi wa kikundi itaundwa na viongozi watano na ambao ni Mwenyekiti, Katibu, Mwekahazina na Wahesabu fedha wawili. Majukumu yao ni kama ifuatavyo:

5.3.1.  MWENYEKITI
5.3.1.1.      Kuongoza kikundi
5.3.1.2.      Kuwakilisha kikundi kwa watu wa nje na wasio wanakikundi
5.3.1.3.      Kuhakikisha sheria za kikundi zinafuatwa nakuheshimiwa
5.3.1.4.      Kuwashauri wanakikundi
5.3.1.5.      Kutafuta suluhisho la ugomvi miongoni mwa wanakikundi
5.3.1.6.      Kuhitimisha mikutano
5.3.1.7.      Kufungua mikutano na kutangaza agenda
5.3.1.8.      Kutangaza makusanyo yaliyo pita (uwekaji fedha) na baadae kutoa mikopo.
5.3.1.9.      Kuhakikisha usalama wa mali zote za kikundi.
5.3.1.10. Kushirikiana na wajumbe wengine wa kamati ya uongozi kulipa mali pale inapobainika kuwa wao ndio wahusika wa upotevu wa mali hizo.

5.3.2.  KATIBU
5.3.2.1.      Kuandika na kukumbuka shughuli zote zinazofanywa na kikundi katika kila mkutano.
5.3.2.2.      Kuita namba ya wanakikundi wakati wa kununua hisa, uwekaji wa mfuko wa jamii na urejeshaji wa mikopo.
5.3.2.3.      Kutoa taarifa na shughuli za kikundi kwa mwezeshaji wakati wa ufuatiliaji.
5.3.2.4.      Kulipa fedha zinazo potea ikibainika kuwa kamati ya uongozi wa kikundi imehusika.
                
5.3.3.  MWEKAHAZINA
5.3.3.1.      Kuweka fedha za kikundi
5.3.3.2.      Kuhakikisha usalama wa fedha na mali za kikundi
5.3.3.3.      Kutayarisha mahesabu katika sanduku la fedha na kusimamia mienendo yote ya shughuli za kibenki.
5.3.3.4.      Kuhakikisha sanduku limefungwa baada ya mkutano wa kikundi
5.3.3.5.      Kuhakikisha marejesho yanatolewa.
5.3.3.6.      Kutunza kumbukumbu zote za fedha za kikundi
5.3.3.7.      Kugonga mihuri na kujaza reja ya mikopo kila wiki.
5.3.3.8.      Kutoa taarifa ya mapato na matumizi mwisho wa kufunga mwaka wa kikundi.
5.3.3.9.      Kulipa fedha zinazo potea ikibainika kuwa kamati ya uongozi wa kikundi imehusika.






SEHEMU YA SITA

6.                 VYANZO VYA MAPATO NA MIFUKO MIKUBWA
a.                 VYANZO VYA MAPATO
6.a.1.  Michango kutoka kwa wanachama wa Kikundi kwa kulipa kiingilio, Hisa za kila wiki, ruzuku kutoka kwa wafadhili mbalimbali, michango kutoka kwa marafiki na harambee mbalimbali.
6.a.2.  Kupata michango au misaada kutoka kwa watu wasio watanzania.
6.a.3.  Misaada na michango mbalimbali kutoka katika Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na mashirika rafiki.
6.a.4.  Kuuza rasilimali za Kikundi.
6.a.5.  Kupata fedha kutokana na ushauri na mafunzo mbalimbali yatakayo tolewa.


b.                 HISA
6.b.1.  Thamani ya hisa moja ni shilingi 5,000/= Kiwango hiki kitakuwa kinabadilika kila mwaka kutokana na maendeleo ya wanachama wa kikundi.
6.b.2.  Hisa ni mali ya mwanachama kwa hiyo hairuhusiwi kuchukua hisa za wanachama kununulia rasilimali za kikundi.
6.b.3.  Idadi ya chini ya hisa ni moja na idadi ya juu ni hisa tano kila wiki  ya mkutano wa kikundi.
6.b.4.  Kila mwanachama atapewa kitabu cha hisa (excell sheet) na kuingizwa kwenye reja.
6.b.5.  Faida ya kikundi itakayopatikana kutokana na mikopo itakayochukuliwa itagawanywa kwa wanachama kulingana na idadi ya hisa za wanachama. Mwanachama atakaye nunua hisa nyingi atakuwa na faida kubwa na atakaye nunua hisa chache atapata na faida ndogo.
6.b.6.  Iwapo mwanachama ana mkopo, hisa zake hazitaruhusiwa kuchukuliwa hadi amalize deni lake au la mwanachama aliye mdhamini ndani ya kikundi.
6.b.7.  Mwanachama ambaye hatanunua hisa katika kikundi atatakiwa kulipa faini sh 2000/=
6.b.8.  Vitabu vya hisa vitakuwa na namba zinazo fuatana na mwanachama atajulikana kwa namba katika Leja ya kikundi.
6.b.9.  Fedha zitakozowekwa kwenye kikundi zitaletwa na mwanachama husika au mwanachama mwenzake. Mtu ambaye siyo mwanachama hataruhusiwa kushiriki kwenye zoezi la kibenki ndani ya kikundi
6.b.10.                     Kitabu cha hisa hakina budi kionyeshwe wakati wote wa kununua hisa au wakati wa kuchukua mkopo.
6.b.11.                     Mkopo utatolewa mara tatu tatu ya hisa za mwanachana lakini kwa kuangalia idadi ya wakopaji mwezi huo na fedha zilizopo na uhitaji wa mwanachama.


c.                  BIMA YA MIKOPO YA KIKUNDI
Kila mwanacha atatakiwa kutoa 2% ya mkopo wake ilikuukinga mkopo wake dhidi ya janga la Kifo au ulemavu wa kudumu. Mfuko huu utakuwa na jukumu la kuhudumia janga litakalotokea baada ya mwanachama kukopa mkopo wa kuendeshea biashara/mradi.

Mwanachama akifariki au kupata ulemavu wa kudumu ambao utamfanya asiweze kuendelea na shughuli za kikundi, deni lake litafidiwa na mfuko bima ya kikundi na malimbikizo yake ya Hisa na mfuko wa jamii atakabithiwa mrithi wake.

Mwanakikundi akijitoa hatarejeshewa mfuko wa bima kwa kuwa mfuko huu utaendelea kulinda madeni miaka hadi miaka na iwapo kikundi kitavunjika basi mfuko wa Bima atachanganywa na ziada ya mikopo na kugawanywa kama gawio kwa wanahisa wote.


d.                 MFUKO WA JAMII
Kila mwanachama atachangia shilingi 5,000/= kwa ajili ya mfuko wa jamii na ambao utatoa mikopo ya sherehe,kufiwa na afya. Mfuko huu utakopeshwa kwa wanachama kutokana na matatizo ya afya pamoja na matatizo ya elimu. Mfuko huu utakopeshwa kwa muda wa miezi mitatu na mkopaji atarudisha mkopo huo bila ziada/riba ya mkopo kwenye kikundi chake kila mwezi.

Kikundi kitapanga kiwanga cha juu cha kukopeshana na kiwango hiki kitakuwa kina badilika miaka hadi miaka kutokana na kukua kwa mfuko wenyewe au kuongezeka kwa michango ya kila wiki. Mfuko huu ni mali ya wanachama na iwapo mwanachama atajiondoa katika kikundi fedha zote alizochangia katika mfuko huu atarejeshewa pamoja na mfuko wa Hisa.



SEHEMU YA SABA

7.                 AKAUNTI NA VITABU VYA FEDHA
7.1.         Fedha zote zitakazo pokelewa na kikundi zitahifadhiwa kutokana na mfumo wa kikundi unavyo eleza na kikundi kitakuwa na akaunti katika benki.
7.2.         Fedha zote za Kikundi hiki zitatumika katika kukopesha wanachama, kusaidia katika matatizo ya dhararu na kuwarudishia wanachama hisa zao wote ambao wamajitoa katika kikundi.
7.3.         Fedha zote zitakazo pokelewa na kutolewa zitakuwa zinaingizwa kwenye excel sheet.
7.4.         Mwezeshaji atashirikishwa kwenye jambo lolote litakalo fanyika ndani ya kikundi hasa kwa ushauri na hii itatokea kutokana na uelewa wake mpana wa uendeshaji wa vikundi hivi vya kikundi.
7.5.         Fedha zote zitakazo potea wahusika watawajibika kuzilipa kutokana na mazingira ya wizi ulivyojitokeza.
7.6.         Mwaka wa fedha wa kikundi hiki utakuwa ni mwezi Semptemba, tarehe 30 ambapo wanachama watagawana faida na kufanya tafrija ndogo ya kupongezana jumapili ya mwisho wa mwezi september.
7.7.         Kikundi kitaweka kumbukumbu zote za fedha ikiwemo ripoti za fedha na za miradi na kuwasilishwa kwa wanachama kila mwisho wa mwaka wa fedha.

7.8.         Akaunti ya kikundi itafunguliwa na wajumbe watatu. Kati ya wajumbe hawa wajumbe wawili wataruhusiwa kutoa fedha za kikundi baada ya kupitishwa katika kikao na wanachama kuidhinisha utoaji wa fedha hizo za kikundi.







SEHEMU YA NANE

8.                 KUVUNJIKA KWA  KIKUNDI
8.1.         Kikundi hii kinaweza kunvunjwa kwenye mkutano mkuu wa wanachama wote iwapo theluthi mbili ya wanachama wakipiga kura.
8.2.         Wakati wa kuvunjwa rasilimali zote ikiwemo mali na fedha zitagawanywa kwa kila mwanachama kama alivyo changia na zitakzo baki zitagawiwa kama gawio la faida.


SEHEMU YA TISA

9.                 MABADILIKO YA KATIBA
a.                 Baada ya katiba hii kukubalika na kupata usajili wa kisheria hakuna mwenye ruhusa ya kubadilisha katiba hii bila idhini ya wanachama wa kikundi hiki.
b.                Mabadiliko yoyote yatakayotakiwa kufanyika katika katiba hii kamati ya uongozi wa kikundi itayawasilisha kwenye ofisi ya maendelo ya wilaya.
c.                  Maboresho yakikubalika wajumbe watatakiwa kupiga Kura na thelusi mbili wakikubali basi katiba hiyo itatakiwa kufanyiwa maboresho.


SEHEMU YA KUMI

10.            MAKOSA MBALIMBALI NA ADHABU ZAKE.

10.1.    Mwanachama atakaye ongea ndani ya mkutano bila ruhusa ya mwenyekiti atatozwa faini ya TSH 2,000/= Na kiwango kitapangwa na kikundi na kitakuwa kinabadilika mara kwa mara.

10.2.    Mwanachama ambaye simu yake itaita kwa sauti na kusababisha kuharibu kwa mazingira ya utulivu atalipa faini ya tsh 2,000/=  na kiwango kitakuwa kinabadilika mara kwa mara.

10.3.    Mwanachama atakaye chelewa kufika kwenye mkutano wa kikundi kama ilivyo kubaliwa na wanachama wote bila taarifa atatozwa faini ya  Tsh 5,000/= ili kulinda nidhamu na kuhakikisha shughuli za kikundi zinafanyika kwa muda uliopangwa,kutohudhuria bila tarifa 10,000/=,tsh 2,000/= kama ametoa taarifa



Michango mbalimbali
10.4.    Mwanakikundi atakaye fariki dunia katika kikundi cha UMOJA WA WANACHUO STEMMUCO atachangiwa kwa kadiri wanachama watakavyokubaliana. Fedha hizo atakabidhiwa mrithi wake wake pamoja na mafao mengine ambayo ni Hisa na jamii.

10.5.    Mwanachama yeyote atakeye fiwa na Mume, mke na  watoto/tegemezi wake kama alivyoandikia majina yao katika daftari la tegemezi atachangiwa na kila mwanachama wa kikundi hiki.

10.6.    Michango mingine ni katika sherehe ambazo ni ndoa, harusi, sendoff, kitchen party, graduation, ubatizo, vipaimara na komuniyo.

















NB :

TAFSIRI:
2.1
Umoja wa wanachama ambao wana lengo moja, wameamua na wako tayari kuwa pamoja kwenye maswala mbalimbali ya maendeleo.  Ni chombo huru na cha hiari chini ya sheria na taratibu za nchi.
Association



2.2
Uongozi uliochaguliwa kukiongoza chama na mkutano wa wanachama kwenye Mkutano Mkuu na wanachama wote wa Association.
Kamati



2.3
Mkusanyiko wa wanachama wote wa Association kwa uwiano utakaotokana na makubaliano ya pamoja katika Association kutokana na idadi ya wanachama katika maeneo ya uwakilishi.
Mkutano Mkuu



2.4
Mwanachama mmoja mmoja ambaye amelipa kiingilio kwa mujibu wa makubaliano ya wana Association wote.


Mwanachama
2.5
Maswala na mahitaji ya msingi yanayogusa wanachama kama msingi wa uanzishaji wa Association kwa niaba na ridhaa ya wanachama wenyewe au yanayohitaji msaada wa pamoja wa Association


Huduma
2.6
Akiba ni fedha anayoweka mwana Association kwenye mfuko wa pamoja na ni fedha inayomsaidia mwana Association/ chama kujipatia mkopo pale ambapo association itaamua kutoa huduma ya mikopo.

Akiba



                    
2.7
Ada ni fedha inayotolewa na mwanachama kila mwezi ili aweze kutambulika kama mwanachama hai.

Ada
2.8
Hisa ni umiliki wa sehemu ya investment ( ) inayofanywa na Association au biashara yoyote inayofanywa ndani ya association.
Hisa
2.9
Mwanachama hai ni yule aliyelipa kiingilio na anatoa ada kila mwezi na kulipa michango mingine na kushiriki kikamilifu kwenye shughuli zilizowekwa kwa makubaliano ya zaidi ya ½ ya wanachama wote.
Mwanachamai hai










Comments

Popular posts from this blog

Information technology

MKATABA WA KUPANGA NYUMBA

Unominishaji,