semantiki ni msingi wa taaluma nyingine za isimu”Thibitisha kauli hi kwa mifano bayana ya kiswahili.
CHUO
KIKUU KISHIRIKI CHA STELLA MARIS MTWARA
(Chuo
Kishiriki cha Chuo Kikuu cha Mtakatifu Agustino - Tanzania)
KITIVO
CHA ELIMU NA SAYANSI
IDARA: ELIMU
KITENGO: KISWAHILI
MSIMBO WA KOZI: SW
323
JINA LA KOZI SEMANTIKI
YA KISWAHILI
MHADHIRI: HAONGA,
E
AINA YA KAZI: KAZI YA KIKUNDI
TAREHE YA KUWASILISHA: 03/05/2021
WASHIRIKI:
NAMBA |
MAJINA |
NAMBA
ZA USAJILI |
SAHIHI |
1 |
MONICA ZAKARIA |
STE/BAED/164093 |
|
2 |
LILIAN M COSTA |
STE/BAED/164229 |
|
3 |
JUDITH J KOMBA |
STE/BAED/165199 |
|
4 |
AILEN A MUGANDA |
STE/BAED/164460 |
|
5 |
GASPA D SINKALA |
STE/BAED/165206 |
|
SWALI: “semantiki
ni msingi wa taaluma nyingine za isimu”Thibitisha kauli hi kwa mifano bayana ya
kiswahili.
Kazi hii
imegawanyika katika sehemu kuu tatu, sehemu ya kwanza ni utangulizi kuuleza
dhana ya semantiki kwa mujibu wa wataalamu mbali mbali, sehemu ya pili ni kiini
cha kazi kuueleza umusingi wa semantiki kwa matawi mengine na sehemu ya tatu ni
hitimisho la kazi kwa ujumla.
Massamba (2004:75)
anafasili dhana ya semantiki kuwa ni taaluma ya isimu inayojishughulisha na
uchunguzi na uchambuzi wa maana za maneno na tungo katika lugha. Semantiki
imegawanyika katika makundi manne ambayo ni leksika, mantiki, muundo na
nadharia.
hata hivyo hakuna ufafanuzi wa kutosha kuhusu maana
ingawa katika hali ya kawaida tunaishia kutoa sifa za kitu na siyo maana.
Kwa mujibu wa Crystal, D (1987) semantiki ni utanzu wa
isimu unaochunguza maana katika lugha. Kwa mukhtasari, semantiki hutalii maana
katika vipashio vyote vya kiisimu katika viwango vyote vya lugha mathalan
fonolojia, mofolojia na sintakisia.
Aidha, semantiki inaweza kufasiliwa kwa namna
mbalimbali jinsi ifuatavyo:
Maana anuwai za dhana ya semantiki
1. Semantiki
ni stadi ya maana
2. Semantiki
ni utanzu wa isimu unaongalia maana ya maana.
Kwa mujibu wa
Leech (1981). Semantiki ni taaluma katika isimu ambayo hushughulikia
maana ya maumbo au sentensi katika lugha. Taaluma hii ilianza enzi za Aristotle
na Plato ambao walizingatia zaidi sifa za maana, katika kipindi hicho walitaka
kujua sifa na tabia za maana.
Habwe na Karanja wakimnukuu Richard na Wenzake (1985)
wanasema “Semantiki ni stadi ya maana. Semantiki ni utanzu unaochunguza maana
katika lugha ya mwandamu”. Wanaendelea kusema semantiki hutafiti maana za
fonimu, mofimu, maneno na tungo. Hivyo kutokana na fasili hii maana
hushughulikiwa katika vitengo au viwango vyote vya lugha ambavyo ni fonolojia,
mofolojia na sintaksia.
Hivyo maana zilizotolewa na wataalamu hapo juu Zina
upungufu.
Wanaeleza maana
ya semantiki bila kuzingatia viwango vinavyokamilisha lugha Kama vile maana
kiwango Cha neno , kiwango Cha tungo,na matini nzima.
Hivyo kutokana na maana zilizotolewa na wataalamu
mbali mbali hapo juu wanakundi tumetoa maana ya semantiki kuwa,
Semantiki.ni utanzu wa isimu ambao unajishugulisha na
uchunguzi,uchambuzi na kutafiti maana za lugha ya binadamu kutoka kiwango Cha
neno mpaka kiwango Cha tungo na matini nzima.
Hivyo kwa
ujumla Semantiki ni taaluma katika isimu
ambayo hushughulikia maana ya maumbo au sentensi katika lugha. Taaluma hii
ilianza enzi za Aristotle na Plato ambao walizingatia zaidi sifa za maana,
katika kipindi hicho walitaka kujua sifa na tabia za maana. Hii inamaanisha
kwamba semantiki hutalii maana katika vipashio vyote vya kiisimu katika viwango vyote vya lugha yaani fonolojia,
mofolojia na sintakisia.
Kwa sababu hii ni sawa kusema kuwa maana
hujishugulikiwa katika tanzu za isimu Kama fonolojia ,mofolojia,na sintaksia
.semantiki inakuwa ndio makutano ya taaluma nyingine
Semantiki kama taaluma nyingine ina mahusiano na
taauma nyingine kama ifuatavyo katika mchoro na hatimaye katika maelezo yanayo
eleza vipengele mbalimbali vya lugha:-
Mchoro kuonesha
mahusiano ya semantiki na vipengele vingine vya lugha kama
sintaksia,mofolojia na fonolojia.Kuwepo kwa semantiki katikati inamaana kwamba
tawi hili ni muhimili wa matawi mengine.
Fonolojia ni
tawi la isimu ambalo hujishughulisha na uchunguzi na uchambuzi wa mfumo wa
sauti katika lugha, huchunguza jinsi ambayo vitamkwa au sauti za lugha
zinavyoungana ili kujenga maneno yanayokubalika katika lugha ya mawasiliano.
Ili lugha ya mawasiliano iwe kamili ni dhahiri kwamba mpangilio wa sauti lazima
uwe na maana ili kufikisha ujumbe, hivyo semantiki inauhusiano mkubwa na
fonolojia.kwani katika fonolojia uweza kuangazia foni na kuziunganisha kupata
kiseme kinacho zungumzwa na kuleta maana mfano wa foni zinavyotengeneza kiseme
chenye maana,[b]+[a]+[b]+[a]= #baba#
[s]+[h]+[u]+[l]+[e]= #shule# sauti hizo zikiwa pwekepweke haziwezi
kuleta maana ndipo ukaribu wa taaluma sauti na taaluma maana unapokutana.
Mofolojia ni
taaluma inayoshughulikia vipashio vya lugha katika kuunda maneno. Tawi hili la
isimu huchunguzi na kuchambuzi wa maumbo ya maneno na jinsi maumbo hayo
yanavyotumika katika lugha. Jukumu la mofimu husika katika sentensi hubainika
vyema kulingana na uhusiano baina ya maneno mengine katika tungo. Maumbo ya
kimofolojia huathiri vipengele vingine vya kisemantiki. Hivyo semantiki ina
mahusiano na taaluma ya mofolojia kwa kuwa ili lugha iweze kueleweka lazima iwe
na mpangilio na muundo mzuri wa vipashio vya sentensi ili kuleta maana katika
mawasiliano.
Mfano:
Mwalimu anaimba
Walimu wanaimba
Katika mfano huu katika upande wa kiima kiambishi m
kinaashiria umoja na wa inaashiri wingi, katika upande wa kiarifu viambishi a katika
upande wa kiima vinaashiria nafsi ya tatu umoja na wa vinaashiria nafsi ya tatu
wingi, hivyo maumbo ya maneno lazima yawe na maana.
Sintaksia, ni
utanzu wa sarufi unaojihusisha na uchunguzi wa mpangilio wa maneno katika
sentensi na uhusiano wa vipasho vyake. Utanzu huu huchunguza sheria au kanuni zinazofuatwa katika kuyapanga
maneno ili yalete maana inayokubalika na kueleweka katika lugha husika, . Kwa
mantiki hii, kwa kuwa semantiki hushughulikia viwango vyote vya lugha, basi
hushughulikia pia kiwango cha sintaksia ambapo huangalia maana za neno sentensi
na tungo kwa ujumla kwani tungo lazima ikubalike kwa wazungumzaji pia tungo
lazima ilete maana.
Kwa
mfano,
Pana huimba vizuri akiwa mubashara
Mubashara huimba vizuri akiwa pana.
Vizuri huimba pana akiwa mubashara.
Katika mifano hii sentensi (1) inampangilio sahihi
katika lugha ya Kiswahili hivyo inamaana na inawezesha mawasiliano, na sentesi
zilizobaki hazijafuata mpangilio sahihi wa kimuundo wa lugha ya Kiswahili hivyo hazina maana na
hazifanikishi mawasiliano.
Kutokana na uwanja mkubwa wa semantiki imeweza
kuibua taaluma zingine ambazo zipo ndani
ya semantiki nazo ni isimu ubongo na isimu jamii hivvyo tutaeleza isimu chache
kwenye hii kazi kea sababu swali linataka tuangalie msingi wa semantiki katika
taaluma zingine.
Isimu ubongo
ni tawi la isimu linalochunguza mahusiano kati ya lugha na michakato ya kiakili
(ubongo) uzashaji wa matammshi katika ujifunzaji wa lugha msingi mkubwa katika
tawi hili la isimu ni kuwa mchakato wa uzungumzaji huanza ktk akili ya mtu,
hivvyo kinacho zungumzwa uleta mahusiano makubwa na semantiki ambalo uchunguza
na kuchambua maana ya kile kinacho zungumzwa na msikilizaji unatambua maana ya
kile kinacho zungumzwa na mtu kutoka kwenye ubongoni mwake.mfano juma amesafiri
leo asubuhi.sentensi inapotoka akilini mwa mtu utengeza maana amboyo
msikilizaji unatambua maana ya kile kinacho zungumzwa na mtoa kiseme.hivyo
semantiki ni makutano ya matawi ya isimu katika lugha.
Kwa mujibu
wa Matinde R S akimurejelea Mathooko,P.(2000)
Isimu jamii.ni tawi la isimu linalochunguza namna lugha inavyotumika
katika jamii kwa kuzingatia mazingira (muktadha) husika ambapo kile kinacho
zungumzwa ni lazima kiendana na mazingira ambapo semantiki huusika kwa lengo la
kuhakikisha kile kinacho zungumzwa kinaendana na mazingira (muktadha) kwa
watumiaji na waweze kuelewana, mazungumzo baina ya watu uzungumzwa kwa
kuzingatia maana ya kile kinacho zungumzwa.mfano juma anakamua mbuzi
maziwa.muktadha wa zizini
Asha anakuna Nazi kwa
kutumia mbuzi. Muktadha wa jikoni katika mapishi.hivyo neno mbuzi limetuka
katika muktadha zaidi ya moja kwa kuzingatia muktadha inaleta maana ya kile
kinacho zungumzwa.
Kwa ujumla semantiki ni tawi la isimu kama matawi mengine
ya isimu ambalo haliwezi kujikamilisha lenyewe pasipo kuhusiana na matawi
mengine ili kukamilisha mawasiliano. Lakini semantiki inaweza kutofautiana na
matawi mengine kwa kuanza na tafsiri yake ambayo inajieleza na imetofautiana
kabisa kidhima na matawi mengine ambayo ni fonolojia, sintaksia, na mofolojia.
Pia dhima zake hazifanani na matawi mengine ya isimu.
MAREJEO
Habwe, J na P. Karanja (2004). Misingi
ya Sarufi ya Kiswahili.
Nairobi: Phoenix Publishers Ltd.
Massamba (2004) Anafasili dhana ya semantiki kuwa ni taaluma
ya isimu inayojishughulisha na uchunguzi
na uchambuzi wa maana za maneno na tungo katika lugha.
Massamba P. B. D
(2004) Kamusi ya Isimu na Falsafa ya
Lugha. Dar es Salaam: TUKI
Massamba, D.P.B na wenzake (1999). Sarufi Miundo ya Kiswahili Sanifu:
Sekondari na Vyuo. Dar essalaam: TUKI.
Leech, G (1981), Semantics, Harmondsworth:
Penguin books limited hazel Watson & veney
Ltd.
Mofolojia
Comments
Post a Comment